Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kulinda Utambulisho Wetu wa Kikristo
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Februari 15
    • 4. Yesu alikaziaje uhitaji wa kulinda utambulisho wetu wa Kikristo ulio wazi?

      4 Hata hivyo, tukiwa watumishi wa Yehova waliojiweka wakfu, tunatambua kwamba lingekuwa jambo la kuhuzunisha kwa yeyote kati yetu—kijana au mzee—kupoteza utambulisho wetu wa Kikristo. Kuwa na maoni yanayofaa kuhusu utambulisho wa Kikristo kunaweza kutegemea tu viwango vya Yehova na mambo anayotarajia kutoka kwetu. Hiyo ni kwa sababu tumeumbwa kwa mfano wake. (Mwanzo 1:26; Mika 6:8) Biblia inafananisha utambulisho wetu wa Kikristo ulio wazi na mavazi ya nje, yanayovaliwa ili kuonwa na wote. Kuhusu nyakati zetu, Yesu alionya hivi: “Tazama! Ninakuja kama mwizi. Mwenye furaha ni yule anayekaa macho na kutunza mavazi yake ya nje, ili asipate kutembea akiwa uchi na watu waitazame aibu yake.”a (Ufunuo 16:15) Hatungependa kuvua sifa zetu za Kikristo na viwango vya mwenendo na kuruhusu ulimwengu wa Shetani utufinyange. Ikiwa jambo hilo lingetokea, tungepoteza ‘mavazi hayo ya nje.’ Hali hiyo ingekuwa yenye kusikitisha na yenye kuaibisha.

  • Kulinda Utambulisho Wetu wa Kikristo
    Mnara wa Mlinzi—2005 | Februari 15
    • a Huenda maneno hayo yakarejelea kwa njia isiyo ya moja kwa moja kazi za ofisa wa hekalu la mlimani huko Yerusalemu. Wakati wa makesha ya usiku alitembea hekaluni ili kuona ikiwa walinzi Walawi walikuwa macho au walikuwa wamelala mahali pao pa kazi. Mlinzi yeyote aliyepatikana amelala alipigwa kwa kijiti, na huenda mavazi yake ya nje yalichomwa kama adhabu ya kumwaibisha.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki