Wimbo Na. 74
Shangwe ya Yehova
Makala Iliyochapishwa
1. Twaziona ishara za Ufalme.
Twajulisha watu wote.
Inueni vichwa, wokovu waja.
Wakati wakaribia!
(KORASI)
Shangwe ya Yehova ngome yetu.
Imbeni, shangilieni.
Furahieni tumaini lenu,
Musifuni Yehova Mungu.
Shangwe ya Yehova ngome yetu.
Jina lake litangazwe.
Tufanye mapenzi ya Mungu wetu.
Na tufurahie huduma.
2. Enyi nyote, tegemeeni Mungu.
Musihofu, ana nguvu.
Simameni na kupa’za sauti;
Na tumwimbie Yehova!
(KORASI)
Shangwe ya Yehova ngome yetu.
Imbeni, shangilieni.
Furahieni tumaini lenu,
Musifuni Yehova Mungu.
Shangwe ya Yehova ngome yetu.
Jina lake litangazwe.
Tufanye mapenzi ya Mungu wetu.
Na tufurahie huduma.
(Ona pia 1 Nya. 16:27; Zab. 112:4; Luka 21:28; Yoh. 8:32.)