Wimbo Na. 44
Kuyashiriki Mavuno kwa Furaha
Makala Iliyochapishwa
1. Twaishi siku za mavuno,
Pendeleo kubwa muno.
Malaika ni “wavunaji.”
Twashiriki utendaji.
Yesu aongoza shambani;
Tunamwiga hudumani.
Tuna pendeleo kubwa sana,
Tufanye kazi ya Bwana.
2. Mungu, jirani, tukipenda,
Tutachochewa kutenda.
Tuna kazi muhimu sana,
Mwisho u karibu sana.
Tuzidipo kufanya kazi,
Shangwe y’onekana wazi.
Kazi ya Ufalme tushiriki,
Mungu atatubariki.
(Ona pia Mt. 24:13; 1 Kor. 3:9; 2 Tim. 4:2.)