Wimbo Na. 107
Njooni Kwenye Mlima wa Yehova
Makala Iliyochapishwa
1. Tazama uone,
Mulima wa Yehova.
Uko, juu zaidi,
Kuliko mingine.
Kutoka dunia,
Watu wapiga mwendo.
Nao waita wengi,
Wamwabudu Mungu.
Mudogo, munyonge,
’takuwa taifa hodari.
Twapiga hatua,
Yehova anatubariki.
Umati mukubwa,
Unajiunga nasi.
Nao waukubali
Ufalme wa Mungu.
2. Agizo tunalo,
La kuhubiri Neno.
Nasi tunatangazia
wote Ufalme.
Kristo atawala,
Awahimiza wote.
Pote duniani
Wamusikie Yeye.
Neno la Yehova,
Linawafungulia njia.
Tunayo furaha,
Kuwasaidia wengine!
Sote tushiriki
Kwa kuwasaidia
Watu wajue Mungu
Wapate uzima.
(Ona pia Zab. 43:3; 99:9; Isa. 60:22; Mdo. 16:5.)