Wimbo Na. 29
Kutembea kwa Utimilifu
Makala Iliyochapishwa
1. Nihukumu, Nakutumaini;
Na utimilifu wangu uchunguze.
Nichunguze na unijaribu;
Nisafishe moyo, na unibariki.
(KORASI)
Ee Yehova, Nimeazimia
Siku zangu zote, kuwa mwaminifu.
2. Sikuketi na watu waovu.
Nimelichukia kutaniko lao.
Nafsi yangu usiiondoe
Nao wapendao rushwa na ugomvi.
(KORASI)
Ee Yehova, Nimeazimia
Siku zangu zote, kuwa mwaminifu.
3. Nyumba yako naipenda sana.
Na ibada yako, naunga mukono.
Nizunguke madhabahu yako,
Nitangaze kote kazi zako zote.
(KORASI)
Ee Yehova, Nimeazimia
Siku zangu zote, kuwa mwaminifu.
(Ona pia Zab. 25:2.)