Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w15 7/1 uku. 16
  • Majibu ya Maswali ya Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Majibu ya Maswali ya Biblia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari Zinazolingana
  • Majibu ya Maswali ya Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Majibu ya Maswali Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Je! Wema Utapata Kuushinda Uovu Wakati Wowote?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1993
  • Majibu ya Maswali ya Biblia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 7/1 uku. 16

MAJIBU YA MASWALI YA BIBLIA

Uovu unatokana na nini?

Yesu akipinga jaribu la Ibilisi la kumpa falme zote za ulimwengu

Ni nani aliyemjaribu Yesu ili atende uovu?—mathayo 4:8-10

Kwa kawaida, watu hupenda kuwa wenye amani, unyofu, na fadhili. Hata hivyo, kwa nini kuna jeuri, ukosefu wa haki, na ukatili? Ni jambo la kawaida kusikia taarifa za habari zinazotisha. Je, kuna mtu fulani anayewachochea watu kutenda maovu?—Soma 1 Yohana 5:19.

Je, Mungu alimuumba mwanadamu akiwa na mwelekeo wa kutenda maovu? Hapana, Yehova Mungu aliwaumba wanadamu kwa mfano wake, wakiwa na uwezo wa kuiga sifa ya Mungu ya upendo. (Mwanzo 1:27; Ayubu 34:10) Hata hivyo, Mungu alimpa pia mwanadamu uhuru wa kuchagua. Wazazi wetu wa kwanza walipochagua kutenda uovu, walikataa kumwiga Mungu na hivyo wakawa watenda dhambi. Tumerithi mwelekeo wa kutenda dhambi kutoka kwao.—Soma Kumbukumbu la Torati 32:4, 5.

Je, uovu utaendelea kuwapo?

Mungu anataka tupinge mielekeo mibaya. (Methali 27:11) Hivyo, anatufundisha jinsi ya kuepuka kufanya yaliyo mabaya na jinsi ya kupata furaha ya kweli. Kwa sasa, hatuwezi kuiga upendo wa Mungu kikamili.—Soma Zaburi 32:8.

Ingawa leo kuna uovu mwingi, Mungu ameacha hali hiyo yenye kuhuzunisha kwa kipindi fulani tu cha wakati ili watu waone matokeo ya kutotii. (2 Petro 3:7-9) Hata hivyo, hivi karibuni dunia yote itajawa na wanadamu wenye furaha wanaomtii Mungu.—Soma Zaburi 37:9-11.

Kwa habari zaidi, ona sura ya 3 ya kitabu Hiki, Biblia Inafundisha Nini Hasa?, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Pia kinapatikana kwenye www.jw.org/sw

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki