Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yb88 kur. 66-135
  • Ailandi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ailandi
  • 1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Vichwa vidogo
  • KITO CHA ZUMARIDI
  • C. T. RUSSELL AWASHA CHECHE YA UKWELI
  • UKOSEFU WA UMOJA KATIKA WAZO
  • ROHO YA KUTAKABARI KATIKA DUBLIN
  • KATIKA AILANDI KASKAZINI
  • KUFUNGUA MACHO KWA DRAMA YENYE PICHA
  • UKWELI JUU YA MOTO WA MATESO
  • “TANGAZENI . . . MFALME NA UFALME WAKE”
  • KUPEPETA KATIKA BELFAST
  • HOTUBA ZA RUTHERFORD ZAONGEZA KICHOCHEO
  • KUTIWA NGUVU NA MIUNGANISHO YA REDIO NA SIMU
  • UPINZANI WENYE KUENDELEA KATIKA KUSINI
  • JEURI ZAIDI KUTOKA KWA WAPINZANI WA KIDINI
  • HIMAYA YA YEHOVA KATIKA KASKAZINI
  • YEHOVA AANDAA
  • RIZIKI YA CHAKULA CHA KIROHO WAKATI WA VITA
  • WATENDEWA KWA DHIHAKA
  • KUPAINIA KATIKA ILE JAMHURI
  • JEURI YA WATU WENYE GHASIA KATIKA CORK
  • UPINZANI WENYE KASIRANI WAENDELEA
  • MASIKIO YENYE KUITIKIA KATIKA DUBLIN
  • JAMAA YA KIKATOLIKI YAITIKIA
  • WAMISIONARI WAONGEZA KICHOCHEO
  • WAMISIONARI WAVUNJA KIZUIZI CHA KIKATOLIKI
  • SHAMBULIO LA WATU WENYE GHASIA KARIBU LIMERICK
  • VIWANGO MARADUFU VYENYE KUFADHAISHA
  • “NJIA YA MUNGU NI UPENDO”
  • HATIMAYE—JUMBA LA UFALME KATIKA DUBLIN!
  • AFISI YA TAWI YAANZISHWA
  • KUSHINDWA KWA JUMUIYA YA WAKRISTO KWAKAZIWA
  • WASHAMBULIWA NA WATU WENYE GHASIA KATIKA WEXFORD
  • KUWAPO KWA MAPAINIA KWAHISIWA
  • MKUSANYIKO WA KIMATAIFA—DUBLIN, 1965
  • KUSHINDA VIZUIZI VYOTE
  • KUFAULU KWELI KWELI
  • AILANDI YOTE CHINI YA TAWI MOJA
  • KUTOKUWAMO IJAPOKUWA MIKAZO
  • KUJIFUNZA KUISHI PAMOJA NA TAABU
  • KWENDA KOTE KOTE PAMOJA NA HABARI NJEMA
  • UTAMBULISHO WENYE KOSA
  • WATAMBULIWA KUWA MASHAHIDI
  • MASIKIO YENYE KUITIKIA KATIKA MAENEO YA KIKATOLIKI
  • KUONA ULE UVUMBUZI HALISI WA ZILE TAABU
  • YEHOVA AENDELEA KUIFANYA IKUE
  • UKUZI WENYE KUENDELEA KATIKA ILE JAMHURI PIA
  • KUTUMIKIA AMBAKO UHITAJI NI MKUBWA ZAIDI
  • UASI-IMANI MARA NYINGINE TENA KATIKA DUBLIN
  • “KITABU CHANGU CHA HADITHI ZA BIBLIA” KATIKA KIAIRISHI
  • MPANUKO NA UTENDAJI WENYE KUONGEZEKA WA UJENZI
  • MAJUMBA YA UFALME YENYE KUJENGWA KWA HARAKA
  • MATAZAMIO MAANGAVU YA MAVUNO
1988 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
yb88 kur. 66-135

Ailandi

“WAKATI wa zile Enzi za Giza,” Ailandi “ilikuwa ‘kile kisiwa cha watakatifu na wanachuo’ ambacho kiliendeleza ile nuru ya elimu ya Kikristo iking’aa wakati ilipokuwa ikizimwa kwingineko,” akaandika Donald S. Connery katika kitabu chake The Irish. Hata hivyo, ile miale ya elimu ya kweli ya Kikristo iliwaka kwa uangavu katika Ailandi baada tu ya miaka ya utendaji wa uaminifu na juhudi upande wa watumishi wa Yehova. Hadithi ya ushindani wao dhidi ya upinzani usiokoma na uhasama wenye kuendelea husimama ikiwa ushuhuda wa imani yao thabiti na kupiga moyo konde, pamoja na upendo wao wenye kina kwa Yehova na wale watu ambao wao walijaribu kusaidia. Ni nani hawa watumishi wa Yehova na hadithi yao ni ipi?

Watu wanaozidi kidogo tu 5,000,000 ndio wanaoishi katika Ailandi. Hawa wametenganishwa vibaya sana na mawazo ya kisiasa na chuki za kidini ambazo zinaweza kuchochewa, na katika miaka ya karibuni zimechochewa kwa urahisi kuwa pigano la waziwazi na ujeuri wenye matendo ya kinyama. Ingawa hivyo, wewe utaona pia kwamba Waairishi si kwamba tu ni wenye moyo mkunjufu na wachangamfu bali ni wakaribishaji-wageni na wasioharakishwa.

Historia yao tangu wakati wa wale wavamizi Waselti wa karne ya nne K.W.K. kuteremka kupitia wakati wa waakuaji Wavaikini na Wanormani kufikia wakati wa wafalme wa Uingereza ni hadithi ya uchungu yenye kuhuzunisha, umwagaji-damu, na uonevu. Kwa zaidi ya miaka 750 Ailandi ilitawalwa kutoka Uingereza. Katika 1922, kufuatia ushindani kwa ajili ya kujitawala, kile kisiwa kiligawanywa. Ile sehemu ya kaskazini, inayokaliwa sana sana na Waprotestanti, ilibaki katika United Kingdom (Uingereza). Zile sehemu nne kwa tano zilizobaki za kisiwa kile, ambazo karibu zote ni za Kikatoliki, zikawa ile Jamhuri ya Ailandi yenye kujitawala.

KITO CHA ZUMARIDI

Ujapokuwa ule upande wenye huzuni wa historia ya Ailandi, ile nchi humeta kwa uzuri wa rangi kijani. Hiyo ni kito zumaridi cha kisiwa chenye sehemu za mashambani zenye ukungu na majani mabichi zenye kuzungukwa na pwani yenye miamba-miamba. Safiri zile kilometa 272 zayo kutoka mashariki kwenda magharibi nawe utafurahia kuona nyanda za kati zenye rutuba za nchi, zenye kuzungukwa na vilima vilivyopanuka-panuka kwa utaratibu na milima yenye fahari. Shika njia kwenda kutoka kaskazini kuelekea kusini (mwendo upatao kilometa 480) nawe utapendezwa mno na mandhari hayo yenye maziwa na mito, na uzuri wa sura yenye kupendeza ya pwani yayo, pamoja na rangi za aina mbalimbali, na wingi wa mimea mibichi na maua. Ukiisha onwa, uzuri wa Ailandi ni vigumu kusahaulika.

Ingawa kwa msingi nchi ni ya kilimo, katika miaka ya majuzi viwanda fulani vimetokea-tokea upesi. Vile vitovu vikubwa vichache vyenye idadi ya watu kama Dublin, mji mkuu wa Jamhuri, na Belfast, mji mkuu wa Ailandi Kaskazini, hutofautiana kabisa na ile miji yenye utulivu na amani pamoja na vijiji vya sehemu za mashambani. Ilikuwa katika mazingira haya kwamba cheche ya ukweli iliwashwa katika sehemu ya mwisho-mwisho ya karne ya 19.

C. T. RUSSELL AWASHA CHECHE YA UKWELI

Katika 1891 Charles T. Russell, msimamizi wa kwanza wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi Biblia na Trakti, alizuru Ailandi. Ilikuwa ndiyo bandari yake ya kwanza kuzuru wakati wa kusafiri kutoka United States ili kupanua kazi ya kuhubiri ukweli wa Kikristo katika Ulaya. Russell, yeye mwenyewe akiwa wa mzao wa wazazi wa Kiskochi na Kiairishi, alishuka toka melini katika Queenstown (sasa Cobh) kusini mwa Ailandi.

Likiwa tokeo la kazi yake, maeklesia, au makundi, yalianzishwa katika Dublin na Belfast, na kutoka kwa hayo ujumbe wa ukweli ukaanza kutiririka. Wakati wa pindi hii ya mapema, akina ndugu waligawa matrakti kwenye milango ya makanisa ya Kiprotestanti na wakashiriki katika kutoa ushuhuda vivi hivi badala ya ule uliopangwa kitengenezo. Mnara wa Mlinzi (Kiingereza) katika 1904, uliripoti hivi: “Katika Ailandi, pia, ule Ukweli unaenea: wale ndugu wapendwa katika Dublin wanaendelea kutawanya ule ujumbe wa upendo, wakijiletea wenyewe shangwe kuu.”

Katika 1908 watu wapatao 300 walihudhuria mhadhara wa Russell katika Belfast juu ya kichwa “Kupinduliwa kwa Milki ya Shetani.” Kufikia wakati huo Belfast ulikuwa na eklesia ya Wanafunzi wa Biblia wapatao 24. Katika Dublin, baada ya kukutana pamoja na ndugu na watu wengine wenye kupendezwa karibu 40, yeye alisema kwa hadhirina ya watu zaidi ya elfu moja.

Miaka mitatu baadaye katika ziara nyingine, Russell alikutana na Wanafunzi wa Biblia wapatao 40 katika Belfast. Jioni hiyo watu wapatao elfu moja walikuja kwenye Ulster Hall kusikiliza hotuba yake “Ni Ipi Iliyo Gospeli ya Kweli?” Katika hotuba yake Russell alitetea Biblia kisulubu dhidi ya uchambuzi wa juu zaidi na akakazia kwa uthabiti uhitaji wa kurudia Biblia badala ya kushikilia itikadi na mafundisho ya wanadamu.

UKOSEFU WA UMOJA KATIKA WAZO

Hata hivyo, ijapokuwa hii mianzo yenye matumaini, kazi ya kuhubiri haikusonga mbele bila shida. Katika siku hizo wakati Wanafunzi wa Biblia katika Ailandi walikuwa ndipo tu wanaanza kufahamu zile kweli za Biblia, hakukuwa na ule umoja katika wazo ambao tangu hapo umesitawi miongoni mwa watu wa Yehova duniani pote. Kwa sababu gani? Kwa sababu wengi ambao walishirikiana nao walishindwa kuona ule uhitaji wa ‘kuunganishwa na kushikamanishwa pamoja’ ili kutimiza penzi la Mungu.—Waefeso 4:1-6, 16.

Kufikia 1914 walikuwako Wanafunzi wa Biblia wapatao 70. Kwenye mikutano wengi wangeendeleza fasiri yao wenyewe ya Maandiko makundi yalipokuwa yakizungumza, mathalani, ule mfululizo wa vitabu Millennial Dawn. Wao wakawa wenye ubinafsi na wakahisi kwamba ufahamu wao wa Biblia ulikuwa wa juu zaidi. Na wakati ilipopata kuwa wazi kwamba 1914 hautaleta mwisho kabisa wa mfumo huu wa mambo, hesabu kadha wa kadha ya hawa Wanafunzi wa Biblia walikataa njia ya ukweli ambayo Yehova alikuwa akitumia.

ROHO YA KUTAKABARI KATIKA DUBLIN

Vita ya Ulimwengu ya Kwanza ilipokuwa ikijikokoteza, ile roho ya kutakabari ya watu wenye akili ya kujitegemea ilipanda mbegu za matatizo zaidi. Wao walifikiri kwamba mafundisho ya Biblia yaliyoendelezwa na Ndugu Russell hayakuwa na maana kwa vyo vyote. Hivyo, wao walishindwa kung’amua kwamba Yehova alikuwa na kazi ya maana kwa watu wake kufanya.

Kufikia 1919 wazee wa kuchaguliwa katika kundi la Dublin walikuwa wakipinga kwa bidii shauri na mwelekezo uliokuwa ukija kutoka tengenezo la Yehova. Wao walichukizwa na cho chote ambacho kiliingilia mamlaka yao juu ya kundi. Maoni na mawazo yao ya kibinafsi yakawa ndiyo ya maana zaidi. (Warumi 12:3) Ijapokuwa hawa wazee walisomea kundi zile barua zilizopelekwa kutoka Sosaiti, wao walipuuza shauri au mwelekezo wo wote uliotolewa na hizo. Waaminifu wachache katika kundi waliendelea kufanya yale waliyoweza kwa njia ya kugawa matrakti pamoja na vitabu kama The Divine Plan of the Ages, lakini walio wengi hawakuwa na tamaa ya kuhusika katika kazi hiyo.

Charles Wilson, mmoja wa akina ndugu katika hilo kundi la mapema katika Dublin, alikumbuka jinsi mambo yalivyofikia upeo jioni moja katika 1920. Kufikia wakati huo walio wengi wa wale waliokuwa katika kundi walikuwa wamepoteza uthamini kwa tengenezo la Yehova. Yeye anatuambia yaliyotukia:

“Sisi tulienda kwenye mkutano usiku huo na tukaambiwa na mmoja wa wazee kwamba kundi lilikuwa likienda kupiga kura kutuondoa katika kampuni yao. Wakati walipotuambia kwamba wao walikuwa wakijitenga na Wanafunzi wa Biblia wa Kimataifa na kuanzisha tengenezo lao wenyewe, mimi nilisema, ‘Basi, ninyi hamna haja ya kupiga kura kutuondoa katika kampuni yenu. Sisi tunaondoka!’ Mimi niligeuka na nikaenda nje ya mlango. Ndugu na Dada Brown na Dada Rutland wakanifuata nje.”

Suala moja lililoleta mgawanyiko lilihusiana hasa na kazi ya kuhubiri kwa kutumia The Golden Age na vichapo vingine. Jingine lilikuwa kama inafaa kukubali njia ya kitheokrasi zaidi ya tengenezo kama ilivyokuwa ikizungumzwa wakati huo katika Mnara wa Mlinzi. Kilikuwa kipindi kigumu sana. Kusafisha halisi kulitokea. Kati ya washiriki wa kundi karibu mia moja, ni wanne tu walioshikamana na tengenezo la Yehova. Wale waliojitenga hatimaye walivunjika-vunjika wakawa vikundi vidogo-vidogo vilivyofarakana na visivyopatana, kila kimoja kikiwa na kiongozi wacho chenyewe.

Kazi ya kuhubiri katika Dublin ikakaribia kukoma. Hata hivyo, kadiri wakati ulivyoendelea, wengine wakachukua mwito wa kutangaza habari njema si katika Dublin tu bali kote kote katika Ailandi wakiwa makolpota, au wahubiri wa wakati wote.

Nyakati nyingine makolpota walifukuzwa kutoka mahali pao pa kulala yakiwa ni matokeo ya upinzani uliochochewa na viongozi wa kidini. Ingawa hivyo, sikuzote wao walikaribishwa na Dada Rutland, ambaye hapo kwanza alikuwa polisi-mwanamke na mmoja wa wale wachache washikamanifu waliobaki katika Dublin. Akina ndugu na dada wengi wanamkumbuka kwa shauku za upendo kama “Ma” Rutland nao wanashukuru kwamba yeye alifanya kao lake kuwa himaya kwa wale waliolihitaji wakati mambo yalipokuwa magumu. Sikuzote wewe ungeweza kupata “kitafuno na kandirinya ikikaa juu ya jiko” kwa “Ma” Rutland.

KATIKA AILANDI KASKAZINI

Hata hivyo, kabla ya sisi kuendelea na hadithi ya Jamhuri ya Ailandi, acheni tupate habari za matukio katika Ailandi Kaskazini. Pembe hii ya kaskazini-mashariki ya kile kisiwa, pamoja na nchi yenye mashamba mapana-mapana yayo na milima mifupi, ilikuwa imefanywa koloni katika karne ya 17 na Waprotestanti kutoka Uingereza. Watu wa Ailandi Kaskazini wapatao theluthi mbili ni wazao wa Waprotestanti Waingereza na Waskochi. Uprotestanti wa namna ya kivita hasa umesitawi tangu hapo, ukiwa na tabia ya kuchukia vikali sana Ukatoliki. Katika sehemu hii ya kisiwa pia, watu walikuwa katika giza la kiroho na katika hali ya kutojua kusudi la Mungu, wakipofushwa na mafundisho ya Babuloni Mkuu kama vile walivyokuwa watu waliokuwa upande wa kusini. Wao pia walihitaji msaada ili wawe huru.—Ufunuo 17:1, 2; 18:2-4.

KUFUNGUA MACHO KWA DRAMA YENYE PICHA

Kuanzia katika 1914 ile Photo-Drama of Creation ilitumiwa kusaidia kufungua macho ya watu. Toleo hili, ambalo lilitia ndani slaidi zenye rangi, picha zenye mwendo, na sahani za santuri zilizoambatanishwa vizuri, zilionyesha kutimizwa kwa kusudi la Mungu tangu uumbaji na kuendelea mpaka mwisho wa ule Utawala wa Miaka Elfu wa Yesu Kristo. Dada Maggie Cooper alisaidia katika kuonyesha Photo-Drama kote kote Ailandi Kaskazini.

“Jumba lilisongamana [watu] kila usiku, bila upinzani mwingi na kukiwa na uthamini mwingi sana,” akasema. “Hiyo ilivunja chuki nyingi isiyo na sababu nzuri dhidi yetu.” Yeye anakumbuka jinsi haikuwa kazi rahisi kusafirisha vyombo vyote vya maonyesho ya saa nane vya Photo-Drama. “Nikitazama nyuma,” yeye alisema, “Mimi siwezi kufahamu jinsi tulivyofanya hilo. Kulikuwako vizuizi vingi sana na mizigo chungu nzima ya kubeba kote kote tulikoenda.” Kwa itibari na uhakika katika Yehova, hata hivyo, wao waliweza kushinda vizuizi hivyo vyote.

UKWELI JUU YA MOTO WA MATESO

Matrakti yenye kufunua wazi mafundisho-bandia kama vile moto wa mateso yalipenya ndani ya ule utusi-tusi wa kidini uliokuwako katika Ailandi Kaskazini. Mathalani, wakati wa Vita ya Ulimwengu ya Kwanza, tangazo moja katika nyusipepa moja ya Belfast lilinasa jicho la Bob Oliver. Lilisomwa hivi: “Yasema Nini Maandiko Juu ya Moto wa Mateso? Ili upate trakti ya bure juu ya habari hii andikia Shirika la Wanafunzi wa Biblia wa Kimataifa, 34 Craven Terrace, London, W.2.” Bw. Oliver, ambaye wakati huo alikuwa mshiriki wa Kanisa la Presbiteri, alikuwa na mashaka mengi juu ya fundisho la moto wa mateso. Kwa hiyo yeye alijibu tangazo lile na akatambua ukweli katika yale aliyosoma. Kutuma jibu ili apate trakti hiyo ilikuwa hatua ya kwanza katika mwendo wa maisha katika utumishi wa Yehova unaoendelea mpaka leo hii.

Akiwa msichana mchanga, Susan Milne alikuwa amehudhuria mikutano mingi hemani yenye kuvuta maono ya moyoni iliyofanywa na mafarakano mengi ya wazaliwa-mara-ya-pili katika Ailandi Kaskazini, ambako wahubiri walirudia-rudia kutaja juu ya kuhukumiwa adhabu ya milele katika mioto ya mateso. Susan alikata maneno kwamba yeye hakustahili kuokolewa, kwa kuwa yeye hakuhisi kamwe lile ono la wokovu ambalo wengi waliohudhuria mikutano hiyo walidai kuwa nalo. Hata hivyo, katika 1922, yeye alisoma trakti moja yenye kichwa Where Are the Dead? Baada ya hilo matazamio yake yote yakabadilika.

Kabla ya hili baba yake alikuwa amemshangaza wakati aliposema: “Mimi nimeanza kufikiri kwamba hakuna kitu kama moto wa mateso.” Kwa msichana huyo hilo lilikuwa kufuru. Lakini sasa yeye alijua yale ambayo Yesu alimaanisha aliposema, “hiyo kweli itawaweka huru”—hasa kutoka kwa mafundisho-bandia ya kidini. (Yohana 8:32) Kwa hiyo baada ya kusoma trakti hiyo, yeye alitembelea baba yake, na kwa furaha yao wote wawili, walipata kuona kwamba wote wawili walikuwa wakisoma vichapo kutoka chanzo kile kile kimoja—lile Shirika la Wanafunzi wa Biblia wa Kimataifa. Msichana huyo na mume wake, baba yake, na wengine wa jamaa yake wote wakaja katika ukweli.

“TANGAZENI . . . MFALME NA UFALME WAKE”

Dada Milne aliona kwa haraka uhitaji wa kuchukua hatua. Mara nyingi yeye alirudia-rudia ile shime kutoka ule mkusanyiko wa Cedar Point wa 1922, “Tangazeni, tangazeni, tangazeni, Mfalme na Ufalme wake.” Na kwa kuitikia yeye na jamaa yake walikampeni kwa mapana na marefu wakitumia The Harp of God na wakashiriki kwa idili katika kuongoza mitaala ya funzo kwa kutumia kichapo hicho chenye kutoa nuru ya elimu.

Akina ndugu na akina dada, kutia Bob Oliver na Susan Milne, walianza kutoa ushuhuda Jumapili katika Ailandi Kaskazini kwa kutumia The Harp of God. Wale watu waliotolewa ushuhuda walikuwa na pokeo la Kipresbiteri lililotia mizizi sana ambalo lilitia ndani kukirihi sana lo lote ambalo lingeweza kuonwa kuwa kuvunja Sabato. Kwa hiyo itikio lenye kasirani likawa kawaida ya kila siku.

Mashahidi walionyesha ushujaa uo huo wakati walipokuwa wakigawa matoleo ya The Golden Age ambayo yalikuwa na ujumbe wenye kusema waziwazi ukiwashutumu viongozi wa kidini kwa sehemu yao waliyoshiriki katika kuficha ukweli na kutesa Wakristo wa kweli. Ndugu Oliver anakumbuka vizuri sana kielezi kimoja katika toleo la pekee la The Golden Age—kiongozi wa kidini akipunga sime iliyokuwa ikitiririsha damu penye ncha yayo. Maneno ya maelezo yalikuwa ni ule ujumbe kutoka Yeremia 2:34 (King James Version): “Katika marinda yako imeonekana ile damu ya zile nafsi za wale maskini wasio na hatia.”

Akina ndugu walipanga pia kutoa hotuba za watu wote wakitangaza Ufalme ko kote walikoweza. Hivyo ndivyo Bob Dempster alivyokuja kukutana na ukweli katika mji wa kwao wa Comber, karibu Belfast. Hata hivyo, kadiri kazi ya utangazaji ilivyopata nguvu, ule upinzani uliongezeka pia. Wakati Ndugu Dempster mwenyewe alipoanza kutangaza Ufalme, wale viongozi wa kidini walitumia njia zenye hila kujaribu kumzuia. Mathalani, katika wakati ambapo kulikuwa ukosefu mkubwa wa kazi za kuajiriwa, wao walitumia uvutano wao juu ya mkuu wa serikali aliyeshughulikia mambo hayo ili akatae kumpa Ndugu Dempster usaidizi uliohusiana na ukosefu wa kazi ya kuajiriwa. Lakini Ndugu Dempster alikataa kuogopeshwa. Yeye alianza kushirikiana na kundi dogo ambalo lilikutana katika kao la jamaa ya Milne, kwa manufaa yao wote.

Pole kwa pole lakini kwa uhakika kadiri nuru ya Ufalme ilipoenea, makundi yakaanza kukua. Hata hivyo, si maadui wote wa ule ukweli waliokuwa wa kutoka nje.

KUPEPETA KATIKA BELFAST

Kama vile akina ndugu katika Dublin walivyokuwa wamehisi yale matokeo mabaya ya wazee wa kuchaguliwa kwa kura wenye akili za kujitegemea huko nyuma katika 1920, ndivyo walivyohisi wale waliokuwa katika Ailandi Kaskazini, hasa katika Belfast. Kwa hiyo wakati wa kupepeta ukaanza. Ushikamanifu kwa tengenezo la Yehova na idili kwa ajili ya kazi ya peupe ya kuhubiri kwa mara nyingine tena likawa jambo kuu ambalo lilitenganisha watu. Mwanafunzi wa Biblia mmoja ambaye alikuwa amekutana na Ndugu Russell wakati wa ziara yake huko Belfast katika 1908 akaja kupendelea mawazo na maoneleo yake mwenyewe. Hatimaye yeye akaanzisha kikundi chake mwenyewe, ambacho yeye alikiita Wanafunzi wa Biblia Mathubuti.

Baadaye, kichapo The Finished Mystery kikiwa na shutumu lenye nguvu juu ya dini ya bandia kilipokuwa kimekwisha kutolewa katika 1917, wengine wakawa waoga na wakavunja ushirika. Mshiriki mmoja mashuhuri wa kundi la Belfast aliweka ilani penye dirisha la duka lake ambayo ilisoma hivi: “Mimi sina uhusiano na lile Shirika la Wanafunzi wa Biblia wa Kimataifa wala na kile kitabu The Finished Mystery.” Yeye pia alianzisha kikundi chake mwenyewe na akadai kushikamana na mafundisho ya Ndugu Russell. Katao la namna hiyo la njia ya Yehova likifanywa na wale waliokuwa mashuhuri katika kundi lilitahini imani na ushikamanifu wa wale ndugu waliobaki.

Mtihani mkubwa hata zaidi ulikuja kutoka kwa baadhi ya watu mmoja mmoja ambao walibaki ndani ya kundi. Kadiri kazi ya kuhubiri ilipopata mwendo wenye nguvu, mgawanyiko halisi wa wazo ulizidi kuwa wazi kati ya wale ambao walithamini kabisa uhitaji wa kutangaza Mfalme na Ufalme, na wale wazee waliochaguliwa kwa kura waliokuwa na maoni yaliyo tofauti.

Kama wale waandishi na Mafarisayo wa siku za Yesu ambao ‘walipenda mahali pa mbele,’ hawa walipendezwa zaidi na cheo na mapendeleo kuliko kuendelea na kazi ya kuhubiri. (Mathayo 23:2-7) Mwelekeo wao wa kiburi na makuu ulifanyiza wasiwasi na ukosefu wa furaha katika kundi. Hali ya shuku na kutokuwa na itibari hatimaye ilizuka kadiri kila mzee alivyojaribu kujiinua mwenyewe na kuimarisha cheo chake katika kundi.

Wakati wa uchaguzi wa wazee ulipofika kura ziliombwa-ombwa. Baadhi ya wazee walipanga kuwe na karamu za pekee za chai na wakaalika akina ndugu na dada kwa kusudi pekee la kupata kuungwa mkono nao na kuvuta kura zao. Kwa sababu hawa wazee walishindwa kutambua Kristo kuwa kichwa cha kundi, kutopatana, vikundi-vikundi vya wenye maoni mamoja, na migawanyiko ilizuka. Hili linaelezwa vizuri na jambo lililotukia katika Korintho wa kale. Kwa sababu ya kuwapa wanadamu fikira isivyofaa, washiriki wa lile kundi la Korintho walifarakana wakawa vichamkano, wakisema: “Mimi ni wa Apolo, na, mimi ni wa Kefa, na, mimi ni wa Kristo.”—1 Kor. 1:11, 12.

Baadhi ya akina ndugu, kama vile Diotrefe wa siku ya Yohana, hawakuonyesha heshima nyingi sana kwa mwelekezo wo wote uliokuwa unakuja kupitia tengenezo la Yehova, na wao kwa makusudi wangejaribu kuingiza mashaka kuhusu Sosaiti ndani ya akili na mioyo ya wale waliokuwa wanyenyekevu, na watiifu. Katika njia hii wao waliiga roho ya Diotrefe kwa ‘kutoa upuzi juu ya akina ndugu kutoka tawi kwa maneno maovu.’—3 Yn. 9, 10.

Kwa kumaliza Yehova akatenda. Yale matoleo ya Agosti 15 na Septemba 1, 1932, ya Mnara wa Mlinzi yalieleza kwa sababu gani kikundi cha akina ndugu wakomavu chenye kuitwa halmashauri ya utumishi chapaswa kuongoza kundi, si “wazee waliochaguliwa kwa kura.” Jambo jipya hili la kitengenezo lilipepeta na kutoa nje ya kundi wale wa mwisho wa wale wenye uasi, likiacha wahubiri wa kawaida 12 tu katika Belfast ambao walishikamana na ule ukweli.

HOTUBA ZA RUTHERFORD ZAONGEZA KICHOCHEO

Wakati wa muda wa tangu 1930 kikundi hiki kidogo cha akina ndugu katika Ailandi Kaskazini kilifuatana na matukio miongoni mwa watu wa Yehova wa duniani pote. Kwa idili wao walianza kutumia hotuba zilizorekodiwa za J. F. Rutherford, aliyekuwa wakati huo msimamizi wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi. Mambo yaliyoonwa yenye kusisimua kutokana na kutumia mashine za kutangazia habari zilizorekodiwa katika sahani za santuri yakafuata upesi.

Alex Mitchell alikuwa baharia. Alipokuwa baharini akiwa mhandisi katika 1927, yeye alisoma vile vitabu The Divine Plan of the Ages, The Time Is at Hand, na The Harp of God naye akaona nuru ya ukweli. Aliporudi nyumbani Belfast, alianza mara moja kutafuta msaada zaidi wa kufahamu Biblia. Baadhi ya washiriki wa Wanafunzi wa Biblia Mathubuti walijaribu kumvunja moyo asisome vichapo vya Sosaiti. Lakini yeye tayari alikuwa ametambua ule mlio wa ukweli katika vichapo hivi, na hatimaye yeye aliwapata wale Wanafunzi wa Biblia wa kweli.

Upesi yeye akaanza kazi ya kuhubiri. Yeye alikumbuka vizuri jinsi yeye na Ndugu Oliver walizoea kubeba ile mashine ya kuchezea sahani za santuri kote kote mjini Belfast. Walianza kazi hii bila kuwa na gari. Kwa hiyo jiwazie ukiwaona wanaume wawili wakipiga miguu kutoka barabara moja ya mji kwenda barabara nyingine ya mji na katika maeneo ya mashambani wakiwa wanakokota vyombo vyao vyote kwa kamba za ngozi zilizozungushwa juu ya mabega yao!

Mojapo madaraka ya Ndugu Mitchell lilikuwa kutafuta majumba yanayofaa ambamo kutoka humo wangetangaza zile hotuba zilizorekodiwa. Majumba yangeweza kupatikana—lakini kwa kawaida ilikuwa mara moja tu. Kwa sababu gani? Kwa sababu sehemu zilizo nyingi zilikuwa chini ya macho yenye kutazama ya viongozi wa kidini wa mahali-mahali, ambao walichukizwa na ujumbe uliokuwa ukitangazwa. Wakati ambapo hawakuweza kukodi majumba, hawa ndugu walitumia mashine zao za kutangazia ujumbe uliorekodiwa katika barabara za Belfast na katika sehemu za mashambani za karibu-karibu.

Aghalabu wao walichagua barabara za Kiprotestanti ambazo katika hizo wangetangaza zile hotuba kwa sababu wakati huo watu wa Kiprotestanti kwa ujumla walikuwa waitikivu zaidi. Wakati mmoja, Ndugu Mitchell na Ndugu Milne waliendesha gari lao kwenye barabara ndogo yenye utulivu bila ya kukagua eneo kwanza. Walitayarisha vyombo vyao kama kawaida, wakapiga muziki kidogo kuvuta fikira, na ndipo wakaalika watu wa mahali pale kusikiliza mhadhara wa Biblia. Hata hivyo, bila kujua, wao walikuwa wameendesha gari lao kwenye eneo la Ukatoliki thabiti, ambako waliainishwa kimakosa kuwa Waprotestanti. Watu wa mahali pale wakaanza kuwapiga kwa mawe. Kwa haraka wakarundika vyombo vyao vyote tena ndani ya gari lao na kutoroka. Ndugu walipokuwa wakiondoka, kundi hilo lenye ghasia likaponda-ponda kiwiliwili cha gari lao kwa fito za chuma na wakavunja-vunja kioo cha kuzuia upepo. Hata hivyo, kando na mshtuo huo, wao waliponyoka bila dhara lo lote baya, na tukio hilo halikushusha kwa vyo vyote idili yao kwa ajili ya kazi.

Alasiri moja Ndugu Mitchell alirushiwa makombora ya viazi. Kwa tokeo zuri vilikuwa vimepikwa na kwa sababu hiyo vilikuwa vyororo. Alipokuwa akiendesha gari lake kutoroka, Ndugu Mitchell alisema na umati kupitia kipaaza sauti jinsi alivyoterema kwa vile hakuwa amekuja asubuhi, kwani viazi hivyo vingalikuwa vigumu zaidi!

Akina ndugu pia walifanya tumizi zuri la kinanda chenye kubebwa. Ijapokuwapo vikosa-vikosa fulani, kama vile kusahau kuweka rekodi mahali payo kabla ya kuondoka nyumbani kwenda kwenye huduma, wao walipata kuwa stadi sana katika kutumia chombo hiki. Wakiwa na baiskeli moja, kinanda kimoja, na seti moja ya rekodi, na kisanduku kimoja cha vitabu, wao walikuwa na vifaa vya kutosha kwa ajili ya kazi ya siku nzima ya kutoa ushuhuda.

KUTIWA NGUVU NA MIUNGANISHO YA REDIO NA SIMU

Kusikia mihadhara ya Ndugu Rutherford ikitangazwa moja kwa moja kutoka sehemu kama vile London na New York kuliwatia nguvu akina ndugu. Katika 1938 ule mhadhara wenye nguvu nyingi wenye kichwa “Kabili Mambo ya Hakika” ulivuta hadhirina ya zaidi ya 2,500 kwenye lile Jumba la Mfalme katika Belfast.

Kuhusiana na kutangazwa kwa hotuba hii, baadhi ya akina ndugu wangali wana kumbukumbu dhahiri sana za ule utangazaji wa kupiga miguu uliofanywa kupitia Belfast. Kwa sababu ya hali ya kidini yenye mkazo katika Ailandi Kaskazini wakati ule, wengi walihisi kuwa na wasiwasi kuhusu taraja la utangazaji wa kupiga miguu. Lakini wao walifanya gwaride 25 katika barabara kuu za mji bila kufanyiwa vitendo vyo vyote vya jeuri.

Baadhi ya akina rafiki walivalia kadi kubwa zilizotangaza ule mhadhara wa watu wote. Wengine waliinua ishara zilizokuwa na shime kama vile “Dini ni Mtego na Hila” na “Mtumikieni Mungu na Kristo Mfalme.” Kijana mmoja mleta-habari za magazetini, alipoona ile shime “Dini ni Mtego na Hila,” aliuliza: “Je! ninyi mnapata kujua hilo sasa hivi tu?”

Ule mhadhara “Serikali na Amani” ulikuwa ukitolewa moja kwa moja kutoka Madison Square Garden Mjini New York kwa kuunganishwa kwa nyuzi za simu. Wakati wa hotuba hii mapolisi walilinda lile jumba katika Belfast ambamo akina ndugu walikusanyika. IRA (Jeshi la Jamhuri ya Ailandi) lilikuwa limetisha kupiga lile jumba kwa kombora ikiwa ule mhadhara haukufutwa. Akina ndugu hawakuvunjwa moyo. Zile jitihada za IRA za kuogopesha akina ndugu katika Belfast zilishindwa kufanikiwa kama zile jitihada za Aksio la Katoliki za kuvunja ule mhadhara katika New York.

Matangazo haya ya moja kwa moja yalisitawisha hisi ya umoja miongoni mwa akina ndugu. Ijapokuwa ile juhudi ya kidini na ya uzalendo iliyokuwa ikizidi kupata nguvu vita ilipokuwa ikitisha Ulaya, kikosi hiki kidogo cha akina ndugu katika Ailandi kiliweza hivyo kuona kwamba kilikuwa sehemu ya tengenezo lenye kukua la ulimwenguni pote. Hata hivyo, kabla ya kuendelea na matukio katika Ailandi Kaskazini, acheni turudi nyuma na kuendelea na hadithi katika Jamhuri ya Ailandi.

UPINZANI WENYE KUENDELEA KATIKA KUSINI

Wakati wa kipindi cha kuanzia 1920 kufika Vita ya Ulimwengu ya Pili, ni akina ndugu na dada wachache tu waaminifu waliokuwa wakijitahidi kuendelea katika Dublin wenyewe, hali katika sehemu ile nyingine yote ya kusini ya Ukatoliki ni kazi ya kolpota tu iliyokuwa ikifanywa hapa na pale.

Maelezo fulani kutoka Vitabu vya Mwaka vya Mashahidi wa Yehova vinatupa wazo la hali ambazo hawakuwa na budi kuvumilia.

1935: “Akina ndugu wameletewa hasara, na wengine wakaumizwa kimwili, na vitabu ambavyo vingesaidia watu vimeharibiwa.”

1937: “Ailandi ndiyo sehemu yenye giza zaidi ya Visiwa vya Uingereza. . . . Makasisi . . . hufuata mapainia kutoka mahali kwenda mahali, wanatafuta mahali ambako vitabu vimeachwa . . . na mara moja kuagiza viharibiwe.”

1938: “Upinzani mwingi kwa wahubiri wa ujumbe wa Ufalme. Watu wenye ghasia wameshambulia Mashahidi wa Yehova kwa kuchochewa na makasisi wa Katoliki ya Roma . . . Upinzani bado haujafikia kilele chao.”

Mapema, wakati wa 1926, Ndugu Pryce Hughes, ambaye baadaye alitumikia akiwa makamu wa msimamizi wa Shirika la Wanafunzi wa Biblia wa Kimataifa katika London, na waandamani wake watatu walienda Waterford katika kusini mwa Ailandi. Walikaribishwa na ndugu watatu waliokuwa wameenda huko mapema. Kabla ya Ndugu Hughes kuwasili, akina ndugu katika Waterford walikuwa wamevumilia shambulio la Wakatoliki wenye ghasia lililofanywa na wahuni ambao waliteketeza vile walivyofikiria kuwa ‘vitabu viovu.’

Baada ya kuangushia vitabu watu wenye kupendezwa, akina ndugu wangesonga mbele kwa haraka. Walipata makao kwa watu wa Kiprotestanti na kujaribu kueneza sehemu kubwa zaidi iwezekanavyo kabla ya kasisi wa mahali hapo kupata kujua lililokuwa likitukia. Katika mji mmoja, magazeti ya mji huo yalichapisha maonyo juu ya utendaji wao, na watoto wangewatemea mate walipokuwa wakipita barabarani. Hivyo ili waepuke kutambuliwa kwa haraka sana, wao walifanya kazi kuanzia nje ya sehemu yao ya eneo lililochaguliwa na kumalizia na mji ambako walikuwa na mahali pao pa kulala.

Pindi nyingine, katika mji mdogo wa soko la Graiguenamanagh, walikutana na upinzani mkali. Waliporudi mahali pao pa kulala, walikabiliwa na umati wa vijana wenye kufanya mzaha, ambao waliwapiga kwa mawe. “Hii ilikuwa ‘siku kuu,’ ‘Siku ya Mtakatifu’ Patrick,” akasema Ndugu Hughes, “na mikokoteni yenye kukokotwa na nyumbu ilikuwa imekuwa ikija ndani ya mji siku nzima kwa ajili ya Misa za pekee. Wakati wa Misa, kasisi wa mahali hapo alikuwa amechochea kila mtu dhidi yetu.” Waking’amua kwamba ilikuwa sharti waondoke mahali hapo kwa haraka, yeye na waandamani wake walipeleka vyombo vyao kwa baiskeli kwenye stesheni ya reli iliyokuwa karibu zaidi.

Makolpota walijifunza kujipatanisha na tisho hili lililoendelea daima la jeuri. Wakati mmoja mtu akiwa na uma mrefu alifukuza Ndugu Hughes kutoka upande mmoja wa shamba mpaka upande mwingine. Wakati mwingine mkulima mmoja alifyatua bunduki kwa ghafula kwenye nyayo za Ndugu Hughes!

Kolpota mwingine, Jack Corr, aliwasili Dublin katika 1930. Wazazi wake walikuwa Wakatoliki, kwa hiyo yeye alikuwa ametayarishwa vizuri kuzungumza na watu wa Kikatoliki aliokuta. Yeye alipata kuona kwamba ijapokuwa Katiba ya Ailandi ilihakikisha uhuru wa dini, watu wengi waliitikadi kwamba hilo halipasi kutia ndani kazi ya kuhubiri ya Mashahidi wa Yehova.

Ndugu Corr mara nyingi alihisi ghadhabu kali ya viongozi wa kidini wenye kasirani na waungaji mkono wao. Kundi moja la watu wenye ghasia, likichochewa na kasisi wa parokia, walimburuta kutoka kitandani usiku wa manane na kisha wakateketeza vitabu vyake vyote katika uwanja wa mji. Wakati mwingine watu wenye ghasia wapatao 200 walikuwa wakigonga-gonga penye mlango wa mahali pake pa kulala. “Yule mpangizaji-nyumba mwanamke mwenye kuogopa sana alijaribu kunisukuma chini ya kitanda, huku akilaani vibaya sana kwa kupaazia sauti ule umati kupitia dirisha,” akaripoti. “Mimi niliweza kutuliza woga wake, na baada ya robo saa wale watu wenye ghasia walitoweka kama moshi, hilo likiniwezesha niendelee kama kwamba hakuna lo lote lililokuwa limetukia.”

JEURI ZAIDI KUTOKA KWA WAPINZANI WA KIDINI

Katika 1931 Victor Gurd na mwenzake Jim Corby waliwasili katika jiji la Cork, karibu na mahali ambapo Ndugu Russell alikuwa ameshukia katika Ailandi miaka 40 mapema. Kikundi kingine cha akina ndugu kilijiunga nao kwa muda. Walipitia sehemu za mashambani, wakigawa nakala za Studies in the Scriptures na The Harp of God.

Wakati akina ndugu walipokuwa wakitoa ushuhuda kwenye Roscrea, katika mkoa wa Tipperary, watu wenye bunduki waliwatisha, wakachukua vitabu vyao vyote, na kuwaonya waondoke wilaya hiyo. Wakati akina ndugu walipowasili kwenye mahali pao pa kulala, walipata matata zaidi. Wapinzani walikuwa wamechukua akiba yao ya vitabu, wakavilowesha petroli, na kuviwasha moto. Kuzunguka huo moto mkubwa walisimama mapolisi wa mahali hapo, viongozi wa kidini, na watoto kutoka eneo hilo, wakiimba “Imani ya Baba Zetu”!

Karibu na wakati huu John Retter na waandamani wake walikuja Limerick. Kwa sababu yeye alikuwa amezaliwa katika Austria, yeye alitolea ushuhuda Wajeremani wengi waliokuwa wamehamia pwani ya magharibi ya Ailandi. Alikuwapo pia John Cooke (anayetumikia sasa kwenye Betheli katika Afrika Kusini), ambaye katika 1936 alitupwa ndani ya gereza la Dublin kwa sababu yeye alisisitizia kufanya kazi ya Yehova.

HIMAYA YA YEHOVA KATIKA KASKAZINI

Wakati wa kipindi hiki cha kabla ya Vita ya Ulimwengu ya Pili, makolpota wengine waliongoza kazi katika Ailandi Kaskazini. Sarah Hall aliwasili katika Mkoa wa Tyrone katika 1926. Yeye alikuwa amepata kujua maarifa ya ule ukweli katika Uingereza katika 1915 baada ya kusoma The Divine Plan of the Ages. Yale aliyosoma yalimchochea aingie ile kazi ya kolpota.

Watu walio wengi aliosema nao hawakushiriki uthamini wake wa ukweli wa Biblia. Umbile lake dogo, jembamba na uelekevu wa upole haukuzuia mwanamke mmoja kumfukuza akiwa na uma mrefu au mwanamume mmoja ambaye alikasirikia ujumbe wake kumwita “Delila” na kujaribu kumkaba koo.

Bila hofu, yeye alionyesha hali ya kupiga moyo konde na ustahimilivu mkubwa. “Kwa ujumla, haikuwa mbaya,” yeye akasema, akifikiria nyuma walipohubiri chini ya hali zenye kutahini. “Sisi tulizoea kusikia wao wakipigia sisi kelele. Ikiwa wewe unasali upate himaya ya Bwana, yeye anakupa wewe hiyo.” Hao makolpota walikuwa na uhakika kwamba Yehova angekuwa ‘pamoja nao kuwaokoa wao.’ Na yeye alikuwa nao!—Yer. 1:7, 8; Zab. 23:4, 5.

YEHOVA AANDAA

Billy Holland alikuja katika ukweli katika 1926 baada ya kusoma The Divine Plan of the Ages. Kama vile makolpota wengi, yeye alitegemea sana ahadi ya Yehova kwamba watumishi wake ‘hawangeachwa kabisa’ kamwe.—Zab. 37:25, NW; Mt. 6:28-34.

Ndugu Holland anaeleza: “Nyakati nyingine nilikosa kiamsha-kinywa; nyakati nyingine nilikuwa na vipande vichache vya mkate bila siagi. Nakumbuka wakati mmoja ambapo mimi nilikuwa nje katika sehemu za mashambani katika Mkoa wa Down. Baada ya kutumia wakati fulani katika huduma, mimi niliteremka kupitia kijia kimoja na nikaegemeza baiskeli yangu kwenye ua. Mimi niliketi chini na nikawa ninakula mkate wangu mkavu na kusikiliza ndege wakiimba. Kisha mimi nikatazama kwa ukaribu zaidi kwenye ule ua na kuona baadhi ya beri nyeusi zenye kupendeza. Mimi nilichuma baadhi yazo na kuziweka katikati ya vipande vyangu vya mkate. Ikawa tu kama jamu ya beri nyeusi—mimi niliifurahia kweli kweli!”

Yeye alikuwa na roho iyo hiyo wakati alipopungukiwa pesa. “Viatu vyangu vilikuwa vikichakaa na nyayo zangu zingelowa,” yeye anakumbuka. “Ndipo siku moja yenye jua nilikuwa nikitembea kwenye barabara ya mashambani, joto likawa kali sana, nayo lami juu ya barabara ikaanza kuyeyuka. Ile lami ikajaa matundu katika soli za viatu vyangu. Kwa hiyo mimi ‘nikatengenezesha’ viatu vyangu.” Na hiyo ilifanywa bila malipo!

RIZIKI YA CHAKULA CHA KIROHO WAKATI WA VITA

Wakati wa Vita ya Ulimwengu ya Pili, kuanzia 1939 kufika 1945, Jamhuri ya Ailandi ilibaki bila kuwamo, bali Ailandi Kaskazini, ikiwa sehemu ya United Kingdom, ilistahimili mashambulizi ya makombora na magumu mengine ya vita.

Tatizo moja ambalo lilizuka wakati wa miaka hii lilikuwa ule uhitaji wa kudumisha riziki ya chakula cha kiroho. Wakati wa ile vita serikali ya Uingereza iliamrisha kuwe marufuku ya ukaguzi wa vitabu ambayo ilikataza kuingiza nchini na kutoa nchini Mnara wa Mlinzi na vichapo vingine vya Sosaiti. Hila hii ya Shetani ya kukata njia za mawasiliano na akiba kwa akina ndugu haikufaulu. Ilishindwa. Jinsi gani? Kwa njia ya kwamba Sosaiti ilipanga akina ndugu katika mahali kama vile United States na Kanada wapelekee akina ndugu katika Belfast nakala za Mnara wa Mlinzi chini ya jalada lisilo na maandishi.

Nakala hizi zilipopokewa, akina ndugu wenye madaraka walifanya kazi kwa haraka wakanakili makala kuu. Kisha wao wakazigawa kwa makundi. Mara nakala hizi za magazeti zilipoanza kuja, akina ndugu hawakukosa kamwe cho chote cha chakula chao cha kiroho cha muhimu.

Bob Oliver anakumbuka akipata Mnara wa Mlinzi kutoka kwa Ndugu Kelly katika United States. Ndugu Kelly angetia ndani pia habari juu ya yale ambayo “Mjomba Nathan” (Nathan H. Knorr, msimamizi wa tatu wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi) alikuwa amekuwa akisema, hivyo akitoa habari juu ya makusanyiko na kadhalika. Nyakati nyingine akina ndugu walipata Mnara wa Mlinzi au kitabu kama vile “The Truth Shall Make You Free” katikati ya kifurushi cha chakula walichotumiwa. Wakati nakala ya Mnara wa Mlinzi isiyofichwa ilipowasili bila kuguswa, akina ndugu katika Belfast walifanya ucheshi kwamba lazima iwe iliponyoka ikapita wakati mkaguzi alipokuwa amechukua wakati kwenda kunywa chai.

WATENDEWA KWA DHIHAKA

Wakati wa vita akina ndugu katika Ailandi Kaskazini walikuwa hawana budi kuvumilia uhasama mkali wenye kuendelea kutoka kwa viongozi wa kidini na waliowaunga mkono ambao waliunga mkono kikamilifu jitihada za vita. Yesu alisema kweli kama nini wakati aliposema: “Sasa kwa sababu ninyi si sehemu ya ulimwengu, . . . kwa sababu hii ulimwengu unachukia ninyi”!—Yn. 15:18, 19, NW.

Kifani cha dharau la watu ni barua inayofuata, iliyopelekwa kwa Kundi la Belfast katika Agosti 1943:

“Bwana:

“Nikiisha kufanywa mpokeaji asiyetaka wa mojapo vikaratasi ambavyo ninyi mna ukavu wa macho kupasisha juu ya halaiki yenye uvumilivu sana sana, inanipasa mimi nitake kuchukua nafasi hii ya kutaarifu kwamba mimi nakataa katakata wo wote wa wafuasi wenu kuingia juu ya ardhi yangu kwa kisingizio cho chote kile. Kulingana nayo, tafadhali shauri mkusanyo wenu uliongozwa vibaya wa wenye kufungua-fungua Biblia, walio kama makonokono, kwa kuwa, ikiwa onyo hili litapuuzwa, mwingiliaji bila ruhusa huyo ataondoshwa kwa nguvu—kwa nguvu sana. Mimi nitajizuia kuagiza mbwa amrukie, kwa kuwa mimi sitaki kulazimisha donge lisilo tamu kama hilo juu ya mnyama huyo maskini, lakini ikiwa yeye anaamua kuchukua hatua ya kwanza mwenyewe, bila shaka mimi sitaweka kizuizi cho chote katika njia yake.”

Zijapokuwa nyakati ngumu, kila jitihada ilifanywa kupanua utendaji wa kuhubiri. Je! Yehova aliendelea kubariki ile kazi ya ndugu hao wote waaminifu? Ndiyo! Wakati vita ilipokoma katika 1945, kulikuwako wahubiri wapatao 120 katika Belfast na wapatao 20 katika Dublin.

KUPAINIA KATIKA ILE JAMHURI

Kitabu cha Mwaka 1946 kilionyesha kwamba hakungekuwa na kuacha kueneza habari njema katika Jamhuri ya Ailandi mwishoni mwa Vita ya Ulimwengu ya Pili. “Ni vigumu,” kile Kitabu cha Mwaka kikasema, “kwa wengi kuthamini jinsi Ailandi Kusini ilivyo mahali penye giza kwa habari ya nuru na maarifa ya Neno la Mungu.” Ndipo kikaendelea hivi: “Hapa tena pana nafasi kwa mapainia halisi. Sasa sisi tunafanya mipango kwa baadhi [yao] wapelekwe huko.”

Fred Metcalfe, ambaye sasa ni mshiriki wa Halmashauri ya Tawi la Ailandi, alikuwa miongoni mwa wale mapainia wa pekee wa kwanza waliotumwa. Mgawo wake ulikuwa mji wa Cork kusini mwa ile nchi. Yeye pamoja na mapainia wenzake upesi wakawa shabaha ya upinzani wenye kuchochewa na viongozi wa kidini. Ili kuchochea uchukivu dhidi ya Mashahidi wa Yehova, kwa kurudia-rudia makasisi wangewabandika jina “maibilisi wa kikomunisti.”

“Kwa watu wa wakati huo,” akasema Ndugu Metcalfe, “ule usemi ‘komunisti’ ulimaanisha kwamba sisi ndio tuliokuwa kitu kilichokaribia zaidi Ibilisi akiwa katika umbile la kibinadamu ambacho kingeweza kutokea kwenye mandhari ile!”

Uhasimu ukaongezeka. “Mimi sikuwa nimepata kamwe kuwa na uthamini mwingi zaidi wa Ufunuo 12:17 kuliko wakati huo,” asema Ndugu Metcalfe. “Hakika Ibilisi alikasirikia kijeuri kazi ya kutoa ushuhuda iliyoanza kufanywa katika sehemu hiyo.” Mauwongo yaliyosemwa na makasisi na uadui wenye kuenea kote kote mwishowe ulifikia upeo katika shambulio la watu wenye ghasia juu ya Ndugu Metcalfe na mwandamani wake, Ndugu Chaffin, katika mji wa Cork katika 1948.

JEURI YA WATU WENYE GHASIA KATIKA CORK

Wakati mmoja Ndugu Chaffin alipokuwa katika utumishi wa shambani, umati wa wanawake wenye kutaka vita ulimzunguka, ukamshtaki kuwa mkomunisti, na ukaanza kumshambulia kwa jeuri. Kwa kuwa hakukuwako uwezekano wo wote wa kusababu pamoja na hawa watu wenye ghasia waliokasirika vikali, Ndugu Chaffin alijaribu kutoroka kwa kuingia katika basi lililokuwa karibu. Hata hivyo, lile kundi la wafanya kazi wa basi lilijiunga katika kumshambulia. Baadhi ya washambulizi walitupa mawe, hali wakora wengine walipiga makelele wakisema “Mkomunisti asiyefaa kitu!” na “Tupa yeye ndani ya mto!” Hatimaye, hata hivyo, yeye aliwapiga chenga wafuatiaji wake kwa kuepa na kuingia ndani ya kitalu chenye ukuta mrefu cha kao la kasisi.

Wakati ule ule, ndugu Metcalfe alijikakamua atoroke kwa baiskeli yake lakini akafikiliwa na wale wale watu wenye ghasia. Walimpiga ngumi na mateke na kutawanya vitabu vyake barabarani. Kwa furaha ya Ndugu Metcalfe, polisi mmoja akawa anapita pale. Yeye aliingilia jambo hilo na kutawanya wale watu wenye ghasia. “Mimi nilihisi ulikuwa uongozi wa Yehova,” akasema Ndugu Metcalfe, “kwamba mtu huyu alikuja kwenye tamasha hiyo wakati uo huo na akazuia shambulio hilo.”

Sosaiti iliamua kupigania kesi hii katika mahakama ili kuonyesha wazi kwamba Mashahidi wa Yehova hawakuwa Wakomunisti na ili kuthibitisha kisheria haki yetu ya kuhubiri zile habari njema bila kuingiliwa. Ijapokuwa kuahirisha-ahirisha ili kuzuia kesi hiyo isije mahakamani, hatimaye jaribio lilitukia katika Julai 1948.

Yule polisi ambaye alizuia lile shambulio, ingawa alikuwa Mkatoliki, yeye alikuwa na nia ya kusimama mahakamani na kwa haki kutoa ushuhuda juu ya yale aliyokuwa ameona. Washambulizi kadha wa kadha walipatikana na hatia ya ushambulizi. Utangazaji magazetini uliotokana na kesi hiyo ulisaidia sana kuondoa lile wazo la kwamba Mashahidi wa Yehova walikuwa wakomunisti na pia kuthibitisha haki yetu ya kutangaza habari njema. Hata hivyo, haikumaanisha mwisho wa upinzani wenye jeuri dhidi ya ukweli.

UPINZANI WENYE KASIRANI WAENDELEA

Mathalani, katika mji wa Athlone katika mashamba ya katikati ya Ailandi, mwanamke mmoja alionyesha kasirani yake kwa akina ndugu kwa kuwatupia kandirinya iliyojaa maji yenye kuchemka. Wakazi wa mji huo hata walipelekea Sosaiti ombi la kwamba wao hawakutaka Mashahidi wa Yehova warudi mle—kamwe! kamwe!

Wakati mapainia wa pekee wanne walipotumwa kwenye mji wa Drogheda, wao walitishwa kwa bunduki na wakashambuliwa kwa jeuri na watu wenye ghasia. Mkutano mmoja wenye kujaa watu ulifanywa katika mji, na azimio likakubaliwa la kuomba serikali ipige marufuku Mashahidi wa Yehova nchini. Ilani zilionekana kote kote mjini zikiwa na ujumbe huu: “Tendo la Aksio Katoliki! Wananchi wa Drogheda! Mkutano wa halaiki utafanywa . . . kufikiria njia za kupambana na utendaji wa farakano fulani la dini linaloendesha kazi katika wilaya. Meya na wawakilishi wa matengenezo wa mahali hapa watakuwapo.”

Kwa kukabiliwa na ukinzani wote huo, je! akina ndugu walijikunyata wakati wo wote? Hata kidogo! Wao walistahimili mikazo yote waliyoletewa na wakaanza kupata matokeo ya kazi zao ngumu.

MASIKIO YENYE KUITIKIA KATIKA DUBLIN

Dudley Levis alikuwa miongoni mwa wale wa kwanza kuitikia ujumbe wa ukweli miaka iliyofuata baada ya vita katika Dublin. Yeye alikuwa mshiriki wa Kanisa la Ailandi. Waprotestanti, ambao tayari walikuwa wakiishi chini ya mazingira ambayo karibu yote yalikuwa ya Kikatoliki, waliona kuacha kwake kanisa hili kuwa uhaini. Hivyo, yeye alielekeana na dhihaka na shutumu kutoka kwa wale ambao hapo kwanza walikuwa washiriki wake ambao walichukia imani yake mpya aliyoipata. “Mimi nilitiwa moyo sana sana,” yeye akasema, “na akina ndugu wenye umri mkubwa zaidi, kama vile Edwin Ridgewell, ambaye alikuwa ameonyesha imani halisi sana katika nyakati zenye taabu sana kabla yangu. Kielelezo chao kilinitia mimi nguvu.”

Mashahidi sana sana walielekeza kazi yao ya kuhubiri kwenye maeneo ya Kiprotestanti ambako tendo la kuitikia lilielekea kuwa lisilo na ukali mwingi kama vile ngome za Kikatoliki. Ingawa hivyo, polepole, wao walianza kupenya katika maeneo ya Kikatoliki. Ilikuwa vigumu. Lakini mwelekeo wao ulikuwa kama ule wa mtunga zaburi: “Katika Mungu mimi nimeweka itibari yangu. Mimi sitaogopa. Mwanadamu wa dunia anaweza kufanya mimi nini?”—Zab. 56:11, NW; Yos. 1:9.

JAMAA YA KIKATOLIKI YAITIKIA

Baada ya muda watu wa Kikatoliki walianza kuitikia ukweli. Mathalani, katika 1949, dada mmoja alionana na John Casey. Mwanamume huyu Mkatoliki alionyesha upendezi mwingi katika yale ambayo dada huyo alisema, lakini mke wake, Bridie, alikataa kumpa pesa alizohitaji kupata kile kitabu kilichotolewa, “The Truth Shall Make You Free.” Mwanamume huyu aliuliza dada arudi wiki iliyofuata. Alifanya hivyo, na kwa kushukuru John akakubali kile kitabu. “Mimi nimeupata ukweli,” yeye akasema. “Mimi sitakaribia lile Kanisa Katoliki tena.”

Bridie, hata hivyo, hakupendezwa. Yeye aliuliza swali ambalo akina ndugu walikutana nalo kwa kurudia-rudia katika kazi yao ya kutoa ushuhuda. “Yehova ni nani? Je! yeye ni mtu fulani katika Amerika anayeongoza tengenezo lenu?” Lakini hatimaye yeye pia alikubali ule ukweli wakati alipojifunza kwamba Biblia kwa kweli haifundishi moto wa mateso, utatu, na mafundisho mengine ya kidini yanayomvunjia Mungu heshima.

John na Bridie Casey, kama wale wengine walioanza kuona ile nuru ya ukweli, walipatwa na mkazo wa kifamilia na wa kijumuiya uliokusudiwa kuwavunja moyo wasiendelee na funzo lao la Biblia. “Kila juma mama yangu alipanga tutembelewe na mtu fulani kutoka Lejioni ya Maria (kikundi cha Aksio Katoliki) au kasisi,” akaeleza Dada Casey. “Lakini yule kasisi hakuweza kutumia Biblia kukanusha yale ambayo sasa sisi tulijua kuwa kweli. Mwishowe yeye alitoka kwa fujo ndani ya nyumba, akituhukumia adhabu ya moto wa mateso kwa kupotoa Maandiko!”

WAMISIONARI WAONGEZA KICHOCHEO

Wakati wa kumalizika kwa Vita ya Ulimwengu ya Pili, mapainia walitumwa kutoka Uingereza kwenda miji midogo katika Ailandi Kaskazini. Katika 1946, kwenye mkusanyiko katika Edinburgh, Uskochi, baadhi ya mapainia hawa walimwendea msimamizi wa Sosaiti wakimuuliza kama wangeweza kuhudhuria Gileadi. “Ndiyo,” yeye akajibu, “ikiwa ninyi mnaahidi kurudi Ailandi.” Akina dada watano walitimiza ahadi hiyo.

Kuwasili kwa wamisionari kutoka Shule ya Biblia ya Gileadi ya Mnara wa Mlinzi katika 1949 kuliongeza mwendo wa kazi. Maurice na Mary Jones, ambao walikuwa wamefanya ile kazi nyingi ya taabu, waliwapokea kwa furaha wafanya kazi hawa. Makao mawili ya wamisionari yalianzishwa, moja katika Dublin kwa msaada wa Ndugu Jones, lile jingine katika Cork. Kitabu cha Mwaka 1950 kilitoa elezo kwamba ilichukua kazi nyingi ngumu kumweka huru mtu mmoja kutokana na giza la kiroho ambalo lilifunika wengi sana, hasa kwa sababu wao walikuwa hawajapata kamwe kuona Biblia. “Wale watu,” kikasema, “wanaogopa kuachilia mapokeo yaliyotunzwa kwa muda mrefu sana, na kwa hiyo maendeleo ni ya namna ya kwamba yanahitaji busara na subira nyingi.”

Wale wamisionari waliowasili karibuni walieneza maeneo makubwa mno kwa miguu na kwa baiskeli zao, mara nyingi huku wakipatwa na mashambulio ya maneno na ya kimwili. Na wao walifanya kazi ngumu mpaka usiku sana ili kupalilia kwa upole upendezi wo wote uliopatikana.—Linganisha Hosea 11:4.

Mmoja wa wale wamisionari wa mapema, Elsie Levis (hapo kwanza Lott), alikumbuka jinsi yeye alivyokuwa amejitayarisha kiakili kwa ajili ya hali katika Ailandi. “Kabla ya sisi kuondoka Gileadi,” yeye akasema, “Ndugu Franz alituambia sisi kwamba kufuata India yeye alifikiria Ailandi kuwa mgawo ulio mgumu zaidi ulimwenguni. Kwa sababu ya mwelekeo wa Kanisa Katoliki, yeye alihisi kwamba hilo lilikuwa ndilo eneo gumu zaidi la Kikatoliki ulimwenguni.” Dada huyo aliuona kuwa mgumu. “Lakini,” yeye akaendelea, “sisi tulihisi, pia, kwamba wale watu walikuwa wamecharazwa-charazwa na kani za kisiasa na kidini, kwa hiyo sisi tulikuwa tunahangaikia tu watu kwa sababu wale watu wenyewe, chini ya ule uhasama wote, walikuwa watu wema sana.”

WAMISIONARI WAVUNJA KIZUIZI CHA KIKATOLIKI

Tendo la Wakatoliki wenye ghasia lilikuwa tisho la daima ambalo lilining’inia juu ya wamisionari kama wingu kubwa la mvua lililo tayari kupasuka dakika yo yote. Ili wasizushe shuku na kisha hasira-jeuri ya majirani, wamisionari wangefanya kazi kila mmoja peke yake wakiwa katika utumishi wa mlango kwa mlango lakini wakionana. Kabla ya kuondoka kao la kimisionari kwa utumishi, kila mmoja angefanya pamoja na mwenzi wake wa shambani mazoezi ya ishara za mkono na za kutikisa bega kwa siku hiyo. Ishara hizo zingekuwa onyo lililo kimya la watu wenye ghasia wenye kukaribia.

Mildred Barr (ambaye hapo kwanza alikuwa Willett, sasa akiwa Betheli ya Brooklyn pamoja na mume wake John) anakumbuka akianza utumishi wake wa shambani siku moja kwa pikipiki yake yenye rangi kijivu. Tumbi zake za ngozi zenye kugawanywa za hudhurungi nyeusi au sogi—zikiwa zimepakiwa vitabu vyake vya shambani, chakula cha mchana, chupa ya chai, na viatu vya kuvaa wakati wa theluji vilining’inizwa juu ya madigadi ya nyuma ya pikipiki. Yeye na Frieda Miller waliendesha pikipiki zao kwenye eneo la Kikatoliki la Dublin. Mara walipofika katika eneo, walitengana na kuegesha pikipiki zao katika mahali tofauti-tofauti, wakihakikisha kwamba pikipiki zao hazingeonekana na wenye nyumba lakini zikiwa karibu vya kutosha ili waweze kuzifikia kwa mbio ikiwa wangehitaji kutoroka upesi sana.

Mildred alifungia pikipiki yake kwenye nguzo kwa mnyororo na kufuli na akaanza kutoa ushuhuda nyumba kwa nyumba. Yeye anakumbuka: “Mimi nilikuwa nikisema na mwanamke aliyependezwa sana wakati kwa ghafula macho yake yalifunguka sana na kinywa chake kikalegea. Mimi niliuliza, ‘Kuna nini?’ Hapana jibu, isipokuwa tazamo la woga. Mimi niligeuka na kuelekeana na wanawake wenye ghasia wanane au tisa waliokuwa wakizuia njia kwenye lango la nyumba yake. Kwenye pembe ya jicho langu nilimwona Frieda akinipa ile ishara ya mkono, lakini ilikuwa kuchelewa mno. Wanawake wengine walikuwa wakipiga mbio kuelekea ile nyumba. Mimi nilijua kwamba singeweza kutoroka kupitia lile lango, kwa hiyo mimi nilikimbia kupitia shamba la mwenye nyumba, nikapiga mbio upesi kupitia bustani ya jirani wa karibu, na nikaruka ukuta, nikashughulika kwa shida kuelekea pikipiki yangu.

“Kufikia sasa Frieda alikuwa amepiga moto pikipiki yake; yangu ilikuwa ingali imefungwa kufuli. Mimi nilifungua kufuli na nikarukia kiti cha pikipiki, lakini pikipiki yangu ilikataa kuwaka. Mimi nilikuwa na plagi-cheche katika mfuko wangu! Kwa hiyo mimi nilichomeka ile plagi ndani ya injini, nikaipiga moto tena, na mimi huyo nikaondoka. Lakini haikuwa upesi vya kutosha—na hili ndilo jambo ambalo kila mmoja huchekelea mpaka leo hii. Mwanamke mmoja aliyekuwa akipunga-punga kipangusio alikimbia kunifuata nyuma. Yeye alitoma kichwa cha kipangusio katika shimo la mtaro wa takataka katika barabara ya mji. Nilipokuwa nikiondoka kwa pikipiki yangu mwanamke yule alisukasuka kile kipangusio. Kutoka kichwa cha kile kipangusio likaruka tope la takataka lililonifunika kutoka juu ya kichwa changu na kuteremka kufika mgongo wangu. Nilipomfikia Frieda, yeye alisema: ‘Jamani, Mildred, pyu-u-u! Tufikapo kwenye kao, usijaribu kuingia ndani ya nyumba!’

“Tulipowasili kwenye kao la wamisionari, yeye alimwambia yule dada mwingine misionari kilichokuwa kimetukia. Walitandaza manyusipepa nje karibu na bustani ili mimi nitembee juu yayo nao wakanimwagia ndoo za maji. Oh, kwa muda wa siku nyingi baadaye, kila mtu aliniazima manukato yao. Hata hivyo, hatimaye idadi fulani ya watu walikuja katika ukweli kutoka sehemu hiyo ya Dublin.”

Bridie Casey anakumbuka kisa kingine katika Dublin. Yeye alikuwa pamoja na misionari mmoja katika huduma ya shambani wakati mwanamke mmoja Mkatoliki alipowaambia kwamba wanafanya kazi bure tu. Ile roho ya wamisionari hao ilionyeshwa katika jibu la ndugu huyo. “Huenda ikawa hivyo,” yeye akasema, “lakini angalau dalili za kufaulu zinaanza kuonekana!” Ndiyo, wamisionari hao wakawa mtambo wa kubomolea uliobomoa zile kuta za kizuizi cha Kikatoliki zilizowatia kizuizini Waairishi wenye mioyo ya haki.

SHAMBULIO LA WATU WENYE GHASIA KARIBU LIMERICK

Ijapokuwa watu katika Ailandi kwa msingi walikuwa wenye urafiki na wakaribishaji-wageni, viongozi wa kidini walikuwa wangali na uwezo wa kuchochea baadhi yao kufanya jeuri. Katika Mei 13, 1956, misionari mmoja, Stephen Miller, alikuwa akisafiri pamoja na mhubiri mpya katika utumishi wa shambani katika eneo la mashambani katika magharibi ya nchi hiyo. Kwa ghafula yeye na mwandamani wake walikuta watu wenye ghasia wamezuia njia yao. Wao walirukia pikipiki zao ili watoroke. Lakini wale watu wenye ghasia waliwafuatia wakiwa katika magari na mwishowe wakawanasa katika barabara ambayo haikufika mbali.

Watu hao wenye ghasia, wakiongozwa na padri mmoja, walimsongelea Ndugu Miller. Mmoja wa hao wachokozi akapiga Ndugu Miller ngumi kidevuni. Kisha watu hao wenye ghasia wakamnyang’anya vitabu vyake na kuviteketezea katikati ya kile kijiji kidogo cha Cloonlara karibu Limerick.

Baadaye, kwenye jaribio la mahakama, ule upendeleo wa upande mmoja wa mahakama ulikaziwa. Yule padri na wachochea matata wengine wanane waliondolewa mashtaka kabisa. Yule mchokozi aliyepiga Ndugu Miller alipatikana na hatia lakini akaachiliwa. Kisha Ndugu Miller na mwandamani wake walifungishwa wajibu wa kuendeleza amani kwa kutozwa midhamana ya pauni 200 kila mmoja. Lo! ni dharau kama nini la haki! Ile mahakama iliachilia wale watu wenye ghasia na kuadhibu wale walioshambuliwa! Ingawa mji wa Dublin ulikuwa unafanya maendeleo katika njia yao ya kuwatendea Mashahidi, sehemu nyingi za mashambani zingali zilikuwa zikishikilia kwa ushupavu maoneleo na matendo yazo ya kikale.

VIWANGO MARADUFU VYENYE KUFADHAISHA

Yale matendo yasiyo ya haki na chuki zisizo na sababu nzuri dhidi ya Mashahidi wa Yehova yalikuwa wazi sana yasiweze kupita bila kuonekana. Utangazaji uliotokezwa katika nyusipepa kote kote katika ile Jamhuri ulileta wimbi la mateto na hasira. Kiongozi mmoja wa kidini Mprotestanti, ambaye hakupofushwa hata kidogo na kisetiri cha moshi cha kidini kilichokusudiwa kuvuruga yale masuala, alisema jambo la maana sana katika Dublin Evening Mail ya Julai 28, 1956, chini ya kichwa “Uhuru wa Kidini”:

“Washiriki wa Lejioni ya Maria hutembelea wanaparokia wangu ili kueneza mafundisho ya dini ambayo mimi nakataa kwa dhati. Unataka kuniambia kwamba sasa mimi naweza kukusanya watu wangu pamoja, niwakamate Walejioni, niteketeze vitabu vyao (na pengine nipige mmoja wao kwenye kidevu hata kukibonyeza ili kuonyesha tu kwamba sisi ni Wakristo pia!), na kisha nitazamie kwamba ikiwa wanalalamika watafungishwa wajibu wa kuhifadhi amani, na sisi tuachiliwe?

“Au je! kutakuwako sheria moja kwa Lejioni ya Maria na nyingine kwa Mashahidi wa Yehova?”

Wengine wengi, ingawa wao hawakukubaliana na mafundisho ya Mashahidi wa Yehova, walihisi kwamba lile andalio kuhusu uhuru wa kidini katika ile Katiba ya Jamhuri ya Ailandi lapasa kuheshimiwa. Fungu 44 la ile Katiba hutaarifu: “Uhuru wa dhamiri na uhuru wa dai na kuzoea dini huhakikishiwa kila mwananchi, kwa kupatana na utaratibu na maadili ya halaiki.”

Hata hivyo, ule uadui kuelekea watu wa Yehova na upinzani kwa kazi yao ulikuwa ungali wenye nguvu sana. Baadaye mwaka uo huo katika nyusipepa ya Limerick, ombi lifuatalo lilipelekwa kwa wasomaji Wakatoliki:

“Sisi tunaomba kwa moyo sana mtu ye yote ambaye huenda akafikiwa na wawakilishi wa ile Sosaiti [Mashahidi wa Yehova] asiwe na lo lote la kufanya na propaganda yao na akatae katakata kuingia katika mazungumzo yo yote pamoja nao. Nakala zo zote za vichapo vyao ambavyo wasomaji huenda wakawa wamejipatia zapasa kuharibiwa mara moja. Kanisa linataka kwa dhati sana sisi tuepuke mafundisho yao mabovu hivi kwamba Mkatoliki ye yote ambaye anasoma vichapo vya ile Sosaiti anajiacha mwenyewe wazi kutengwa na ushirika. Urithi wa Ailandi wa Imani, ulioshikiliwa kupitia karne nyingi za mateso, haupasi kubadilishwa na takataka ya mchuzi wa Brooklyn.”

“NJIA YA MUNGU NI UPENDO”

Katika kuangaza nuru ya Ufalme, kampeni moja ya pekee inatokeza. Kile Kitabu cha Mwaka 1954 kiliiita “pasipo shaka mchango ulio mkubwa zaidi sana wa kuhubiriwa kwa ukweli katika Eire [Jamhuri ya Ailandi.]” Ilikuwa nini? Ule mwenezo wa kote kote nchini wa kile kijitabu God’s Way Is Love Kijitabu hiki cha kurasa 32, kikiwa na vinubi vinne vya rangi kijani kwenye jalada lacho, kilinukuu kutoka chapa za Kikatoliki za Biblia pekee. Kilikuwa na vuto la pekee kwa watu wa Kikatoliki katika utoaji wacho mwepesi na ulio wazi wa mafundisho ya msingi ya Biblia. Arthur Matthews, ambaye sasa ni mratibu wa Halmashauri ya Tawi la Ailandi, na mke wake, Olive, pamoja na ndugu wa Olive na mke wake, walifanyiza kikundi kimoja kilichoshiriki katika kazi hii yenye kusisimua.

“Sisi tulichanga mali zetu,” Ndugu Matthews akasema, “nasi tuliweza kununua gari kuukuu aina ya Morris 10 kwa bei nafuu. Hakuna ye yote wetu ambaye angeweza kuendesha, lakini kwenye barabara moja tulivu karibu na kwa ‘Ma’ Rutland, upesi sisi tukapata kulizoea. Katika muda wa siku chache sisi tukaelekea mashambani na vifaa vyetu vyote vya kutolea ushuhuda vikiwa vimerundikwa ndani ya lile gari.”

Hata hivyo, hawakufanikiwa katika utafutaji wao wa mahali pa kulala, kwa hiyo wao wakalala usiku wenye baridi sana na usio na usingizi katika lile gari. Kesho yake wao waliamua kununua karavani au trela. Kulikuwako hatari katika hili, kwa kuwa karavani za akina ndugu katika wakati uliopita zilikuwa zimeshambuliwa na kuharibiwa, lakini wao hawakuwa na jambo jingine la kufanya isipokuwa hilo. Kwa kuuza baadhi ya milki zao, wao waliweza kupata pesa za kununua karavani ya urefu wa mita 4.3. Na ijapokuwa wao walikuwa na mambo yaliyoonwa ya kuogopesha walipoikokota juu ya barabara zenye mawe-mawe na nyakati nyingine zenye milima-milima, angalau tatizo lao la nyumba lilikuwa limetatuliwa.

Wao walikuwa na eneo kubwa la kueneza, kwa kuwa hakukuwa na mhubiri hata mmoja katika eneo lote la kusini mwa Dublin kuendelea mpaka mji wa Cork, kilometa 256 kuelekea upande wa kusini. Ili kutimiza mengi zaidi iwezekanavyo, kile kikundi kilianza utumishi wao wa shambani kila asubuhi saa 2.00. Wao walisafiri kwenye sehemu ya mbali zaidi sana ya eneo lao walilochagua na kisha wakafanya kazi wakirudi kuelekea mahali pa karavani yao. Ili kuzuia mashambulio yo yote juu ya mali yao, walipoanza kuhubiri katika maeneo yaliyo karibu na mahali ambapo walikuwa wameegesha karavani yao, wangeiondoa na kuiweka mahali papya. Walipofika kwenye miji mikubwa, wao walijaribu kutembelea watu wote kabla ya Jumapili, wakati ambao karibu bila kuepukika padri angewaparamia kutoka miambari yake.

Waume hao wawili shupavu na wake zao walipata watu wengi ambao hawakuwa wamepata kamwe kukutana na Mashahidi wa Yehova. Mara nyingi wenye nyumba walisema kwamba wao walikuwa wamekatazwa na kanisa lao hata kusoma Maandiko. “Kwa hiyo,” akasema Ndugu Matthews, “kuongezea kueneza kile kijitabu God’s Way Is Love, sisi tulichukua pia nakala za Biblia ya Douay ya Kikatoliki, ambayo sisi tulitumia na kuwatolea wale watu.”

Kijitabu hiki kilisaidia akina ndugu hao waondolee mbali lile wazo la kutembelea watu wa Kiprotestanti tu. Kila mmoja alifikiwa. Wao walieneza angalau nakala 20,000 za kijitabu hiki katika sehemu ya mashariki ya nchi ile, hali kikundi kingine kilifanya kazi hali moja na hiyo upande wa magharibi. Nao waliona kuwa watu wengi ni wakaribishaji-wageni. “Sisi hatukuwa kamwe na uhitaji wa kununua viazi au maziwa au vitu kama hivyo,” wakasema Ndugu na Dada Matthews.

HATIMAYE—JUMBA LA UFALME KATIKA DUBLIN!

Kufikia wakati huu kundi katika Dublin lilikuwa limekutana katika mahali pa kila aina, pasiwepo mahali po pote pa starehe. Kwenye mahali pamoja pa kukutana, orofa moja juu ya vibanda vya farasi vya madobini, halikuwa jambo lisilo la kawaida kutazama juu na kuwaona panya wakipuruka-puruka kupitia makombamoyo. Kwa hiyo akina ndugu wakaamua wakati ulikuwa umefika wa kupata mahali pa matumizi yao pekee. Baada ya kutafuta-tafuta sana, wao waliweza kukodi jengo moja ambalo lilikuwa limetumiwa kama gereji kwenye James Place, barabara moja ndogo ya kando karibu na Barabara Baggot upande wa kusini wa Dublin.

Kugeuza milki hii kuukuu iwe Jumba la Ufalme lenye kufaa ukawa mradi wa mioyo iliyo thabiti. Kwa jitihada nyingi akina ndugu walitengeneza-upya lile jengo kuukuu likawa Jumba la Ufalme zuri sana. Walikuwapo 134 wakati wa kuwekwa wakfu kwa jumba hilo katika 1953.

Katika Desemba 3, 1954, lile Jumba la Ufalme jipya lilikaribisha wageni wa pekee kutoka makao makuu ya ulimwengu—akina Ndugu Frederick W. Franz na Grant Suiter. Waliokuwapo ili kusikia ndugu hawa wakisema ni wamisionari zaidi ya 20, ambao walikuwa wakikiwasha moto kisiwa hiki kwa kazi yao ya kuhubiri Ufalme.

Katika miaka iliyofuata, hilo Jumba la Ufalme la Dublin lilitumika pia kuwa mahali pa makusanyiko yote ya mzunguko yaliyofanywa katika Jamhuri hiyo. Je! wewe unaweza kuwazia akina ndugu na dada wapatao 200 wakisongamana ndani ya kieneo kidogo cha meta 7 kwa meta 15? Watu wawili hawangeweza kupitia kile kingazi chembamba kilichoelekea kwenye sehemu ya orofa. Wakati wa makusanyiko, chakula kilipotayarishwa orofani, ilikuwa sharti kipitishwe kwa wale waliokuwa wakingojea chini, kutoka mkono mmoja kwenda kwa mkono mwingine, sahani moja baada ya nyingine. Hapakuwa mahali penye kupendeza kama ilivyo kwenye Majumba ya Ufalme ya ki-siku-hizi, lakini ikilinganishwa na baadhi ya mahali walipokuwa wakitumia, palikuwa paradiso.

AFISI YA TAWI YAANZISHWA

Ule mwaka 1957 uliona hatua nzuri ya kusonga mbele kwa ajili ya kazi katika Ailandi. Ndugu Knorr alipanga afisi ya tawi iliyo tofauti ianzishwe katika Dublin. Kufikia wakati huo Dublin ulikuwa umetumiwa kuwa depo ya vitabu, kazi ikiwa inaangaliwa na tawi la Uingereza.

Tawi hili jipya, lililoanzishwa katika nyumba yenye orofa tatu kwenye barabara Lindsay 86 katika upande wa kaskazini, sasa lingeweza kukaza fikira zalo zote kwenye mahitaji halisi ya shamba katika Ailandi. Hata hivyo, kwa wakati uliopo, Ailandi Kaskazini ilibaki chini ya mwelekezo wa tawi la Uingereza. Kazi katika Jamhuri ya Ailandi sasa ilikuwa isimamiwe kutoka hiyo afisi ya tawi mpya.

KUSHINDWA KWA JUMUIYA YA WAKRISTO KWAKAZIWA

Kwa kuelekewa na dharau la kidini lenye kuendelea, akina ndugu walifuliza kufunua Jumuiya ya Wakristo kuonyesha jinsi ilivyokuwa hasa. Chombo kimoja ambacho wao walitumia kilikuwa lile toleo la Novemba 1, 1958, la Mnara wa Mlinzi. Lilikuwa na azimio kutoka Mapenzi ya Kimungu Makusanyiko ya mwaka huo ambalo lilikazia kushindwa kabisa upande wa Jumuiya ya Wakristo kuelekeza watu kwenye Ufalme wa Mungu kuwa utatuzi halisi kwa matatizo ya wanadamu.

Gazeti hilo lilienezwa kwa mapana na marefu miongoni mwa viongozi wa kidini katika Ailandi. Nalo lilitokeza itikio lililoje! Nakala moja ilirudishwa ikiwa na neno “upuzi” likiwa limechorwa-chorwa juu ya ukurasa wa kwanza. Nyingine, iliyorudishwa na kiongozi wa kidini, ilikuwa na ujumbe huu:

“Msitume takataka hii kwangu mimi tena . . . Ninyi mnafanya kazi ya Ibilisi na mnaifanya kwa ajili ya pesa . . . Waacheni watu wema Waairishi. Wao hawatashawishwa nanyi kwa vyo vyote. Tena: Msipeleke kwa posta takataka hii kwangu mimi tena. Mimi sikusoma hata neno moja layo.”

Lakini baadhi ya wale “watu wema Waairishi” walikuwa na njaa kwa ajili ya ukweli na walikuwa wakiitikia. Hata hivyo, watu wengi, waliliona kuwa jambo gumu kuitikadi kwamba roho ya kweli ya kutaka kufanyia watu mema na upendo vilisukuma akina ndugu watumie wakati na mali zao kuwasaidia wengine wajifunze ukweli. Waliliona kuwa jambo gumu jinsi iyo hiyo kuitikadi kwamba wale walioitikia ule ukweli hawakufanya hivyo kwa ajili ya pesa. Hadithi nyingi za bandia zilienezwa juu ya jinsi wale wenye kupendezwa walivyopata pesa au manufaa nyinginezo wakati walipowasikiliza Mashahidi.

WASHAMBULIWA NA WATU WENYE GHASIA KATIKA WEXFORD

Yale mazingira ya kutangaza zile habari njema katika Ailandi yalikuwa yakipata maendeleo polepole. Lakini si watu wote waliokuwa na elekeo la kusikiliza kwa amani ule ujumbe wa Ufalme. Mathalani, acha sisi twende kwenye mji wenye mandhari nzuri wa Wexford, kusini mashariki mwa Ailandi. Mwaka ni 1960.

Ndugu na Dada Alex Turner walikuwa wamekuwa katika Wexford kwa miezi yapata kumi, wakati matata yalipotokea ghafula. Ndugu Turner alikuwa katika kazi ya nyumba kwa nyumba. Alipokuwa akiongea na baadhi ya watu, padri mmoja alikuja nyuma yake. “Nipe vitabu hivyo vichafu,” yule padri akapaaza sauti, akijaribu kunyakua mkoba wa kutolea ushuhuda wa Ndugu Turner. Umati, ambao ulitia ndani padri wa pili, ukakusanyika. Wakati Ndugu Turner alipokataa kumpa mkoba wake, yeye alishambuliwa na kupigwa. Hata hivyo, yeye na mke wake waliponyoka na wakaenda kwenye kituo cha polisi kuripoti shambulio hilo.

Ingawa hakukuwa na wahubiri walioishi katika Wexford wakati huo, jumuiya ya mahali hapo ilichemshwa na utendaji wa mapainia hawa. Chuki hii ilienea na kufikia mahakimu. Baadhi ya maelezo ya hakimu wa wilaya wakati wa jaribio lililofuata yanaelezea hili vizuri:

“Mimi nalazimika kukata maneno kwamba kesi hii imeendelezwa na kulazimishwa katika ile maana ya tamasha ya nyumba za mawonyesho kwa kusudi pekee la kuandalia utangazaji kwa ajili ya Mashahidi wa Yehova; kwamba watu hawa wanashiriki katika mpango wa hila ili kuvunjia heshima wale wanaofikiriwa kuwa viongozi wa kidini wapinzani; kwamba wao wanashiriki katika jambo ambalo kwangu laonekana kuwa jaribio la kijinga na lililotangulia kuhukumiwa ushinde la kuongoa watu wa nchi na mkoa huu. Wao wanalazimisha na wamekuwa wakilazimisha huduma yao isiyokaribishwa kwa wasikilizaji wasiotaka. . . . Hivyo nahisi kwa nguvu sana kwamba watu hawa wameanzisha shambulio juu ya imani ya kimapokeo ya watu wa Wexford, shambulio ambalo limeshindwa, litashindwa na lazima lishindwe.”

Hakukuwa na shaka kubwa sana mahali huruma za yule hakimu zilipokuwa na kulikuwa na uwezekano kidogo sana kwamba haki ingefanywa. Mbele ya mahakama, wale mapadri wote wawili walikana kwamba hawakumshambulia Ndugu Turner. Lakini walipatikana na hatia ya kushambulia kulingana na maoni ya mahakama—na kisha wakaachiliwa waende wakiwa huru kabisa!

Manyusipepa kote kote katika Ailandi na Uingereza yaliripoti tukio hilo. Kesi hiyo ya mahakama ilitokeza itikio lenye uhasama mwanzoni-mwanzoni. Lakini, kwa kweli, ilikuwa na matokeo fulani mema. Utangazaji wa manyusipepa kwa mintarafu ya ubaya wa matendo hayo yasiyopatana na sheria ya mapadri na watu wenye ghasia ulielekea kuzuia mwenendo kama huo usio halali. Wakati hasira ilipopoa, watu wenye kusababu waliona kwamba jeuri ya namna hii ilikuwa isiyokubalika.

Kwa kweli, wakati fulani baadaye, baada ya kundi kuanzishwa katika Wexford, mmoja wa wale mapadri waliohusika katika lile shambulio alikubali nakala moja ya kile kitabu Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele na akaomba radhi kwa mmoja wa wale ndugu kwa sababu ya sehemu yake katika tukio lile.

KUWAPO KWA MAPAINIA KWAHISIWA

Upande wa magharibi wa nchi, pia, wale mapainia waliendelea kufanya kuwapo kwao kuhisiwe. Hivi ndivyo nyusipepa moja ya mahali pale ilivyoeleza kazi yao: “Donegal imevamiwa kwa mara nyingine na sumbuo la wasumbuaji werevu zaidi sana kuliko mbweha au mbweha-ulaya. Jeshi la wanaume na wanawake, baadhi yao wakitalii kuzunguka-zunguka kwa mota-skuta, hufanya ziara nyumba kwa nyumba katika mji na sehemu za mashambani, wakiacha magazeti yao ya bure.”

“Jeshi” hili lilikuwa kubwa kadiri gani? Akina dada wawili mapainia waliotumia mota-skuta moja! Ni kitu gani kilichochea itikio hili? Ulikuwa ni ule mwenezo wa kote kote wa lile Amkeni! la pekee la Oktoba 8, 1960, lenye kichwa “Kanisa Katoliki Katika Karne ya 20.” Elezo la ile nyusipepa juu ya kazi ya kuhubiri iliyofanywa na hao mapainia wawili linatukumbusha sisi juu ya ‘jeshi la nzige’ lililoelezwa na mtume Yohana kwenye Ufunuo 9:1-10.

Mapainia kama hawa walishiriki fungu kubwa katika kufanya zile habari njema za Ufalme zihubiriwe wakati wa miaka ya 1950 na 1960. Ni makundi manne au matano tu yaliyokuwa yakitenda katika ile Jamhuri ya Ailandi wakati huo. Kwingineko kulikuwako vikundi vidogo tu vilivyokuwa peke yavyo vya mapainia na wahubiri, walioonyesha nia ya kuvumilia manyimo na magumu ya namna zote ili kutimiza huduma yao.

Kupata mahali pa kulala penye usalama lilikuwa lingali tatizo kubwa kwa mapainia katika migawo ya maeneo yaliyo peke yayo. Katika miji iliyo mingi lilikaribia kuwa jambo lisilowezekana kupata mahali pa kukaa. Mapainia wa pekee walio wengi waliliona kuwa jambo rahisi zaidi kukodi nyumba ndogo isiyo na fanicha katika maeneo ya mashambani nje ya miji, ambako hakukuwa na uwezekano mkubwa wa kutupwa nje. Kisha Sosaiti iliandaa fanicha ambayo mapainia walilipia kodi ndogo. Nyumba ndogo hizi zilitumika pia kuwa mahali pa kukutania kwa watu wenye kupendezwa. Uhasama ulipopungua, ndipo mapainia wa pekee wakaweza kuhamia mijini. Ile bidii-endelevu ya mapainia ilikuwa sababu kubwa katika ukuzi wa hesabu ya Mashahidi katika ile Jamhuri kutoka wahubiri 211 katika 1962 kufika 253 katika 1965.

MKUSANYIKO WA KIMATAIFA—DUBLIN, 1965

Wakati ilipotangazwa kwamba Mashahidi wa Yehova wangekuwa na mkusanyiko wa kimataifa katika 1965 katika Dublin, fadhaa ilipanda miongoni mwa halaiki ya watu. Kadiri matukio yalivyofunuka, ikawa wazi kwamba hesabu fulani ya watu haikutaka mkusanyiko huo ufanyike.

“Ilikuwa hadithi ya magumu—jambo moja tu baada ya jingine ambalo lingeelekea kufanya isiwezekane ule mkusanyiko uendelee,” akasema Arthur Matthews, msimamizi wa mipango ya mkusanyiko. “Lakini ile jitihada ya kutayarishia, na kuwa hasa na ule mkusanyiko ilitokeza roho nzuri miongoni mwa ndugu wote.” Wao walipiganaje na kivunja-moyo kadiri matatizo yalivyoongezeka? Ndugu Matthews aliweka kadi kwenye dawati yake iliyonakili maneno ya Mithali 24:10, NW: “Je! wewe umejionyesha mwenyewe kuwa mwenye kuvunjika moyo katika siku ya taabu? Nguvu zako zitakuwa haba.”

Upinzani mshupavu uliinua kichwa chao chenye kuchukiza miongoni mwa baadhi ya washiriki wa baraza la mji. Lilitaka mamlaka ikataze tumizi la viwanja vya mpira ambavyo vilikuwa vimekwisha kodishwa kwa ajili ya mkusanyiko. Diwani mmoja alibandika Mashahidi neno “tisho,” na washiriki wengine wa baraza wakahimiza sana kwamba haiwapasi Mashahidi waruhusiwe kutumia vifaa hivyo. Hata hivyo, diwani mwingine kwa hekima alitaja kwamba lingekuwa jambo baya ikiwa ruhusa ya kufanya mkusanyiko huo ingezuiwa katika nchi ambayo yenyewe ilikuwa imekuwa ikipatwa na mateso ya kidini kwa miaka mingi.

Bord Failte (Baraza la Utalii la Kiairishi) ilipendelea mkusanyiko uendelee. “Je! Bord Failte inajaribu kufanya taifa la Kiairishi kuwa baradhuli wa kuchekwa na ulimwengu?” akaandika mtetezi mmoja mwenye kasirani kwenye nyusipepa ya mahali pale. “Mwelekeo wayo lazima ufanyize tisho kubwa zaidi sana kwa Kanisa Katoliki kuliko ule utendaji wa Mashahidi wa Yehova na waendelezaji wengine wote wa dini ya bandia wakiwekwa pamoja.”

Mleta habari za magazetini mmoja alilinganisha Mashahidi na kile chama chenye sifa mbaya cha Ku Klux Klan na kile cha Mafia na akauliza, “Je! mtu ye yote anawataka watu hawa hapa?” Jambo hilo lilitokeza jibu lenye kuhurumia ambalo lilitaarifu kwamba yule mwandikaji aliyeshambulia Mashahidi wa Yehova “apaswa ainamishe kichwa chake kwa aibu.”

KUSHINDA VIZUIZI VYOTE

Mwishowe, ruhusa ilitolewa ili mkusanyiko uendelee. Lakini matatizo yalikuwa ndipo tu yanaanza. Lilithibitika kuwa jambo lisilowezekana kukodi mahali palipokuwa karibu kwa ajili ya vifaa vya kulishia. Hili lilikuwa hangaikio kubwa mpaka wasimamizi wa ule uwanja wakasema kwamba akina ndugu wangeweza kuinua marquee, au hema moja, kwenye uwanja wa mpira wenyewe. Hata hivyo, wale watu wa mahali pale walioleta ile marquee kwenye uwanja, walikataa kuiinua. Kwa hiyo akina ndugu, wakiwa na ujuzi kidogo tu katika mambo hayo, waliachwa wafanye hilo peke yao. Yehova aliingilia kwa msaada fulani. Wanaume kutoka shirika jingine, ambao walikuwa wakisafirisha meza na viti, walikuwa pia na ujuzi wa kuinua marquee. Wakati walipoona ile fadhaa, wao wakatoa msaada na mashauri mengi yenye mafaa na ya ustadi kwa akina ndugu.

Arthur Hewson, mwangalizi wa mkusanyiko, alikumbuka jinsi ilivyokuwa vigumu kupata vyumba kwa wajumbe wote waliotazamiwa. “Upesi kadiri vyumba vingeweza kupatikana, wale mapadri wangetumia mkazo na mahali pa kulala pangefutwa,” akasema. “Kwa ujumla, asilimia 50 ya vyumba vilivyopatikana vilifutwa, na hata baadhi ya mahoteli yalipatikana yakiwa ‘yamejaa’ wakati maombi yalipofanywa.” Siku fulani vyumba vingi zaidi vilifutwa kuliko vile vilivyopatikana.

Wale akina ndugu walisonga mbele wakiwa na uhakika wa kwamba ikiwa yalikuwa ni mapenzi ya Yehova, ule mkusanyiko ungefanyika. Hatimaye mahali pa kulala penye kufaa pa kutosha palipatikana katika makao ya watu wa Dublin kwa Mashahidi wa Yehova zaidi ya 3,500. Matokeo yakawa nini katika mji ule? Ile chuki isiyo na sababu nzuri dhidi ya Mashahidi ikaanza kubomoka. “Sisi hatukuwa tumeambiwa ukweli juu yenu,” wakasema baadhi ya wale wanawake wapangishaji-nyumba baada ya mkusanyiko. “Wale mapadri walituambia uwongo, lakini sasa kwa kuwa tumewajua ninyi, sisi sikuzote tutakuwa na furaha ya kuwa nanyi tena.”

Yajapokuwa yale matendo ya hila marefu kama mlima ya kufanya ule mkusanyiko ushindwe, hakuna lililofaulu. “Mimi sijapata kamwe kuwa kwenye kusanyiko ambapo roho ya Yehova haikuwapo,” akasema Ndugu Hewson, “lakini mimi sijapata kamwe kuhudhuria kusanyiko kabla na tangu hapo mahali ambapo roho ya Yehova ilidhihirika sana hivyo.” Ule ukali wenyewe wa upinzani ulifanya ule ushindi uwe wenye kustahili kuangaliwa zaidi. Ulitia nguvu uhakika wa akina ndugu katika ahadi ya Yehova: “Nao watapigana nawe; lakini hawatakushinda; maana mimi nipo pamoja nawe, ili nikuokoe, na kukuponya.”—Yer. 15:20.

KUFAULU KWELI KWELI

Huu mkusanyiko wa kimataifa wa 1965 ulikuwa tukio lenye maana kubwa katika utendaji wa watu wa Yehova katika Ailandi. Ulitokeza utangazaji mkubwa sana, mwingi wao ukiwa mzuri sana. Kwa mara ya kwanza televisheni ya taifa ilionyesha tamasha kutoka ndani ya mkusanyiko wa Mashahidi wa Yehova. Utangazaji mzuri wa habari pia ulitolewa kuhusu uzamisho. Kwa kuwa hakukuwa na mahali pa ndani ya jengo ambapo pangeweza kukodishwa, akina ndugu walipanga ubatizo ufanyiwe katika bahari pana, katika mahali pa kuogea palipo wazi karibu na boma la kuzuia mawimbi katika Ghuba Dublin. Hapo, wakistahimili mvua yenye kupiga na pepo baridi kali sana, watu 65 walionyesha wakfu wao kwa Yehova.

Katika siku ya mwisho ya ule mkusanyiko, Frederick W. Franz (ambaye baadaye akawa msimamizi wa nne wa Sosaiti ya Mnara wa Mlinzi Biblia na Trakti) alitoa hotuba yenye kuchochea juu ya kichwa “Serikali ya Ulimwengu Begani mwa Mwana-Mfalme wa Amani” kwa hadhirina ya 3,948. Ikitayarishwa kwa kufikiria sana watu wa Kikatoliki wa Ailandi, yeye alitumia maneno ya Biblia ya Douay ya Kikatoliki pekee. Lo! ushuhuda mzuri ajabu kama nini!

AILANDI YOTE CHINI YA TAWI MOJA

Mwaka uliofuata, 1966, ulileta hatua nyingine nzuri ya kiroho ya kusonga mbele—nchi yote, kaskazini na kusini, ilikuja chini ya mwelekezo wa afisi ya tawi katika Dublin. Kisiasa na kidini, Ailandi ilikuwa ingali imegawanyika kama zamani, lakini sasa watu wa Yehova walikuwa wameunganishwa katika kila njia. Mwaka huo uliona Mashahidi 268 katika Jamhuri ya Ailandi na 474 katika Ailandi Kaskazini, udugu mzuri ajabu wa 742 ukishirikiana pamoja ili kufanya mapenzi ya Yehova.

KUTOKUWAMO IJAPOKUWA MIKAZO

Ile miaka yenye msukosuko ya 1970 na 1980 iliona harakati za utukuzo wa taifa zikikua na matendo ya uvamizi wenye kutia woga yakiongezeka sana, hasa katika Ailandi Kaskazini. Matokeo yakawaje? Kujikusanya pamoja na kuongezeka kwa jamii za Kikatoliki na za Kiprotestanti zenye kupingana katika sehemu hii ya kaskazini-mashariki ya kisiwa kile.

Norman Richards alikuwa mmoja wa waangalizi wa mzunguko katika Ailandi Kaskazini wakati matata yalipoanza. Yeye anakumbuka jinsi akina ndugu walivyokazwa wajiunge na upande huu au upande ule.

“Jitihada zilifanywa kuwafanya akina ndugu waunge mkono askari-doria usiku na wajiunge katika kuinua vizuizi vya kufunga maeneo yao,” akasema Ndugu Richards. “Hao askari-doria waliomba michango ili kulipia vifaa walivyohitaji ili kulinda eneo lao. Nao walijaribu kuangika bendera za utukuzo wa taifa kwenye majengo yote.”

Akina ndugu walisimama imara walipoelekewa na vitisho. Hakuna aliyeacha kutokuwamo kwake, na upesi ikawa wazi kwa wote kwamba wao walikuwa hawamo kabisa katika shindano hili. Upesi watu waling’amua mwelekeo wa Mashahidi juu ya vita, maoni yao juu ya bendera, na azimio lao la ‘kutokuwa sehemu ya ulimwengu.’—Yn. 17:16, NW; Isa. 2:2-4; 1 Kor. 10:14; 1 Yn. 5:21.

Aghalabu, wakati akina ndugu walipoeleza wazi msimamo wao, hilo lilizusha uhasama katika jumuiya. Majirani waliounga mkono vitendo vya jeshi la mgambo mara nyingi walikataa kuzungumza na akina ndugu. Lakini, baada ya muda, kadiri akina ndugu walivyoendelea kuwa wenye fadhili na wasaidifu katika njia ambazo zilikubalika Kimaandiko, walikubaliwa tena na jumuiya, na msimamo wao wa kutokuwamo kabisa ukatambuliwa.

KUJIFUNZA KUISHI PAMOJA NA TAABU

Wakati jeuri ilipokuwa kwenye kilele chayo, kulikuwako hatari ya daima ya kufyatuliwa kwa bunduki na kutupwa kwa mabomu katika sehemu mbalimbali za mkoa. Kazi ya kutoa ushuhuda ilipungua mwendo kwa sababu watu waliogopa kufungua milango yao baada ya giza kuingia. Lakini utendaji wa ziara za kurudia na kazi ya funzo la Biblia la nyumbani iliendelea kwa haraka.

Kwa kueleweka, watu waliwaogopa watu waliozuru ambao wao hawakuwatambua. “Alasiri moja ya Jumapili,” akakumbuka Ndugu Richards, “sisi tulibisha mlango na mwanamume mmoja akaufungua kwa tahadhari. Sisi tulijitambulisha wenyewe na kumwambia ni kwa sababu gani tulikuwa tunamtembelea. Yeye aliondoa mkono wake kutoka nyuma, nasi tukaona kwamba ulishika bastola iliyokuwa na risasi. ‘Mimi ni polisi,’ yeye akasema, ‘nami nilifikiri ninyi huenda mkawa mmetoka kwenye IRA.’”

Akina ndugu walijipatanishaje ili waishi chini ya hali za namna hiyo ya vita? Wao walifuata shauri la Yesu katika Mathayo 10:16 kuwa “na busara,” wakijiepusha na vitendo vyo vyote vya upumbavu. Walipokuwa katika huduma, ikiwa bomu lililipuka ujiranini, wao wangetumia tu tukio hilo katika mahubiri yao, wakisema jambo kama hili: “Je! wewe unajua kwamba Mungu anaahidi kutakuwa na mwisho wa jambo kama hilo?” na kisha wangeendelea na mazungumzo yao. Bila shaka, jeuri haikupiga sehemu zote za Ailandi Kaskazini; wala hakukuwako milipuko ya vitendo vya wavamizi wenye kutia woga nyakati zote. “Sisi hatukuwa tukiepa mabomu na marisasi kila siku,” akasema ndugu mmoja. “Wakati ulio mwingi ulikuwa bila matata.”

KWENDA KOTE KOTE PAMOJA NA HABARI NJEMA

Mapema muda wa tangu 1970 wanajeshi wa mgambo walikuwa wameonya akina ndugu kwamba wangepigwa risasi ikiwa wangeingia katika maeneo fulani. Tahadhari ilitaka tuache kwa muda. Hivyo, maeneo kadha wa kadha ya Kikatoliki katika Belfast hayakuwa yakienezwa katika kazi ya kutoa ushuhuda. Mmoja wa akina ndugu alieleza jinsi alivyoanza tena kutoa ushuhuda katika maeneo hayo. Yeye aliishi kwenye ukingo wa mitaa ya Wakatoliki na Waprotestanti katika Belfast. Yeye na mke wake walichukua mtoto wao mchanga pamoja nao katika kigari cha kubebea mtoto, na polepole wakafanya kazi zaidi na zaidi kuingia sehemu ya Wakatoliki, upesi mapainia wawili wa pekee wakajiunga nao. Polepole wakawa wenye kukubalika zaidi, na upesi wakawa wamefanya mipango ya vikundi vya kutoa ushuhuda katika maeneo haya kadiri wahubiri wengine walivyojiunga nao.

Ni nini kilichowapa himaya Mashahidi katika maeneo ya Kikatoliki? Kutokuwamo kwao. Jambo moja lililoonwa linatoa kielezi cha hili: “Yapata miezi mitatu au minne baada ya sisi kuanza kufanya kazi katika eneo moja, mwanamume mmoja alitukaribisha ndani ya nyumba moja. Mazungumzo yalipokuwa yakiendelezwa, yeye alituambia kwamba Mashahidi wa Yehova wanakaribishwa katika eneo hilo. Yeye alitambua kutokuwamo kwetu katika mambo ya kisiasa, jambo ambalo yeye alisema lilikuwa tofauti kabisa na utendaji wa mapadri wengi. Wakati nilipotaja kwamba mimi nilikuwa nimekuwa nikitembelea eneo hilo kwa muda fulani, yeye aliweza kutuambia sisi wakati na mahali tulipoingilia kwa mara ya kwanza eneo hilo na kwamba sisi tulikuwa tumekuwa tukichunguzwa tangu hapo!”

Katika pindi moja jeshi lilimsimamisha ndugu huyu na kumchukua kwenye makao makuu ya kijeshi ahojiwe. Wao walimtaka yeye awe mtoa-habari kwa majeshi yao ya usalama na awe mpelelezi alipokuwa akiendelea na kazi yake ya kuhubiri. Hata hivyo, baada ya yeye kueleza msimamo wake wa kutokuwamo kuhusiana na siasa akiwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova, wao walimwacha aende.

Hesabu fulani ya akina ndugu kutoka Uingereza walikuwa wamehamia kundi moja katika mji uliokuwa karibu na eneo la mpakani kati ya Ailandi Kaskazini na Jamhuri ya Ailandi. Katika kipindi cha miaka miwili au mitatu, kitovu cha mji kilikuwa kimebomolewa na mabomu mara zipatazo 200, mbali na vitendo vya ghasia na mitupo ya risasi iliyofanywa karibu kila usiku. Lakini wakati huu wote akina ndugu walihisi mkono wa Yehova wenye kutoa himaya. Nyakati nyingine watu wa mahali hapo waliwaonya Mashahidi kabla ya matata kulipuka. Kujapokuwa ule msukosuko wa daima, akina ndugu sikuzote walifanya mikutano yao na wakaendelea na huduma yao. “Majeshi ya ulinzi nyakati nyingine yalinyimwa ruhusa ya kuingia maeneo fulani,” akasema Shahidi mmoja wa mahali, “lakini akina ndugu sikuzote waliweza kuingia na kufanya kazi ya kuhubiri, hata ingawa hesabu fulani yao walikuwa Waingereza, kwa sababu wao sikuzote walikuwa wameeleza wazi kutokuwamo kwao.”

UTAMBULISHO WENYE KOSA

Ingawaje, pindi fulani-fulani, baadhi ya wahubiri katika kazi ya kuhubiri walijikuta wenyewe katika mahali penye hatari. Kwa kuitibari katika Yehova na kudumisha hali ya utulivu, akina ndugu waliponyoka wasipatwe na jeraha baya. Mathalani, ndugu mmoja kijana painia wa pekee alifikiriwa kimakosa kuwa mshiriki wa majeshi ya usalama. Yeye anaeleza hivi:

“Mimi nilikuwa nikifanya ziara za kurudia fulani katika mtaa wa kuwapa watu nyumba uliojulikana kuwa ulishiriki sana maoni ya IRA, wakati gari moja liliposimama. Mmoja wa waliokuwamo alinilenga kwa bunduki na kuniamuru niingie ndani ya gari. Wale wanaume katika gari wakanipekua-pekua mara hiyo. Mwanzoni mimi nilifikiria ningepigwa risasi kwa sababu wao walikuwa wamenichukua kimakosa kuwa mwanajeshi katika mavazi ya kiraia. Nilipelekwa kwa gari kwenye nyumba moja na kufungiwa katika kibanda kidogo kwa wakati ulioonekana kwangu kuwa muda wa maisha yote. Kisha nilitolewa nje, nikafungwa macho, na kuongozwa ndani ya nyumba moja ambamo niliulizwa maswali kwa muda mrefu kuhusu mimi ni nani na yale niliyokuwa nikifanya katika lile eneo. Tangu mwanzo kabisa nilikuwa nimesali kwa Yehova kwamba nisiwape sababu yo yote ya kutenda kupita kiasi kwa sababu ya lo lote nililosema au kufanya.

“Mimi nilieleza kwamba nilikuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova na kwamba nilikuwa tu napendezwa katika kusaidia watu waelewe Biblia. Niliweza kusikia wanaume kadha wakipekua-pekua vifaa vya mkoba wangu wa utumishi na wakisema-sema mambo fulani kuhusu maandishi yangu ya nyumba kwa nyumba. Mmoja wao akaondoka chumbani, akisema: ‘Endeleeni kumlenga kwa bunduki, na ikiwa yeye anajongeza hata kidogo—mlipulie mbali kichwa chake!’ Hatimaye mwanamume huyu akarudi. Lazima yeye awe aliweza kuthibitisha hadithi yangu kwa sababu yeye aliwaambia wengine ningeweza kuachiliwa. Nikiwa ningali nimefungwa macho na kulengwa kwa mtutu wa bunduki, nilirudishwa kwenye gari na nikaachiliwa karibu na kitovu cha mji.

“Mimi nina hakika kwamba roho ya Yehova iliniweka nikiwa mtulivu kabisa, nikiweza kusema na kufanya mambo yanayofaa hivi kwamba walikubali kwamba mimi nilikuwa simo kabisa. Alasiri iyo hiyo mwenzangu aliambatana nami kwenda kwenye ziara ya kurudia iliyokuwa imepangwa kwa mtu mwenye kupendezwa katika mtaa ule ule wa kuwapa watu nyumba, na hatimaye tukafanya kazi huko mara nyingi bila ya kutaabishwa tena.”

WATAMBULIWA KUWA MASHAHIDI

Katika pindi nyingine wawili wa mapainia walikuwa wakifanya kazi katika ule mji mdogo wa mpakani Crossmaglen upande wa ndani tu wa Ailandi Kaskazini. Wao walikuwa hawajulikani na wengi katika eneo hilo. Pasipo wao kujua, vikaratasi vilikuwa vimegawanywa karibuni na IRA kuonya watu katika mji huo kuhusu kuwasili kulikokaribia kwa kikosi maalumu cha Jeshi la Uingereza, SAS—kikosi kilichopewa mazoezi ya hali ya juu sana ambacho mara nyingi kilifanya kazi bila kuvalia mavazi ya kijeshi. Watu wa mahali pale walishuku kwamba wale akina ndugu mapainia walikuwa washiriki wa kile kikosi cha SAS.

Wakiwa tayari kurudi nyumbani baada ya kumaliza ziara zao za utumishi wa shambani, wale akina ndugu walitua wapate kikombe cha kahawa wanapongojea basi. Walimuuliza mwanamke katika hoteli ikiwa basi lilikuwa limewasili mjini. Kwa kasirani mwanamke aliwashtaki kuwa askari na kisha akatoka nje. Wale akina ndugu waliondoka pia kwenye ile hoteli. Walipokuwa wakisimama wakingojea basi, wanaume fulani wakawasili kwa gari, wakaenda ndani ya ile hoteli ya kahawa, muda mfupi baada ya hapo wakatoka kwenye ile hoteli, na kisha wakaendesha gari lao polepole kuzunguka ule uwanja kwenda walipokuwa wale akina ndugu wakingojea na kuwauliza maswali fulani. Wale ndugu waliitikadi kwamba wao walikuwa washambulizi wa kutumia bunduki wa IRA. Ndugu hao wanatusimulia yaliyotokea baadaye:

“Basi liliwasili, gari kuukuu lililobondeka-bondeka. Sisi tulilipa nauli zetu na kuingia ndani. Ndipo tulipoona kwamba wale wanaume waliokuwa wametuuliza-uliza maswali walikuwa wakiongea kwa bidii sana na dereva wa basi. Upesi baada ya hapo lile basi likaanza mwendo, lakini wakati ule ule lile gari lililojaa wanaume likaanza mwendo. Sisi tuliogopa kwamba mpango fulani ulikuwa umefanywa wakutane mahali fulani penye utulivu kwenye barabara ya mashambani nje ya mji. Usiku uliotangulia tu minibasi moja ilikuwa imesimamishwa katika eneo lile, na watu kumi walikuwa wamepangwa mstari na kupigwa risasi, tisa kati yao wakauawa.

“Zile kilometa ndefu kwenda nyumbani zilielekea kutokuwa na mwisho, lakini tulipokuwa tukikaribia mji tuling’amua hakuna lo lote ambalo lingetukia. Tulipomuuliza dereva asimame tushuke, yeye aliuliza, ‘Niambieni, je! ninyi mna vyo vyote vya vitabu vyenu?’ Kwa wazi yeye alitujua, nasi tulimpa yeye nakala za karibuni za Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Ndipo tulipomuuliza wale wanaume waliotuuliza maswali walikuwa akina nani. ‘Ah, msijali,’ yeye akajibu. ‘Mimi nilijua ninyi ni akina nani. Mimi niliwaeleza vizuri. Msijali hata kidogo. Ninyi mko salama kabisa sasa!’”

MASIKIO YENYE KUITIKIA KATIKA MAENEO YA KIKATOLIKI

Kwa miaka mingi katika Ailandi Kaskazini itikio lililo jingi kwa ukweli lilikuwa limeonekana katika maeneo ya Kiprotestanti. Lakini sasa Wakatoliki zaidi na zaidi walidhihirisha kupendezwa walipoanza kuona kwamba mfumo huu hauna cho chote cha kuwatolea na kwamba kanisa lilikuwa limeshindwa kushikamana na kanuni za Biblia. Mwanamume mmoja kijana Mkatoliki, aliyekuwa akifanya kazi kama muuguzi, alikutwa katika kazi ya nyumba kwa nyumba. Maitikio yake yalikuwa nini?

“Walikuwa Waingereza,” yeye akasema kuhusu ndugu waliomtembelea, “na mwelekeo wangu wa kwanza ulikuwa kwamba hakuna mgeni anayepaswa kuja na kufundisha sisi dini katika Ailandi.” Hata hivyo, wale akina ndugu kwa ustadi walitumia Biblia kujibu vipingamizi na maswali yake. Baada ya dharau lake kugeuka kuwa heshima, yeye alikubali nakala ya kile kitabu Kweli Iongozayo Kwenye Uzima wa Milele. Yeye alitamani sana kujua zaidi juu ya neno la Mungu, kwa kuwa yeye aling’amua kwamba yeye hakujua cho chote juu ya Biblia hata ingawa watatu wa wajomba wake walikuwa makasisi Wakatoliki. Hata hivyo, hali yake ya kikazi ilibadilika, naye akapoteza mwonano na akina ndugu.

Kadiri matata katika Ailandi Kaskazini yalivyoongezeka, yeye alijionea mwenyewe hospitalini ambako alifanya kazi yale matokeo yenye kuogopesha sana ya mitupo ya marisasi na mabomu. Akijaribu kuepukana na hofu hizi, yeye alianza kuvuta sigareti na kunywa pombe sana. Yeye hakuweza kujizuia ila kuuliza, “Ni kwa sababu gani yote haya yanatukia? Ni kwa sababu gani Mungu anayaruhusu?” Hata hivyo, kupitia yote hayo, yeye alikumbuka mwonano wake wa kwanza pamoja na ukweli, naye aling’amua kwamba majibu yamo katika Biblia. Yeye alianza kunyoosha maisha yake na akasali kwa Mungu kwa ajili ya msaada.

Alipotembelea kao la wazazi wake, mshangao wenye kupendeza ulimngojea. Ndugu yake mdogo alikuwa akijifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova! “Sisi tulikaa mpaka saa kumi asubuhi tukizungumza mambo aliyokuwa akijifunza ndugu yangu,” yeye akaeleza. “Lilikuwa jambo zuri ajabu kujifunza kwamba kuna Mungu anayejali, ambaye atasafisha dunia na kuondoa ugonjwa na kifo. Ilikuwa ni lazima tu mimi nijifunze zaidi.”

Yeye alirudi kazini mwake katika Londonderry. Asubuhi moja kengele ya mlango ililia. Kwa kawaida hangesikia ile kengele, kwa kuwa yeye alifanya kazi ya zamu ya usiku, lakini wakati huu yeye aliamka na kwa usingizi yeye akaenda mlangoni. Dada wawili, wakifikiri kwamba hakuna aliyekuwa nyumbani, walikuwa wanateremka kurudi kwenye kijia. Yeye aliwauliza kama wao walikuwa Mashahidi wa Yehova. “Waliposema ndiyo, moyo wangu uliruka kwa shangwe,” yeye anasimulia, “nami nikawaomba funzo la Biblia!” Kama ilivyo kawaida ya wengine wengi wenye malezi ya Kikatoliki, yeye alifanya maendeleo ya haraka kuingia katika ukweli.

KUONA ULE UVUMBUZI HALISI WA ZILE TAABU

Katika eneo jingine la Ukatoliki wenye nguvu la Belfast, wanawake wawili vijana walikuwa wametatanishwa katika lile shindano la kisiasa na utendaji wa jeshi la mgambo la siku zile. Hatimaye wakafahamu kwamba hivi sivyo mambo yanavyopasa kuwa. Walianza kutia mashaka juu ya chuki walizoona kati ya washiriki wao, pamoja na ukosefu wa heshima kwa uhai ulioonyeshwa na watu mmoja mmoja waliokuwa na nia ya kulemaza na kuua kwa masilahi ya kusudi lao.

Wakati mmoja wa wahubiri alipotembelea kao lao na kusema nao juu ya ukweli, mwanzoni wao walitia shaka. Lakini polepole wao wakaja kuona kwamba ahadi ya Mungu ya serikali ambayo ingenyoosha mambo duniani ilikuwa ndiyo uvumbuzi pekee wenye mafaa kwa matatizo yaliyokuwa yakisumbua Belfast. (Zab. 46:8, 9; Isa. 2:4; Dan. 2:44) Pale mwanzoni ilikuwa vigumu kwao kuitikadi kwamba ye yote angeweza kuwa bila kuwamo katika mazingira kama yao, lakini kadiri walivyoshirikiana na wale akina rafiki kwenye Jumba la Ufalme, wao waliona kwamba kutokuwamo kwa Kikristo kuliwezekana. Wao walikuja kuona umoja halisi na upendo ulioonyeshwa miongoni mwa wafuasi wa Kristo na upesi wakaja kuingia katika ukweli.—Yn. 13:34, 35.

YEHOVA AENDELEA KUIFANYA IKUE

Yehova anaweza kufanya mbegu ya ukweli ikue katika mioyo ya watu, hata ingawa huenda ikakaa bila kufanya lo lote kwa miaka mingi. (1 Kor. 3:6, 7) Watu kama hao wanaweza kwa ghafula kufanya maendeleo ya haraka kuingia katika ukweli. Hilo lilitolewa kielezi kwa dada mmoja ambaye alikuwa akishiriki katika kutoa ushuhuda barabarani.

“Mimi nilishtuka kidogo kuona mwanamume mmoja aliyekuwa na mfuko wa bidhaa alizonunua dukani katika kila mkono akinijia akiwa na kusudi sana,” yeye akasema. “Alisimama, akaweka mifuko yake chini, na kuniuliza kama mimi ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova. Niliposema nilikuwa mmoja wao, yeye aliomba nakala moja ya ‘kile kitabu chekundu,’ Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Ndipo ukaja ule mshangao. Yeye aliuliza kama mtu fulani anaweza kumtembelea ajifunze Biblia pamoja naye!”

Mwanamume huyu alikuwa amepokea nakala ya kile kitabu “Babylon the Great Has Fallen!” God’s Kingdom Rules! kutoka kwa mfanya kazi mwenzake katika 1963. Yeye alikisoma, akaona kwamba huu ulikuwa ndio ukweli, lakini hakufanya lo lote juu yao. Baadaye, alipokuwa angali mseja, yeye alisali kwa Yehova, akifanya ahadi kwamba ikiwa Yehova angemwandalia mke na watoto, yeye angewalea watoto wamtumikie Yehova. Sasa, miaka 20 baadaye, akiwa amefunga ndoa na akiwa na watoto wanne, yeye alikuwa bado hajatimiza ahadi hiyo. Kwa sababu ya matatizo ya kibinafsi, yeye alikuwa katika hatari ya kupoteza jamaa yake.

Akiuona uhitaji wake wa kiroho, yeye aliwatafuta akina ndugu. Yeye alijua kutokana na mmoja wa jirani zake ni kona gani ya barabara ambapo Mashahidi wangeweza kupatikana kila Jumamosi karibu wakati wa chakula cha mchana. Kwa hiyo huyo akaenda kuwatafuta. Tangu mwanzo yeye alianza kuhudhuria mikutano kwa ukawaida, akileta watoto wake pamoja naye. Kadiri alivyothamini zaidi viwango vya Yehova, yeye alianza kufanya mabadiliko katika maisha yake. Yapata miezi miwili baada ya yeye kukutana na akina ndugu, yeye alikuja kwenye kusanyiko la mzunguko lake la kwanza, jambo ambalo lilimpa yeye nguvu ya kuacha zoea la kuvuta tumbako.

Ndipo likaja jaribu kweli kweli. Kama tokeo la upinzani kutokana na jamaa yake, mke wake alikataa kusema naye kwa majuma na hatimaye akatisha kutengana naye ikiwa yeye hangeacha ukweli. Ilikuwa kinyume cha mambo kwamba kile kitu ambacho yeye alikuwa amejia katika ukweli akiokoe, yaani, ndoa yake, sasa kikawa kinatishwa kama tokeo la kumtumikia Yehova. Hata hivyo, kwa hekima yeye alisababu kwamba kwa kutupilia mbali ukweli sasa, hatimaye yeye angepoteza kila kitu kwa ajili yake mwenyewe na jamaa yake. Kwa hiyo yeye akasimama imara. Kama ilivyotukia, mke wake kwa kweli hakutaka watengane bali yeye alikuwa tu anashindwa na mkazo wa jamaa. Sasa yeye anakubali kwamba kama haikuwa ni kwa sababu ya mume wake kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova, wao hawangeendelea kuwa pamoja.

UKUZI WENYE KUENDELEA KATIKA ILE JAMHURI PIA

Katika ile Jamhuri ya Ailandi, pia, ule uendelevu wa akina ndugu na dada katika kuangaza ile nuru ya ukweli kila mahali ulianza kuleta matokeo.

Mume na mke mmoja Wakatoliki walikuwa wamehuzunishwa na kifo cha binti yao mwenye umri wa miaka minne. Watu fulani walisema kwamba ilikuwa sharti afe “kwa sababu Mungu alitaka yeye katika mbingu” na kwamba “yeye hakukusudiwa kamwe awe katika ulimwengu huu.” Jambo hilo halikueleweka hata kidogo kwa wazazi hao wenye kuhuzunika. “Sisi tulikuwa Wakatoliki wazuri,” wao wakasema. “Sisi tulienda kwenye Misa nasi tuliitikadi katika Mungu, lakini sisi hatungeweza kuelewa ni kwa sababu gani ilikuwa lazima yeye afe!”

Yule mama akaanza kujifunza, lakini mume wake, mwanzoni, hakuvutiwa na ukweli. ‘Hakuna ukumbusho wa siku za kuzaliwa! Hakuna Krismasi! Kuwa na sharti la kwenda kwenye mikutano hiyo yote! Kuwa na sharti la kuacha kuvuta sigareti! Hayo mimi siwezi,’ yeye akafikiri. Lakini ndani ndani sana yeye alimheshimu mke wake kwa kujitolea kwake Yehova kulikokuwa kukikua. Mwanzoni wakati akina ndugu walipokuja kwa ajili ya funzo la Biblia, yeye angetorokea mlango wa nyuma. Hata hivyo, baadaye, yeye alikaa na kusikiliza na akaanza kuona thamani ya ukweli.

Yeye alishtuka kujifunza kwamba Yehova alikuwa, kwa kweli, yule Mungu wa kweli. “Mimi nilifikiri yeye alikuwa Mwamerika fulani milionea” yeye akasema. Hatimaye ile jamaa ikaunganishwa katika kumtumikia Yehova. Imani yao katika yule Mungu wa kweli iliwapa imara kubwa ya kuvumilia wakati mwana wao aliye mkubwa zaidi alipokufa kwa ghafula sana kwa ugonjwa wa lukemia. “Kama sisi hatukuwa tumejua ukweli na kuwa na wale marafiki katika kundi, sisi tungalijiua wenyewe,” yeye akakiri.

Mwanamume mwingine Mkatoliki alitatizwa na ukosefu wote wa haki na kuteseka katika ulimwengu. Ile vita ya Vietnam, zile hofu za Biafra, yale mamilioni ya watu wanaokufa kwa ukosefu wa chakula katika ulimwengu wenye wingi wa vyakula—yote yalionekana kutofaa sana. Ili kufutilia mbali mambo haya ya hakika yenye kuhuzunisha, yeye alianza kunywa pombe sana. Alipofikiwa na ujumbe wa Biblia, alielezwa sababu za mfumo huu wa mambo wa kishetani wenye kuogofya.

Yeye alifanya maendeleo katika ukweli na akahusika kabisa katika utumishi wa Yehova. Alipokuwa akitembelea baadhi ya akina ndugu katika Belfast, yeye alijiunga nao katika kazi ya nyumba kwa nyumba katika eneo la mji la Washikamanifu (waliopinga Utetezi wa Taifa). Kabla ya hilo, yeye hata hangefikiria kamwe kutembelea Ailandi Kaskazini, achilia mbali kuthubutu kuingia katika eneo la Washikamanifu. Hata hivyo, alikuwa hapo. Alialikwa ndani ya nyumba moja, naye mwenye nyumba akang’amua kwamba yule ndugu alikuwa amekuwa Mkatoliki. Kwa hiyo yeye akamuuliza: “Wewe ulipokuwa Mkatoliki, je! uliunga mkono IRA?” Yule ndugu aling’amua kwamba mwanamume huyu angeweza kugeuka na kuwa mjeuri, kwa kuwa alikuwa ameachiliwa karibuni kutoka kizuizini baada ya kukamatwa akiwa na bunduki alipokuwa akienda kumuua Mkatoliki. Kwa hiyo yule ndugu akasema: “Mimi si Mkatoliki sasa. Mimi ni mmoja wa Wakristo mashahidi wa Yehova. Nikiwa Mkristo wa kweli, mimi singeweza kumuua ye yote kwa ajili ya serikali yo yote au mtu ye yote.” Kusikia hayo yule mwenye nyumba alimsalimia kwa mkono na kusema: “Kuua ko kote ni kubaya. Ninyi watu mnafanya kazi njema. Endeleeni kuifanya.”

KUTUMIKIA AMBAKO UHITAJI NI MKUBWA ZAIDI

Msaada uliokuwa mkubwa katika kuongeza mwendo wa kazi katika Ailandi ulikuwa ule moyo wa kupenda wa ndugu wengi kutoka nchi nyingine kuondoka ili kutumikia mahali ambako uhitaji ulikuwa mkubwa zaidi. Wao waliitikia mwito kama ule uliosikiwa na mtume Paulo: “Vuka, uje Makedonia utusaidie.” (Mdo. 16:9) Ilihitaji upendo wenye kina kwa ajili ya Yehova na roho halisi ya kujidhabihu. Lakini matokeo na thawabu vimekuwa vyenye kutokeza.

Bila shaka, kulikuwako magumu ya kushinda, kama vile kupata kazi ya kuajiriwa na kupangia elimu ya watoto. Lakini akina ndugu na dada hawa walimweka Yehova kwenye mtihani, na yeye hakushindwa kamwe kuwasaidia. “Watoto wetu walistarehe kwa urahisi,” wakasema mume na mke mmoja, “nasi tulipata kuona kwamba tumejihusisha zaidi katika mambo ya kiroho kama jamaa yakiwa matokeo ya kuhamia hapa.” Kichwa mmoja wa jamaa alitaja jinsi jamaa yake mwenyewe ilivyonufaika kutokana na kuhamia Ailandi. “Kumetusaidia tuepuke kuvutwa kando kwenye vitu vya kilimwengu,” yeye akasema, “nasi tumefikia mradi mmoja wa kupainia tukiwa jamaa.”

Linalohusiana karibu karibu na hili limekuwa ni ule utegemezo uliopewa makundi na mapainia shujaa, ambao walio wengi wao walikuja kutoka Uingereza. Baadhi yao hata walilowea Ailandi baada ya kupata jamaa zao wenyewe. Waume na wake wengi mapainia mwanzoni walikuja Ailandi wakiwa na wazo la kukaa mwaka mmoja au miwili na kisha warudi kwenye nchi ya kwao. Baadhi yao walifanya hivyo, nao walitoa mchango mzuri katika kusogeza mbele kazi hapa. Wengine, hata hivyo, waliweza kukaa katika Ailandi.

Kawaida ya mambo katika Ailandi ni mume na mke waliofunga ndoa kuwa na jamaa kubwa na kupata watoto upesi iwezekanavyo. Basi, watu Waairishi, mara nyingi walifikiri ni jambo lisilo la kawaida kuwaona waume na wake mapainia bila watoto. Wakati watu wa mahali walipogundua kwamba wale mapainia waliokuwa wakiwatembelea hawakuwa na watoto, hilo mara nyingi lilitokeza maneno haya ya kusihi “Nitawaashieni mshumaa!” Mara wale mume na mke mapainia waliokaa katika mtaa wa mahali walipopata watoto, walikubaliwa zaidi na watu wa mahali pale. Jambo hilo lilikuwa na tokeo la kuimarisha makundi. Badala ya kuhamisha mapainia katika migawo mbalimbali, kukaja kuwa na udumifu zaidi wa mambo.

Makundi yapatayo 30 kati ya yale 80 yana kiini kizuri cha wazee na wahubiri wengine kutokana na zile jamaa za mapainia ambao walilowea hapa. Katika kundi moja wanne kati ya wazee watano mwanzoni walikuja katika Ailandi wakiwa mapainia. Ni kwa sababu gani walikaa huko? Majibu yao ni: “Kumekuwa nyumbani kwetu.” “Sisi tulitaka kuendelea kutumikia mahali ambapo uhitaji ulikuwa mkubwa.” “Ilionekana hakuna haja ya kurudi mahali ambako hakukuwa na uhitaji mkubwa.” Yehova alibariki huduma yao. Kufikia 1982 kulikuwako Mashahidi 2,021 katika Ailandi.

Kazi ikiwa inafanikiwa katika Ailandi Kaskazini na ile Jamhuri ya Ailandi pia, ilitazamiwa kwamba mashetani wangekuwa na shughuli hata zaidi katika jitihada zao za kuzuia maendeleo. Silaha moja ambayo walitumia tena ilikuwa uasi-imani.

UASI-IMANI MARA NYINGINE TENA KATIKA DUBLIN

Katika 1982 namna ya uasi-imani yenye kudhuru sana ilisitawi, hasa katika eneo la Dublin. Baadhi ya akina ndugu walianza kuchukia mamlaka ya kundi na kutilia shaka fungu la mafundisho ambayo yanakubaliwa na watu wa Yehova kuwa ukweli. Wao waliendeleza lile wazo la kwamba kila Mkristo apaswa aweze kujiamulia mwenyewe mambo mbalimbali ya fundisho.

Polepole na kwa hila wao walipanda mbegu za mashaka katika akili za wengine kuhusu fundisho. Ukamilifu wa washiriki wa Baraza Linaloongoza ulitiliwa shaka. Wale wenye kuleta faraka waliokuwa wakitumikia kama wazee na watumishi wa huduma walidharau maagizo ya kitengenezo. Kutoka jukwaani, na katika nyakati nyingine kwa siri, walieneza mawazo yao wenyewe, wakidhoofisha uhakika wa wengine katika tengenezo la Yehova.

Kadiri mwelekeo huu wa uasi ulipodhihirika zaidi na zaidi, wale wazee washikamanifu katika makundi walijaribu kusaidia hao wapate tena usawaziko wao wa kiroho na imani na hivyo waepuke angamio la kiroho. (1 Tim. 1:19) Wale washikamanifu walijua hatari za hali kama hiyo, kama ilivyotabiriwa na wote wawili mtume Paulo na mtume Petro.—Mdo. 20:30; 2 Pet. 2:1, 3.

John Barr, kutoka lile Baraza Linaloongoza, na Robert Pevy, ambaye alikuwa amepainia katika Ailandi na ambaye sasa anatumikia kwenye Betheli ya Brooklyn, walitoa msaada. Walichukua wakati kutoka safari zao za likizo katika Uingereza kuja Ailandi kuongea na wale akina ndugu na kuwatia moyo. Walisababu kirefu pamoja na wale ndugu na kuzungumzia kikamili maswali mengi yaliyotokezwa juu ya mambo ya kimafundisho. Hata hivyo, ilionekana wazi, kwamba yale maswali yaliyotokezwa na wale wasiotosheka yalikuwa kisetiri tu cha moshi. Suala halisi lilikuwa kama hili, kwa kweli, lilikuwa tengenezo la Yehova au la.

Kadiri hili katao la ukweli lilivyokuwa wazi zaidi, wale wazee bado walijaribu kusaidia wale walioathiriwa na kufikiri kwa uasi-imani. Wakati ule ule, hata hivyo, wao pia waliona uhitaji wa kufuata shauri la mtume Paulo kwa Timotheo ‘kuwaamuru akina mwafulani wasifundishe fundisho tofauti.’ (1 Tim. 1:3, NW) Kama Paulo alivyomwonya Timotheo, mafundisho ya waasi-imani kama hao ‘huenea kama donda-ndugu.’ Mwishowe wale wazee hawakuwa na budi ila kuwaondosha watu wa namna hiyo kutoka katika kundi.—2 Tim. 2:17.

Kuondolewa kwa wale waliokataa tengenezo la Mungu kuliruhusu kazi isitawi. Katika 1982, wakati uasi-imani ulipoanza, kulikuwako wastani wa Mashahidi wa Yehova 2,021 katika Ailandi. Katika 1983 hiyo ilikua ikawa 2,124, katika 1984 ikawa 2,278, katika 1985 ikawa 2,403, na katika 1986 ikawa 2,472, kukiwa na kilele cha 2,661 katika Mei 1987. Mwendo huo wa kusonga mbele usiopungua waendelea. Ushikamanifu ulikuwa umetahiniwa kwa ukamilifu, lakini walio wengi zaidi walikuwa wameweka ushikamanifu wao kwa Yehova na tengenezo lake mbele ya ushikamanifu kwa mwanadamu ye yote. Wao walitambua ulipokuwa ukweli na ni kutokana na chanzo gani walikuwa wamejifunza huo, nao walishikamana kwa imara nacho. Wao waliendelea kujishughulisha na ile kazi muhimu ya kuhubiri na kufundisha.

“KITABU CHANGU CHA HADITHI ZA BIBLIA” KATIKA KIAIRISHI

Kwa miaka mingi watu wa Yehova walikuwa tu na trakti moja au mbili na kijitabu kimoja katika lugha ya Kiairishi. Basi, ilikuwa kwa msisimuko mkubwa kwamba, wakapokea Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia katika Kiairishi kwenye mkusanyiko wa wilaya wao katika 1982. Kiingereza ndiyo lugha inayotumiwa kwa ukawaida katika Ailandi. Kwa muda wa miaka michache iliyopita, hata hivyo, kumekuwako na kufufuliwa kwa kupendezwa katika lugha ya Kiairishi (lugha ya zamani zaidi ya Kiselti). Katika maeneo fulani ya nchi (maeneo ya Gaeltacht) ndiyo lugha pekee inayotumiwa. Sasa akina ndugu walikuwa na kitu fulani cha maana cha kutoa katika maeneo haya, hasa kwa watu waliokuwa wanapendezwa na lugha yao ya kienyeji.

Walimu wengi wa shule, kutia mapadri na wale walio katika upadri wa Kikatoliki wa kufundisha wa “Mabradha wa Kikristo” walikubali nakala za Mo Leabhar de Scéalta ón mBíobla, kama kilivyo katika Kiairishi. Ile njia ambayo katika hiyo kitabu hiki kilipokelewa inatoa kielezi cha mwelekeo wenye maendeleo wa wengi kuhusu Mashahidi wa Yehova. Padri mmoja mwenye kufundisha, akitilia hali chumvi kidogo alieleza hivi: “Kama tungalikubali vitabu kutoka kwenu miaka 30 iliyopita, tungalichomwa penye mti!”

Kwenye shule moja dada wawili walimkuta mkuu wa shule, ambaye alikuwa mtawa wa kike. Wakati Mashahidi hao walipomhubiri nje ya chumba cha walimu, yeye alichunguza kile kitabu kisha akasema kwa haraka, “Ngoja kidogo.” Dakika chache baadaye alitokea tena akiwa na pesa mkononi na kusema, “Nitachukua nakala tisa, tafadhali.” Kwenye shule nyingine, mwalimu aliyeangalia ununuzi wa vitabu kwa ajili ya shule alichunguza kitabu cha Hadithi za Biblia katika Kiairishi na akaagiza seti moja ya 35 kwa darasa.

Wengine licha ya wale walio katika kazi ya ualimu wanavutwa kwenye uelezaji ulio mwepesi ajabu wa maandishi ya Biblia katika kitabu hiki. Wengine ambao kwa kawaida hawangechukua vitabu kutoka kwa Mashahidi wamekubali nakala kadhaa.

Ndugu mmoja alitembelea mama mmoja ambaye alikuwa amemfanyia kazi ya kimwili. Alipotaja kuwa alikuwa na kitabu kipya katika Kiairishi, mwanamke huyo alisema “hakupendezwa hata kidogo na cho chote kinachohusiana na Mashahidi wa Yehova.” Hata hivyo, ndugu alimwonyesha kitabu kile. “Mimi sidhani kina ile imprimatur ndani yacho?” mwanamke yule akauliza. Yule ndugu alikubali kwamba kitabu kile hakikuwa na alama hii ya kibali cha Katoliki ya Roma, lakini yeye alimwonyesha yule mama jinsi kitabu kile kilivyokuwa na marejezo yote ya Maandiko yakionyeshwa mwishoni mwa kila hadithi. “Nao Mashahidi wa Yehova wanapata nini kutokana nacho?” mwanamke yule akauliza, bado akisita-sita kidogo. Yule ndugu alimweleza kwamba Mashahidi wa Yehova wanapendezwa tu katika kusaidia kila mmoja afahamu Biblia. Hiyo ndiyo sababu wao walikuwa wamechapa kitabu kama hiki. Mwanamke huyu alichukua nakala ya kitabu Hadithi za Biblia. Katika ziara iliyofuata mwanamke yule akauliza, “Je! kitabu hiki hakipiti kiasi kidogo katika kutumia-tumia jina Yehova?” Yeye alishangaa sana wakati yule ndugu alipomwonyesha kutoka kamusi ya watoto wake mwenyewe kwamba Yehova kwa kweli ni jina la Mungu na kwamba linaonekana zaidi ya mara 7,000 katika yale maandishi ya awali ya Biblia.

Dada mwingine alitembelea majirani wake wote akiwa na kitabu Hadithi za Biblia, katika lugha ya Kiingereza na ya Kiairishi pia. Watoto wake huenda shuleni pamoja na wengi wa watoto wa mtaa wake, naye aling’amua kwamba yeye hakuwa kamwe amesema kweli kweli na majirani wake juu ya ukweli. Yeye alisali kwa Yehova ampatie imara naye akaenda kutoa ushuhuda. Kwa sababu yeye alitambuliwa kuwa jirani yao, yeye alikaribishwa ndani ya nyumba nyingi na akawa na mazungumzo mazuri sana. Mwishowe yeye aliangusha vitabu Hadithi za Biblia 75!

MPANUKO NA UTENDAJI WENYE KUONGEZEKA WA UJENZI

Hesabu zenye kuongezeka za watu waliokuwa wakikubali ukweli zilifanyiza uhitaji mwingine katika Ailandi—ule uhitaji wa vifaa vikubwa zaidi vya tawi na mahali pa mikutano pazuri zaidi kwa ajili ya makundi.

Katika 1980 makao mapya ya tawi yaliwekwa wakfu katika Dublin. Kwa miaka mingi jengo la tawi lilikuwa limekuwa dogo sana. Fred Metcalfe anaeleza jinsi ukosefu wa nafasi ulivyofanyiza magumu fulani: “Nyakati nyingine ilikuwa sharti tutumie meza ya chumba cha kulia kwa kazi ya kupiga taipureta na kazi nyinginezo za afisi. Ilikuwa sharti twende chini kwenye mwisho wa bustani kupata vitabu kwa ajili ya makundi. Kile kibanda kilichokuwa kule kilikuwa ndicho mahali pekee pafaapo tulipokuwa napo pa kuweka vitabu.”

Baada ya miaka 12 ya kutafuta-tafuta, akina ndugu walipata na wakanunua kisehemu cha ardhi kifaacho, ambacho Mashahidi katika Ailandi walichangia fedha zilizo nyingi. Afisi ya tawi nzuri sana ilijengwa ambayo ilitoa vifaa vikubwa na vizuri zaidi kwa kushughulikia ukubwa uliokuwa ukiongezeka wa kazi kadiri Ailandi ilivyopata mpando katika kazi ya kukusanya. Lile Jumba la Ufalme ambalo lilishirikishwa katika ujenzi wa tawi si kwamba tu liliandaa mahali pa mkutano penye kuhitajiwa sana kwa makundi yaliyokuwa yakiongezeka bali pia liliamsha kupendezwa katika kujenga Majumba ya Ufalme mengine na likayawekea viwango vipya.

Ni makundi machache sana kufikia wakati huo yaliyokuwa na Majumba ya Ufalme yao wenyewe. Ama walikosa machumo yaliyohitajiwa kabisa kwa sababu wahubiri walikuwa wachache katika hesabu au lilithibitika kuwa jambo lisilowezekana kukodi makao yanayofaa kwa sababu ya chuki isiyo na sababu nzuri. Makundi fulani yalikutana katika vyumba vidogo juu ya ngazi nyingi za kupanda juu. Mahali pa mikutano palikuwa baridi na penye unyevunyevu, kukiwa na vifaa vichache vya kupasha joto. Kundi moja lilitumia jengo lililokuwa na mabati kwenye pande zalo. Watoto wa mahali hapo walizoea kujifurahisha sana kwa kutatarisha vijiti kwenye pande za jumba hilo wakati mikutano ilipokuwa ikiendelea.

Hesabu fulani ya makundi madogo yangali yanakutana katika vyumba vya kukodishwa juu ya mahoteli na mahali kwingineko, lakini hesabu yenye kuongezeka yameweza kujenga Majumba ya Ufalme. Hawa akina ndugu na dada wamefuata kwa furaha shauri hili: “Mheshimu Bwana [Yehova, NW] kwa mali yako.”—Mit. 3:9.

MAJUMBA YA UFALME YENYE KUJENGWA KWA HARAKA

Ujenzi wa Majumba ya Ufalme yenye kujengwa kwa haraka umesisimua akina ndugu katika Ailandi. Badala ya kazi ya ujenzi kuchukua miezi mingi, ikiwa si miaka, ya kazi ngumu ili kumaliza, Majumba ya Ufalme sasa yanajengwa katika muda ulio chini ya siku mbili! Jambo hili limeandalia makundi vifaa vya kukutania bila kuvuruga kazi ya kuhubiri Ufalme kwa vipindi virefu. Nao umekuwa ushuhuda mzuri ajabu mahali ambako majumba haya yamejengwa.

Jumba la kwanza lililojengwa kwa haraka lilikuwa katika Downpatrick katika Ailandi Kaskazini katika Juni 1985. Waliokuwa katika ile timu ya ujenzi yenye ujuzi walikuwa ndugu kutoka Uingereza waliosafiri kuja Ailandi Kaskazini kwa kulipia kabisa gharama zao wenyewe. Ndugu mafundi wa mahali pale walijiunga nao, licha ya wenye kujitolea wengine wenye nia. Wenye kujitolea zaidi ya 600 walihusika katika mradi huu.

Kwa sababu ya hesabu ndogo ya akina ndugu, wakati wazo hilo lilipotolewa swali lilikuwa, “Je! inawezekana katika Ailandi?” Kundi lilisonga mbele na mipango yalo likiwa na tumaini hakika katika utegemezo wa Yehova. “Sisi tulihisi kwamba tulikuwa tunachukuliwa na Yehova,” wakasema. Nayo imani yao ilithawabishwa wakati kundi hili dogo la wahubiri 19 tu lilipoona Jumba la Ufalme lao jipya likimalizika upesi mbele ya macho yao wenyewe.

Makundi mengine yakafuata. Upesi Ailandi ikawa na timu yayo yenyewe kwa ajili ya majumba yenye kujengwa kwa haraka. Hilo liliwezekanaje? “Lilifanikiwa,” akasema mwangalizi wa ujenzi, “kwa sababu ndugu na dada wote walikuwa wakivuta pamoja chini ya uvutano wa roho ya Yehova.”

Kundi moja lilijenga jumba lalo kwa muda ulio chini ya saa 36 ijapokuwa mvua yenye kunyesha sana. Kwenye mahali pengine mamia ya watu Wakatoliki wa mahali hapo walitembelea eneo la ujenzi baada ya kuhudhuria Misa Jumapili asubuhi. Wengi walivutiwa sana hivi kwamba walifanya mchango kwa ukarimu kusaidia gharama ya kulisha wafanya kazi wa ujenzi.

MATAZAMIO MAANGAVU YA MAVUNO

Lo! mambo yamebadilika kama nini kwa muda wa miaka 80 iliyopita! Ndugu mmoja alitaja kwamba miaka 20 iliyopita mapainia wa pekee katika kundi lake huenda wangaliweza kugawa magazeti kumi tu kwa muda wa mwezi mmoja hata ingawa walitumia saa 150 katika huduma. Hilo lilitoa nafasi ndogo kwa ziara za kurudia. Sasa kila mhubiri wa kundi anaweza, kwa wastani, kugawa magazeti 13 au 14 kila mwezi. Mwingi wa ule uchungu na chuki ya miaka iliyopita umetoweka.

Ni rahisi zaidi sana kushiriki katika huduma leo, kukiwa na uwezekano mdogo sana wa jeuri au mashambulizi ya watu wenye ghasia. Kungali kuna upinzani, lakini pia kuna nia kubwa zaidi ya kusikiliza ukweli. Katika muda wa mwaka uliopita mafunzo ya Biblia ya nyumbani 683 yaliongozwa, yakionyesha uwezekano mzuri sana wa maendeleo.

Kwenye umalizio wa safari yake katika 1891, Ndugu Russell alieleza hivi: “Uingereza, Ailandi, na Uskochi ni mashamba yaliyo tayari na yanayongojea kuvunwa.” Wengine huenda wakawa walifikiri, wakati mambo yalikuwa katika hali yayo mbaya sana, kwamba mavuno hayangekusanywa kamwe na kwamba nuru ya ukweli wa Biblia haingepenya kamwe lile giza la kiroho lililopofusha akili na mioyo ya watu katika Ailandi. Ilichukua muda mrefu zaidi kidogo kuliko ilivyotazamiwa mwanzoni, lakini hatimaye sisi tunaona yale mavuno yaliyotumainiwa kwa muda mrefu. Sasa kuna wahubiri 2,661 katika lile shamba, katika makundi 81.

Kazi nyingi inabaki kufanywa, lakini baraka ya Yehova ikiwa juu ya watumishi wake washikamanifu katika Ailandi, wengi zaidi wangali watakubali ukweli. Watu wote waaminifu wa Yehova katika Ailandi wanarudisha mwangwi wa kilio cha Yesu Kristo: Ndiyo, “mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache. Basi mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake.”—Mt. 9:37, 38.

[Ramani/Picha katika ukurasa wa 71]

(Ona mpangilio kamili katika nakala iliyochapishwa)

AILANDI

USKOCHI

BAHARI KUU ATLANTIKI

BELFAST

Londonderry

Downpatrick

Newry

Donegal

Crossmaglen

Drogheda

DUBLIN

Athlone

Galway

Roscrea

Limerick

Wexford

Waterford

Cork

Bahari Airishi

WALES

[Picha katika ukurasa wa 95]

Fred Metcalfe, mmoja wa mapainia wa pekee wa kwanza kupewa mgawo kwenye Jamhuri ya Ailandi

[Picha katika ukurasa wa 95]

Saba wa wale akina dada wamisionari wa kwanza kabisa waliokuja Ailandi katika 1949 ni, kushoto kwenda kulia: Mildred Willett (sasa Barr); Bessie Jones; Joan Retter (sasa Miller); Joey Orrom; Elsie Lott (sasa Levis); Ann Parkin (sasa Carter); Barbara Haywood (sasa Steffens)

[Picha katika ukurasa wa 98]

Olive na Arthur Matthews (picha ndogo), pamoja na ndugu ya Olive na mke wake, walitumia karavani hii ya urefu wa meta 4.3 wakati wa kampeni ya kile kijitabu “God’s Way Is Love” katika 1953

[Picha katika ukurasa wa 104]

Afisi ya tawi ya kwanza katika Ailandi, Barabara Lindsay 86, Dublin

[Picha katika ukurasa wa 130]

Jengo la sasa la tawi katika Finglas, Dublin, na washiriki wa Halmashauri ya Tawi, kushoto kwenda kulia: Peter Andrews, Arthur Matthews (mratibu wa Halmashauri ya Tawi), na Fred Metcalfe

[Picha katika ukurasa wa 135]

Juu: Jumba la Ufalme la kwanza lililojengwa kwa haraka katika Jamhuri ya Kiairishi, lilimalizwa Mei 1986 katika Dun Laoghaire

Katikati na chini: Jumba la Ufalme la kwanza lililojengwa kwa haraka katika Ailandi Kaskazini, lilimalizwa Juni 1985 katika Downpatrick

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki