Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yp2 sura 37 kur. 304-310
  • Nibatizwe?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Nibatizwe?
  • Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Badiliko Kubwa Maishani
  • Ubatizo​—Lengo Muhimu!
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Ubatizo​—Takwa kwa Wakristo
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Vijana Je, Mko Tayari Kubatizwa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
  • Uharibifu wa Sodoma na Gomora
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
Pata Habari Zaidi
Maswali Ambayo Vijana Huuliza—Majibu Yafanyayo Kazi, Buku la 2
yp2 sura 37 kur. 304-310

SURA YA 37

Nibatizwe?

Tia alama taarifa zifuatazo ikiwa ni kweli au si kweli:

Kila Mkristo anapaswa kubatizwa.

□ Kweli

□ Si kweli

Kusudi kuu la kubatizwa ni kukuzuia usitumbukie katika dhambi.

□ Kweli

□ Si kweli

Ubatizo ni hatua inayokuelekeza kwenye wokovu.

□ Kweli

□ Si kweli

Usipobatizwa, Mungu hatakuhukumu kwa matendo yako.

□ Kweli

□ Si kweli

Ikiwa rafiki zako wanabatizwa, basi wewe pia uko tayari kubatizwa.

□ Kweli

□ Si kweli

IKIWA unaishi kupatana na viwango vya Mungu, unakuza urafiki pamoja na Mungu, na kuzungumza na wengine kuhusu imani yako, ni kawaida kuanza kufikiria ubatizo. Lakini utajua jinsi gani kwamba uko tayari kuchukua hatua hiyo? Ili kujibu swali hilo, kwanza tuchunguze taarifa zilizo juu na kuona ikiwa ni kweli au si kweli.

● Kila Mkristo anapaswa kubatizwa.

Kweli. Yesu aliagiza wanafunzi wake wabatizwe. (Mathayo 28:19, 20) Hata Yesu mwenyewe alibatizwa. Ili kuwa mfuasi wa Yesu, unahitaji kubatizwa unapokuwa na umri wa kutosha kufanya uamuzi huo na kuwa na tamaa ya kutoka moyoni ya kufanya hivyo.

● Kusudi kuu la kubatizwa ni kukuzuia usitumbukie katika dhambi.

Si kweli. Ubatizo huonyesha waziwazi kwamba umejiweka wakfu kwa Yehova. Ubatizo wako si mkataba unaokuzuia kufanya mambo ambayo moyoni mwako ungependa kuyafanya. Badala yake, unaweka maisha yako wakfu kwa Yehova kwa sababu unataka kuishi kulingana na viwango vyake.

● Ubatizo ni hatua inayokuelekeza kwenye wokovu.

Kweli. Biblia inasema kwamba ubatizo ni muhimu ili kupata wokovu. (1 Petro 3:21) Hata hivyo, hilo halimaanishi kwamba ubatizo ni kama bima unayojikatia ili kujilinda usipatwe na madhara endapo msiba utatokea. Unabatizwa kwa sababu unampenda Yehova na unataka kumtumikia kwa moyo wako wote, milele.—Marko 12:29, 30.

● Usipobatizwa, Mungu hatakuhukumu kwa matendo yako.

Si kweli. Andiko la Yakobo 4:17 linasema hivi: “Ikiwa mtu anajua jinsi ya kufanya yaliyo sawa na bado hayafanyi, hiyo ni dhambi kwake”—iwe amebatizwa au sivyo. Kwa hiyo ikiwa unajua yaliyo sawa nawe una umri wa kutosha kuchunguza maisha yako kwa uzito, huenda huu ndio wakati wa kuzungumza jambo hilo na mzazi wako au Mkristo mwingine mkomavu. Kufanya hivyo kutakusaidia kujua jinsi unavyoweza kufanya maendeleo kufikia ubatizo.

● Ikiwa rafiki zako wanabatizwa, basi wewe pia uko tayari kubatizwa.

Si kweli. Uamuzi wa kubatizwa unapaswa kuwa wa hiari. (Zaburi 110:3) Unapaswa kubatizwa ikiwa tu unajua vizuri maana ya kuwa mmoja wa Mashahidi wa Yehova na una hakika kwamba uko tayari kubeba jukumu hilo.—Mhubiri 5:4, 5.

Badiliko Kubwa Maishani

Ubatizo ni badiliko kubwa maishani linaloleta baraka nyingi. Pia, ni jukumu zito—la kuishi kulingana na wakfu wako kwa Yehova.

Je, uko tayari kuchukua hatua hiyo? Ikiwa ndivyo, unapaswa kufurahi. Pendeleo kuu zaidi liko mbele yako—pendeleo la kumtumikia Yehova kwa moyo wote na kuishi maisha yanayoonyesha kwamba kwa kweli umejiweka wakfu kwake.—Mathayo 22:36, 37.

KATIKA SURA INAYOFUATA

Jifunze kuweka miradi ili utumie maisha yako kwa njia bora zaidi.

MAANDIKO MUHIMU

“Mtoe miili yenu iwe dhabihu iliyo hai, takatifu, yenye kukubalika kwa Mungu, utumishi mtakatifu pamoja na nguvu zenu za kufikiri.”—Waroma 12:1.

PENDEKEZO

Ukitegemea mwelekezo kutoka kwa wazazi wako, tafuta mtu katika kutaniko anayeweza kukusaidia kufanya maendeleo ya kiroho.—Matendo 16:1-3.

JE, WAJUA . . .?

Kubatizwa ni sehemu muhimu ya “alama” inayokutambulisha kwa ajili ya wokovu.—Ezekieli 9:4, 6.

HATUA ZA KUCHUKUA!

Ili kufanya maendeleo na kufikia ubatizo, nitajitahidi kuelewa vizuri zaidi mafundisho yafuatayo ya Biblia: ․․․․․

Mambo ambayo ningependa kuuliza mzazi (wazazi) wangu kuhusu habari hii ni ․․․․․

UNA MAONI GANI?

● Kwa nini ubatizo ni hatua nzito?

● Ni nini kinachoweza kumfanya kijana achukue hatua ya kubatizwa mapema sana?

● Ni mambo gani yanayoweza kumfanya kijana asitesite bure kujiweka wakfu na kubatizwa?

[Blabu katika ukurasa wa 306]

‘‘Kujua kwamba nimebatizwa kulinisaidia kufanya maamuzi kwa hekima na kutofanya mambo fulani ambayo yangeweza kuwa na matokeo mabaya.’’—Holly

[Sanduku/Picha katika ukurasa wa 307]

Maswali Ambayo Huulizwa Mara Nyingi Kuhusu Ubatizo

Ubatizo unawakilisha nini? Kuzamishwa na kuinuliwa humaanisha kwamba mtu ameacha maisha ya kufanya mapendezi yake mwenyewe, kana kwamba yule mtu wa zamani amekufa, na kuinuliwa akiwa hai, au mtu mpya ili kufanya mapenzi ya Mungu.

Kuweka maisha yako wakfu kwa Yehova kunamaanisha nini? Inamaanisha kujikana mwenyewe, na kuahidi kwamba utatanguliza mapenzi ya Mungu maishani. (Mathayo 16:24) Mtu anapaswa kujiweka wakfu rasmi kupitia sala kwa Yehova kabla ya kubatizwa.

Unapaswa kufanya nini kabla ya kubatizwa? Unapaswa kuwa ukiishi kulingana na Neno la Mungu na kuzungumza na wengine kuhusu imani yako. Unapaswa kujenga urafiki pamoja na Mungu kupitia sala na kujifunza Neno lake. Unapaswa kumtumikia Yehova kwa sababu wewe mwenyewe umeamua kufanya hivyo—lakini si kwa sababu wengine wanakulazimisha ufanye hivyo.

Mtu anapaswa kuwa na umri gani anapobatizwa? Umri si neno. Hata hivyo, unapaswa kuwa na umri wa kutosha, yaani, unapaswa kuwa na ukomavu wa kutosha kuelewa maana ya kujiweka wakfu.

Namna gani ikiwa unataka kubatizwa na wazazi wako wanasema ungoje? Huenda wangependa ujifunze zaidi kuishi maisha ya Kikristo. Usipuuze shauri lao. Tumia wakati huo kukuza urafiki wako na Yehova.—1 Samweli 2:26.

[Sanduku katika ukurasa wa 308, 309]

Ukurasa wa Mazoezi

Unafikiria Kubatizwa?

Kagua maendeleo yako kwa kufikiria maswali na taarifa zilizo hapa chini. Soma maandiko yaliyotajwa kabla ya kuandika majibu.

Unaonyesha jinsi gani kwamba unamtegemea Yehova?—Zaburi 71:5. ․․․․․

Umeonyesha jinsi gani kwamba nguvu zako za ufahamu zimezoezwa kutofautisha yaliyo sawa na yaliyo makosa?—Waebrania 5:14. ․․․․․

Wewe husali mara ngapi? ․․․․․

Wewe hutaja mambo hususa katika sala zako? Sala zako zinafunua nini kuhusu upendo wako kwa Yehova?—Zaburi 17:6. ․․․․․

Andika hapa chini miradi yoyote ambayo ungependa kujiwekea kuhusu sala. ․․․․․

Wewe hujifunza Biblia kibinafsi mara ngapi?—Yoshua 1:8. ․․․․․

Funzo lako la kibinafsi linatia ndani nini? ․․․․․

Andika hapa chini miradi ambayo ungependa kujiwekea kuhusu funzo la kibinafsi. ․․․․․

Wewe hupata matokeo katika huduma yako? (Kwa mfano, unaweza kuwaeleza wengine mafundisho ya msingi ya Biblia? Wewe huwarudia wanaopendezwa? Unajitahidi kuongoza funzo la Biblia?)

□ Ndiyo □ Hapana

Wewe huenda kuhubiri hata ikiwa wazazi wako hawaendi?—Matendo 5:42.

□ Ndiyo □ Hapana

Andika hapa chini miradi yoyote ungependa kujiwekea kuhusu huduma yako.—2 Timotheo 2:15. ․․․․․

Wewe huhudhuria mikutano ya Kikristo kwa ukawaida au mara mojamoja?—Waebrania 10:25. ․․․․․

Unapokuwa katika mikutano, unashiriki jinsi gani? ․․․․․

Wewe huhudhuria mikutano wakati ambapo wazazi wako hawawezi (ikiwa wanakuruhusu kwenda)?

□ Ndiyo □ Hapana

Unaweza kusema kwamba kwa kweli unapenda kufanya mapenzi ya Mungu?—Zaburi 40:8.

□ Ndiyo □ Hapana

Unaweza kutaja visa hususa ambavyo ulisimama imara na kushinda mkazo kutoka kwa vijana wenzako?—Waroma 12:2. ․․․․․

Unapanga kufanya nini ili upendo wako kwa Yehova usipoe?—Yuda 20, 21. ․․․․․

Utaendelea kumtumikia Yehova hata wazazi na rafiki zako wakiacha kumtumikia?—Mathayo 10:36, 37.

□ Ndiyo □ Hapana

[Picha katika ukurasa wa 310]

Kama ndoa, ubatizo ni badiliko kubwa maishani—si jambo linalopaswa kuchukuliwa vivi hivi

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki