Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w88 5/1 kur. 3-6
  • Jinsi ya Kuwa Mzazi Mwenye Mafanikio

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kuwa Mzazi Mwenye Mafanikio
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Mzazi Mwenye Mafanikio Ni Nini?
  • Kwa Sababu Gani Ni Jambo Gumu?
  • Ramani Zenye Mafanikio kwa Wazazi
  • Tendea Kila Mmoja kama Mtu Mwenye Utu wa Kipekee
  • Zoeza “Tangu Utoto Mchanga”
  • Zoeza Mtoto Wako Tangu Utoto Mchanga Sana
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Mzazi Mmoja, Matatizo Mengi
    Amkeni!—2002
  • Wazazi, Fikieni Moyo wa Mtoto Wenu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
  • Kulea Watoto tangu Uchanga
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1988
w88 5/1 kur. 3-6

Jinsi ya Kuwa Mzazi Mwenye Mafanikio

“MIMI nitakuambia yanayohusika katika kuwa mzazi mwenye mafanikio,” anasema Raymond, baba ya watoto watano. “Ni kujikaza kisabuni, kujitaabisha sana, kutoa machozi, na kumwaga jasho!”

Mke wa Raymond anakubaliana na jambo hilo kwa moyo mzima wote. Lakini yeye anaongezea hivi: “Si rahisi kulea watoto leo, lakini unapowaona wakikua wakawe watu wazima wenye kujali madaraka, ule mkazano unakuwa wenye kustahili.”

Kulea watoto hakujapata kamwe kuwa bila masumbuko. Hata hivyo, leo, kwa wazazi wengi inaonekana kama kwamba kulea watoto kumekuwa matata makubwa. “Mimi nafikiri kuwa mzazi leo ni jambo gumu kuliko lilivyokuwa wakati wa wazazi wangu kwa sababu maisha yamekuwa ya kutatanisha zaidi,” anasema Elaine, ambaye ana umri wa miaka 40 akiwa mama ya mwana mmoja tineja. “Si sikuzote unapojua ni wakati gani wa kufuatilia sana mambo na ni wakati gani wa kuyaachilia kidogo.”

Mzazi Mwenye Mafanikio Ni Nini?

Mzazi mwenye mafanikio ni yule anayelea mtoto wake kwa njia ambayo mtoto huyo anakuwa na kila fursa ya kukua akawe mtu mzima mwenye kujali madaraka, ambaye ataendelea kuabudu Mungu kiutendaji, na kuonyesha upendo kwa mwanadamu mwenzake. (Mathayo 22:37-39) Ingawa hivyo, inasikitisha kwamba si watoto wote wanaochukua zamu yao kuwa watu wazima wenye kujali madaraka. Kwa sababu gani sivyo? Je! sikuzote inapokuwa hivyo kasoro ni ya wazazi?

Fikiria kielezi kimoja. Mwanakandarasi wa ujenzi huenda akawa ana ramani na vifaa vya ujenzi vilivyo bora kabisa. Lakini tokeo lingekuwa nini ikiwa mwanakandarasi huyo angekataa kufuata ramani hizo, labda hata aruhusu upumbavu wa kutumia njia za mikato au kuruhusu vifaa duni vitumiwe badala ya vilivyo bora? Je! lile jengo lililokamilishwa halingekuwa na kasoro, hata liwe hatari kutumiwa? Ingawa hivyo, tuseme kwamba mwanakandarasi huyo alifanya mambo kwa kudhamiria na akatenda yote aliyoweza ili afuate ramani zile na kutumia vifaa bora. Je! sasa mwenye jengo lililokamilishwa hangekuwa na daraka la kulitunza kwa utaratibu unaofaa? Je! yeye hangekuwa pia na daraka la kutong’oa vile vifaa bora kwa kuvibadilisha na vilivyo duni?

Kwa njia ya kitamathali, wazazi wanahusika katika ujenzi unaofanana na huo. Wao wanataka kujenga ndani ya watoto wao nyutu nzuri sana. Biblia inaandaa ramani zilizo bora zaidi za kufanyia hilo. Vile vifaa bora, “dhahabu, fedha, mawe yenye thamani,” vinafananishwa katika Maandiko na sifa kama vile imani imara, hekima ya kimungu, utambuzi wa kiroho, ushikamanifu, na uthamini wenye upendo kwa Mungu mweza yote na sheria zake.​—1 Wakorintho 3:10-13; linganisha Zaburi 19:7-11; Mithali 2:1-6; 1 Petro 1:6, 7, NW.

Mtoto pia, anapoendelea kuwa na umri mkubwa, anachukua daraka zaidi na zaidi kujenga ndani yake mwenyewe utu wa kweli ulionyooka. Lazima yeye awe na nia ya kufuata ramani ile ile, Neno la Mungu, na kutumia vifaa bora vile vile ambavyo wazazi wake walitumia. Ikiwa mtoto anapokuwa kijana mtu mzima anakataa kufanya hivyo au anabomoa ujenzi huo ulio mzuri sana, basi yeye ndiye wa kulaumiwa kwa msiba unaotokea.​—Kumbukumbu 32:5.

Kwa Sababu Gani Ni Jambo Gumu?

Kuwa mzazi mwenye mafanikio leo ni jambo gumu kwa angalau sababu mbili. Kwanza, wote wazazi na watoto ni wasiokamilika na hufanya makosa. Mara nyingi, hiyo inahusisha ndani kile ambacho Biblia inakiita kutenda dhambi, na elekeo la kutenda dhambi ni la kurithiwa.—Warumi 5:12.

Sababu ya pili ni hii: Watoto wanaokua wanaongozwa na uvutano wa wengine pia, si wa wazazi wao tu. Mtaa mzima una athari fulani juu ya maadili na matazamio ya mtoto maishani. Kwa sababu hiyo, unabii wa Paulo juu ya siku yetu ni wa kuhangaikiwa na wazazi. Yeye alisema: “Lazima wewe ukubali kuelekeana na uhakika huu: muda wa hatimaye wa ulimwengu huu ni wa kuwa wakati wa mabalaa. Watu hawatapenda kitu ila pesa na wao wenyewe; wao watakuwa wenye kunyeta, wenye kujisifu, na wenye kutukana; bila staha kwa wazazi, bila shukrani, bila uchaji, bila shauku ya asili; wao watakuwa wasiotulizika chuki zao, wachuuzi wa vitendo vya kashifa, wasiozuia hasira yao na wakali, watu ambao ni wageni kwa wema wote, wahaini, wenye kujihatarisha wakijitafutia faida zao, waliofura kwa kujiona mashuhuri. Wao watakuwa watu wanaotia raha katika mahali pa Mungu, watu ambao wanahifadhi umbo la nje-nje la dini, lakini wanadumu wakiwa ukano wa uhalisi walo. Jiepushe kabisa na watu kama hawa.” (Italiki ni zetu.)—2 Timotheo 3:1-5, New English Bible.

Kwa kuwa jamii ya watu wa kisasa imefumwa kwa njia hizo zenye kasoro, je! ni ajabu kwamba wazazi fulani wanakata tamaa kwa kuvurugika akili na kukaribia kuacha kulea watoto? Tazama nyuma kwenye mwaka 1914. Mwaka huo wenye majanga uliona badiliko la msingi katika jamii ya watu, nalo halikuwa badiliko la kuleta nafuu. Vile vita vya ulimwengu viwili vya tangu wakati huo si kwamba vimekumba amani tu duniani. Jamii ya watu leo haina uthabiti ambao inauhitaji ili itimilize fungu layo la kutayarisha watoto kwa ajili ya utu mzima wenye kujali madaraka. Kwa kweli wazazi wenye mioyo ya kupenda uadilifu wanaelekeana na mazingira ya kijamii yaliyo na uhasama kwa maadili ambayo wao wanataka kufundisha watoto wao.

Hivyo, wazazi wana wasaidiaji wachache katika kikoa chao. Wakati uliopita, wao walitegemea shule za kiserikali zisaidie kufundisha watoto wao maadili yale yale ya msingi ambayo wao wakiwa wazazi walithamini katika maskani yao. Lakini mambo hayako hivyo tena.

“Leo mifinyo iliyo juu ya vijana ni tofauti; anasema Shirley, aliyehitimu kutoka shule ya sekondari katika 1960. “Sisi hatukuwa na dawa za kulevya wala ngono za hivi hivi tu wakati nilipokuwa katika shule ya sekondari. Kuponyoka ili mtu akavute kidogo sigareti kulionwa kuwa jambo baya miaka 30 iliyopita. Wakati binti yangu mwenye umri mkubwa zaidi alipohudhuria shule ya sekondari kuanzia 1977 mpaka 1981, utumizi wa dawa za kulevya ulikuwa tatizo kubwa. Sasa dawa za kulevya zimepenya ndani ya shule za msingi. Binti yangu mwenye umri mdogo zaidi, aliye na miaka 13, amelazimika kuelekeana na mfinyo huo wa dawa za kulevya kila siku shuleni kwa miaka miwili iliyopita.”

Pia, wakati uliopita, wazazi wangeweza kutegemea akina babu na nyanya, watu wa ukoo, na majirani wawasaidie kusimamia mwenendo wa mtoto. Lakini hapo tena, mambo yamebadilika. Na inasikitisha kuripoti kwamba, katika jamaa ambazo hesabu yazo inaongezeka, hamna hata kikoa cha ushirikiano wa watu wawili; mzigo mzima wa kulea watoto unaangukia mabega ya mzazi mmoja.

Ramani Zenye Mafanikio kwa Wazazi

Ingawa kulea watoto ni jambo gumu zaidi leo, wazazi wanaweza kufanikiwa wakijifaidi na msaada mmoja ambao mafaa yao yamethibitishwa kwa muda mrefu—Biblia. Neno la Mungu linaweza kuwa ramani au programu yako ya kuchukulia hatua za daraka la uzazi. Sawa na vile mwanakandarasi mwenye hekima anavyotumia vizuri ramani ya mwongozo wa ujenzi wa jengo mpaka lifikie ukamilisho wenye mafanikio, wewe unaweza kutumia Biblia kuwa mwongozo wako katika kulea watoto wako wawe watu wazima wenye kujali madaraka. Ni kweli, Biblia haikukusudiwa iwe kitabu tu cha mafunzo ya uzazi wenye mafanikio, lakini ina mashauri ya moja kwa moja kwa wazazi na watoto. Pia ni akiba kubwa yenye hazina ya kanuni ambazo zinapotumiwa zinaweza kukunufaisha wewe mzazi.​—Kumbukumbu 6:4-9.

Mathalani, fikiria Diane. Wakati Eric, mwanaye wa miaka 14, alipokuwa mchanga zaidi, alikuwa “mtoto wa kununa-nuna, mgumu kuongea naye,” anasema Diane. Hapo ndipo yeye alipogundua hekima inayotegemeza mithali hii ya Biblia: “Shauri [kusudi au mnuio] lililo katika moyo wa mtu ni kama mafungu ya maji yenye kina kirefu, lakini mtu wa utambuzi ndiye ataliteka.” (Mithali 20:5, NW) Kwa watoto fulani, hisia na fikira zao—minuio yao halisi—zimo katika moyo wao kama mafungu ya maji kwenye sehemu ya chini ya kisima cha kina kirefu. Eric alikuwa hivyo. Inahitaji kazi ngumu kwa upande wa mzazi ili kuteka minuio hiyo. “Yeye alipokuwa akija nyumbani kutoka shuleni, hakuwa akibubujika mambo ya kusimulia,” Diane anakumbuka. “Kwa hiyo mimi nilitumia wakati kuuliza-uliza nipate kujua aliyokuwa akielekeana nayo shuleni. Nyakati nyingine nilikuwa nikiongea na Eric muda wa saa nyingi kabla hajanifunulia alilokuwa akifikiria hasa katika kina cha moyo wake.”

Sababu ya Biblia kuwa mwongozo wenye thamani kubwa ni rahisi: Yehova Mungu ndiye Mtungaji wayo. Yeye pia ndiye Muumba wetu. (Ufunuo 4:11) Yeye anajua asili yetu na ana nia ya ‘kutufundisha kujinufaisha wenyewe na kusababisha tukanyage katika ile njia ambamo sisi tunapaswa kutembea.’ Hiyo ni kweli hata kama mtu ni mzazi au ni mtoto. (Isaya 48:17; Zaburi 103:14) Ingawa watu fulani wanalazimika kujitahidi zaidi ya wengine ili wawe mzazi bora, wote wanaweza kuwa bora katika kutunza daraka la uzazi kwa kufuata miongozo iliyoorodheshwa katika Maandiko.

Tendea Kila Mmoja kama Mtu Mwenye Utu wa Kipekee

Watoto wema hawawezi kutokezwa kwa kufuata sheria fulani za kibinadamu zenye kushikiliwa king’ang’a, sawa na vile kila mtu mzima haundwi akiwa mzazi “mkamilifu.” Kila mtoto ana utu wake mwenyewe, na lazima kila mtoto ashughulikiwe kama mtu mwenye utu wa kipekee. Biblia inatambua jambo hilo. Ili kusaidia wazazi waepuke kulinganisha isivyofaa mtoto mmoja na mwingine, kanuni inayotegemeza shauri la Biblia lifuatalo inafaa: “Lakini acheni kila mmoja athibitishe kazi yake mwenyewe ni nini, na ndipo yeye atakuwa na kisababishi cha mchachawo kuhusu yeye mwenyewe peke yake, na si katika mlinganisho pamoja na mtu yule mwingine.”​—Wagalatia 5:26; 6:4, NW.

John, baba ya watoto wawili, anapata kwamba mashauri ya Kimaandiko yaliyo juu yanamsaidia kuendeleza usawaziko wa maoni ya watoto wake juu ya mmoja na mwenzake, au hata juu ya jamaa nyinginezo. “Mimi nawatia moyo watoto wangu wasitazame vitu ambavyo jamaa nyinginezo zinavyo au mambo zinayoyafanya,” John anaeleza. “Sisi tuna kiwango chetu wenyewe cha kijamaa kinachopasa kudumishwa.”

Zoeza “Tangu Utoto Mchanga”

Ni wakati gani dini inapopasa kuwa sehemu ya daraka la uzazi lenye mafanikio? “Huwezi kuanza mapema mno,” anasema Gary, ambaye ndiyo sasa tu mwanaye ameanza kwenda shule ya watoto wadogo. Gary anaitikadi kwamba ni lazima watoto wawe na marafiki wa kweli kweli katika kundi la Kikristo la kwao hata kabla hawajaanza kuhudhuria shule. Hiyo ni sababu moja ambayo Gary na mke wake wamekuwa wakileta Evan kwenye mikutano ya Kikristo yapata tangu siku ile aliyozaliwa. Gary anaiga yale ambayo Eunike, mzazi ambaye anapongezwa katika Biblia, alifanya kuhusu Timotheo mwanaye. Timotheo alijifunza nukta za kwanza-kwanza za mafundisho ya Kimaandiko “tangu utoto mchanga.”​—2 Timotheo 1:5; 3:15, NW.

Mama ya Timotheo na labda nyaya yake, Loisi, walihakikisha kwamba si mawazo yao kibinafsi yaliyomvutia yeye tangu utoto mchanga; bali, wao walijua mafundisho ya Yehova ndiyo yangemhekimisha kwa ajili ya wokovu. Barua aliyoandikiwa Timotheo na mtume Mkristo Paulo inataarifu hivi: “Hata hivyo wewe endelea katika mambo ambayo wewe umejifunza na uliombwa sana uyaitikadi, ukijua ni kutoka kwa watu gani wewe ulijifunza hayo na kwamba tangu utoto mchanga wewe umejua maandiko matakatifu, ambayo yanaweza kukufanya wewe uwe mwenye hekima kwa ajili ya wokovu kupitia ile imani kwa ukamatano pamoja na Kristo Yesu.”​—2 Timotheo 3:14, 15, NW.

Kwa hiyo Loisi na Eunike walisaidia Timotheo asababu mambo kuhusu lile Neno na kutegemeza imani yake juu ya mambo yenye kusemwa na Neno la Mungu lililoandikwa. Kwa njia hiyo msingi wa imani yake haukuwa katika wazazi wake tu bali katika hekima ya kimungu ya Neno la Yehova. Yeye hakufuata ukweli wa Kikristo kwa sababu tu mama na nyanya yake walikuwa waabudu wa Yehova bali yeye alijisadikisha mwenyewe kwamba kwa uhakika mambo aliyofundishwa nao yalikuwa ndiyo ukweli.

Bila shaka, Timotheo alifikiria pia mama na nyanya yake walikuwa watu wa namna gani—watu wa kiroho kweli kweli. Wao hawangemlaghai wala kupotosha ukweli ili watimize makusudi ya ubinafsi; wala wao hawakuwa wanafiki. Basi, Timotheo hakuwa na shaka juu ya mambo aliyojifunza. Na hakuna shaka kwamba maisha yake ya utu mzima akiwa Mkristo mtendaji yalichangamsha moyo wa mama yake mwaminifu.

Ndiyo, kutimiza daraka la uzazi wenye mafanikio ni kazi ngumu, lakini kama vile yule mama aliyetangulia kunukuliwa alivyosema “Ule mkazano unakuwa wenye kustahili.” Hiyo ni kweli hasa wakati wazazi wanapoweza kusema juu ya watoto wao yale ambayo mtume Yohana aliandikia watoto wake wa kiroho “Hakuna kisababishi kikubwa zaidi cha utoaji shukrani ambacho mimi ninacho kuliko mambo haya, kwamba mimi niwe nikisikia kwamba watoto wangu wanaendelea kutembea katika ule ukweli.”​—3 Yohana 4, NW.

[Sanduku katika ukurasa wa 6]

Programu ya Kielimu lliyofuatwa na Wazazi Katika Israeli

Katika Israeli ya kale, wazazi ndio waliokuwa na daraka la kuelimisha na kuzoeza watoto wao. Wao wakawa ndio wafundisha-maagizo na waongozi wa watoto wao. Utimizaji wa ki-siku-hizi wa daraka la uzazi unaweza kunufaisha kwa kufuata programu inayofanana na hiyo. Programu ya kielimu katika Israeli inaweza kujumlishwa kimuhtasari kama ifuatavyo:

1. Hofu kwa Yehova ilifundishwa.​—Zaburi 34:11.

2. Onyo la upole lilitolewa juu ya kuheshimu baba na mama.​—Kutoka 20:12.

3. Maagizo katika ile Sheria, na pia katika utendaji mbalimbali wa Yehova, yalikazwa kikiki.​—Kumbukumbu 6:7-21.

4. Staha kwa watu wazee-wazee ilikaziwa. —Walawi 19:32.

5. Utii ulitiliwa shada.​—Mithali 23:22-25.

6. Mazoezi yenye mafaa kuhusu maisha yaliingizwa ndani kwa uthabiti.​—Marko 6:3.

7. Elimu katika kusoma na kuandika ilitolewa.​—Yohana 7:15.

[Picha katika ukurasa wa 5]

Neno la Mungu ni ramani ya ujenzi, au programu ya kufanyia mambo, kwa ajili ya kutimiza daraka la uzazi

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki