Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/90 kur. 1-2
  • Jenga Imani Katika Neno la Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jenga Imani Katika Neno la Mungu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • KWA NINI KUSAIDIA WENGINE WAJENGE IMANI
  • KITABU KIPYA HICHO KINAJENGA IMANI
  • “Tupe Imani Zaidi”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Je, Kweli Una Imani Katika Habari Njema?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2003
  • Imarisha Imani Yako Katika Muumba
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Onyesha Imani Yako Katika Ahadi za Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2016
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 3/90 kur. 1-2

Jenga Imani Katika Neno la Mungu

1 Ikiwa kuna wakati ambao imani yenye nguvu imehitajiwa, ni sasa. Watu wengi hawana imani kamwe wala tumaini kwa ajili ya wakati ujao. Viongozi wa kidini na kisiasa wametokeza matumaini bandia mara nyingi sana hata kwamba watu wengi wanatamauka kiwaziwazi. Ni kweli, kama mtume Paulo alivyoeleza, “Si wote walio na imani.” (2 The. 3:2) Hata hivyo, Mashahidi wa Yehova wana imani. Tuna uhakika kamili kwamba ahadi zinazopatikana katika Neno la Mungu zitatimizwa.

2 Imani yenye nguvu hufanya Mashahidi wa Yehova wawe tofauti na watu wale wengine. Inachochea kazi njema zinazonufaisha wale wengine na pia sisi wenyewe, huku zikimletea Mungu heshima. Imani hiyo inatokana na kuruhusu Neno la Mungu liwe na nguvu maishani mwetu. Udugu wa kimataifa wa ki-siku-hizi wa Wakristo wa kweli hudhihirisha thamani ya kujenga imani katika Biblia kuwa Neno la Mungu lililovuviwa.—2 Tim. 3:16.

KWA NINI KUSAIDIA WENGINE WAJENGE IMANI

3 Kwa kuwa maisha zimo hatarini, tuna sababu yenye nguvu ya kusaidia wengine wajenge imani yao. Tukiwa tunafikiria hilo, wakati wa Machi tutatoa The Bible—God’s Word or Man’s? kwa mara ya kwanza shambani. Kusudi la kitabu hicho kipya ni kusaidia watu waone kwamba Biblia ni Neno la Mungu. Kinazungumzia na kukanusha mengi ya mashtaka bandia yanayoelekezewa Neno la Mungu. Kinatoa majibu yenye kuridhisha kwa maswali kadhaa, kama vile: Je! Biblia si ya kisayansi? Je! inajipinga yenyewe? Je! ni hadithi ya kutungwa au ya kimapokezi tu? Je! miujiza inayotajwa katika Biblia ilitokea kweli kweli? Je! akiolojia imethibitisha historia ya Biblia si sahihi? Kuongezea hayo, kichapo hiki kinatoa uthibitisho mwingi mzuri wa uvuvio wa Biblia. Pia kinavuta fikira kwenye unabii usiokosea wa Biblia na upatani wayo wa ujumla ulio mzuri ajabu.

4 Hekima inayotumika sana ya Biblia na nguvu zayo za kubadili watu kuwa wema ni sehemu tu ya ushuhuda unaothibitisha kwamba Biblia ni Neno la Mungu. Sisi tuna daraka la kuwasaidia watu wajifunze juu ya ushuhuda huo. Ili kufanya hivyo, ni lazima kwanza tuwafundishe kuamini yale ambayo Biblia inasema.

5 Wengi wetu tulisaidiwaje tujenge imani katika Neno la Mungu? Yaelekea sana ilikuwa kupitia funzo la Biblia la nyumbani ambalo mtu fulani alituongoza kwa subira. Kwa hiyo kuangusha Biblia au kitabu si ndiyo mwisho wa jitihada za kujenga imani; ni mwanzo tu. Kama tumenufaika kwa mtu mwingine kujifunza nasi, sisi tutataka kurudi mara moja kwa wale ambao tunaangushia fasihi na kuwatolea funzo la Biblia la nyumba ili kuwasaidia wajenge imani.

KITABU KIPYA HICHO KINAJENGA IMANI

6 Anapochanganua kwa unyoofu ushuhuda, hakuna mtu yeyote mwenye moyo mweupe anayeweza kushindwa kukubali kwamba Biblia ni Neno la Mungu. Kitabu hiki kipya kinatoa mwingi wa ushuhuda huo katika njia rahisi yenye kukubalika. Tunataka kuwatia moyo wengine wakubali Biblia kuwa Neno la Mungu na kuishi kulingana na shauri layo lililovuviwa. Wale wafanyao hivyo watakuja kurudia kwa shangwe sala ya hisia-moyo ya mtunga zaburi: “Uangalie niyapendavyo mausia yako, Ee BWANA [Yehova], unihuishe sawasawa na fadhili zako. Jumla ya neno lako ni kweli, Na kila hukumu ya haki yako ni ya milele.”—Zab. 119:159, 160.

7 Kupitia Neno lake, Biblia, Yehova huandaa kwa upendo mwelekezo kwa ajili ya wote wanaotafuta njia yake ya ulinzi ili kuokoka “dhiki kubwa.” (Mt. 24:21) Wakati wa Machi, tunaweza kuwatia moyo wengine wasome na kujifunza Neno la Mungu kwa kutoa kitabu The Bible—God’s Word or Man’s?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki