Wimbo 19
Wenye Furaha Mchana Kutwa
1. Furahi! Terema!
Sisi tuna Yehova.
Furahi, daima,
katika kazi yake.
Tumetoshelezwa. Tunaye Mungu.
Tunahitaji nini kingine?
Tunayo amani
Tumeridhika sana.
Bila uhitaji;
Karibia Yehova.
Shangilia sana, usigeuke,
Tunavuna kwa furaha nyingi.
2. Tumewekwa huru
kwa kujua ukweli.
Tunasikiliza
sauti yake Yesu.
Na kwa damu yake tukawa huru
Na tukachaguliwa na Mungu.
Sasa Ufalume
Wake unatawala.
“Mutumwa” wa Yesu
anatutunza sisi.
Tuna maarifa; na tumaini.
Tufariji wanadamu nayo.
3. Ni furaha kubwa
kuhubiria watu.
Kwetu ni furaha
kuwakuta kondoo.
Penda ndugu zako, Wakaribishe,
Tuna amani akili moja.
Daima furahi
Julisha Ufalume
Tazama uone
mukutano mukubwa!
Yehova tulishe utuongoze.
Sifa ni kwako wewe Yehova.