Kutangaza Habari Njema—Kwa Magazeti
1 Hakuna majarida mengine katika historia ambayo yamepata kuwa na uvutano kwa ajili ya mema kadiri hiyo katika maisha za watu kama Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Kila toleo linajaa chakula cha kiroho chenye kutoa uhai. Matokeo ya utafiti wa kina kirefu ukitolewa pamoja na utegemezo imara wa Kimaandiko hukazia katika akili na mioyo yetu ujumbe wa ukweli.
2 Mnara wa Mlinzi, kupitia kurasa zalo hufafanua mafundisho ya Biblia na kuvuta uangalifu wetu kwenye utimizo wa unabii mbalimbali wa Biblia. Huwatia moyo wote wenye njaa ya kiroho wageuze akili zao na kuvaa utu mpya. (Rum. 12:2; Efe. 4:22-24) Amkeni! huwaweka chonjo wasomaji walo waone matukio yenye umaana katika ulimwengu. vielezi vyalo vyenye kuvutia vikionyesha maajabu ya uumbaji huchochea upendezi katika ulimwengu mpya na huupa kina uthamini kwa Muumba mwenye upendo.
SI KAMA MAGAZETI YA KILIMWENGU
3 Magazeti ya kilimwengu hayaonyeshi watu jinsi ya kuonea shangwe maisha yenye uradhi katika ulimwengu huu. Hayatoi tumaini lolote kwa wakati ujao na yanashindwa kufundisha watu jinsi ya kupata uhai wa milele. Magazeti hayo ya kilimwengu yanakusudiwa kuendeleza vitu vya ulimwengu huu. Yanatofautiana kama nini na Mnara wa Mlinzi na Amkeni!—1 Yn. 2:15-17.
4 Bila shaka wewe unahisi shukrani yenye kina kwa ajili ya kila toleo la Mnara wa Mlinzi na Amkeni!—magazeti yenye harufu tamu ya ukweli kutoka kwa “wakili mwaminifu.” (Lk. 12:42) Tunaweza kufanya nini tufanyie maendeleo maangusho yetu ya magazeti na hivyo kusaidia wengi zaidi wanufaishwe na majarida yetu?
KUFANYA SEHEMU YETU
5 Kabla ya kuweza kuwatia moyo watu wenye mioyo yenye ufuataji haki wayasome magazeti yetu, tunahitaji kujua yaliyomo katika kila jarida. Hilo latutaka tusome kila toleo kabla ya kulitumia katika huduma. Tukifahamiana kikamili na yaliyomo, tunaweza kutumia njia za huduma ya nyumba kwa nyumba, na kutoa ushahidi vivi hivi kwa ajili ya kugawanya magazeti.
6 Zaidi ya hilo, kwa kuwa na magazeti yetu tunaponunua vitu madukani, tunaposafiri na usafiri wa umma, shuleni, kwenye mahali petu pa kazi ya kuajiriwa, au popote tuendapo, tutaweza kutwaa fursa zenye kufaa kutoa ushahidi. Utangulizi uliochaguliwa vizuri kutoka kitabu Kutoa Sababu na kuunganisha pamoja na jambo moja kutoka makala mojapo huenda ikaamsha tamaa ya mtu huyo asome magazeti yetu.
7 Ijapokuwa huenda mazungumzo yetu yakawa mafupi wakati wa kutoa magazeti, si lazima kuwekea mazungumzo yetu mpaka wa dakika moja tu. Tunataka kuchukua wakati tuamue kama mtu huyo anapendezwa kikweli katika ujumbe na kama atasoma gazeti hilo. Maswali yakitokea, twapaswa sikuzote kujaribu kujibu maswali hayo kwa kutumia Biblia zetu au kitabu Kutoa Sababu. Kwa kuwa tayari kutetea imani yetu, twaweza kuvuna baraka nzuri ajabu.—1 Pet. 3:15.
8 Mtu huyo akikubali kusoma magazeti, tunaweza kunena juu ya namna ya kazi yetu na jinsi magazeti hayo hutangazwa mara mbili kwa mwezi yakiwa sehemu ya kazi ya elimu ya Biblia ya ulimwenguni pote. Habari iliyo katika ukurasa wa 2 wa Mnara wa Mlinzi au ukurasa wa 4 wa Amkeni! huelezea jambo hilo vizuri sana. Kwa kuwa yatakayokuwamo katika matoleo ya wakati ujao huorodheshwa sikuzote, tunaweza kufafanua maswali yanayohusiana au tuvute uangalifu kwenye makala zijazo. Hilo laweza kuchochea hamu ya mtu huyo na kumsukuma aonyeshe tamaa ya kupata toleo hilo linapotokea. Huo waweza kuwa mwanzo wa kuwa tukimpelekea mtu huyo magazeti kwa ukawaida.
9 Mwisho wa mfumo huu ukaribiapo, na tuharakishe mwendo wetu kusaidia watu wenye mioyo ya ufuataji haki wamkimbie Babuloni Mkubwa na kuingia katika ukweli. (Ufu. 18:4) Mnara wa Mlinzi na Amkeni! hutimiza sehemu yenye nguvu nyingi katika kazi yetu ya elimu ya Biblia ya ulimwenguni pote. Tu wenye shukrani kwamba Yehova ameyaandaa tuyatumie katika huduma. Yehova na aendelee kubariki utumizi wetu wa uangalifu na yenye bidii wa majarida haya!