Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/90 uku. 8
  • Kutoa Habari Njema—Wakati wa Sikukuu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kutoa Habari Njema—Wakati wa Sikukuu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1990
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UWE MWENYE KUFIKIRIA NA KUSTAHI
  • MATANGULIZI
  • Kutangaza Habari Njema-Wakati wa Sikukuu
    Huduma Yetu ya Ufalme—1989
  • Chukua Msimamo Upande wa Ibada ya Kweli
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Watu Hufikiria Nini Hasa Wakati wa Krismasi?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2005
  • Amua Kumwabudu Mungu
    Biblia Inatufundisha Nini?
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1990
km 12/90 uku. 8

Kutoa Habari Njema—Wakati wa Sikukuu

1 Ijapokuwa sherehe nyingi zinazoshirikishwa na Krismasi na Mwaka Mpya zina asili za kipagani, wanaodai kuwa Wakristo zaidi ya bilioni moja huadhimisha sikukuu hizo kila mwaka. Watu wengi huamini kwa moyo mweupe kwamba sherehe hizo wanazoadhimisha hukubaliwa na Mungu. Sisi twaweza kufikiaje mioyo ya watu kama hao kwa habari njema katika pindi ya wakati wa sikukuu hizo?

UWE MWENYE KUFIKIRIA NA KUSTAHI

2 Ikitegemea hali za kwenu huenda wazee wakafanya mipango ya pekee kwa ajili ya kutoa ushahidi wakati wa sikukuu, kwa kuwa wengi wetu huwa na wakati wa likizo kutoka kazi ya kimwili. Wakati wa kuanza kazi ya nyumba kwa nyumba huenda ikahitaji kurekebishwa kwa kufikiria wale wenye nyumba ambao huenda wakawa wamechelewa kuamka katika siku hizo.

3 Tuendeleapo na huduma yetu, yaelekea tutakuta hesabu fulani ya watu wakiwa na shughuli nyingi wakiwa na wageni na kutayarisha milo. Kwa kutambua kwamba ni wakati wa pekee kwao, twaweza kwa staha kufanya maelezo yetu yawe mafupi na yenye kutaja mambo waziwazi. Adabu nzuri ya Kikristo kwa upande wetu huenda ikafungua njia kwa ajili ya ushahidi zaidi wakati ujao.

4 Sisi hatushiriki sherehe hizo za kidini za kilimwengu, na hatubadilishani salamu za sikukuu za kimapokeo. Kwa hiyo, busara yahitajiwa kuhusu jinsi ya kuitikia salamu hizo. Hakuna haja ya kufanya salamu hizo kuwa kibishanio, bali katika visa vingi twaweza kumshukuru tu mwenye nyumba kwa kututakia mema. watu wakiuliza juu ya imani yetu, twaweza kuwahakikishia kwamba sisi twamheshimu Kristo Yesu, kwa kuwa jambo hilo linatakwa kwa wale wanaomheshimu Mungu. (Yn. 5:23) Hata hivyo, desturi nyingi za sikukuu haziheshimu ama Kristo au Mungu. Watu mmoja mmoja wakitamani habari zaidi wakati huo au baadaye, twaweza kushiriki nao habari iliyo katika kitabu Kutoa Sababu katika kurasa 290-2 na 294.

MATANGULIZI

5 Kwa kuwa sikukuu za Krismasi zina asili ya kidini, huenda tukakuta watu wengi ambao wanaelekea zaidi kuongea juu ya Mungu wakati huo kuliko wakati mwingine wowote wa mwaka. Sisi twaweza kujifaidi na uhakika huo katika utangulizi wetu. Kwa kielelezo, twaweza kusema: “Mamilioni ya watu kotekote duniani wanasherehekea Krismasi na Siku ya Mwaka Mpya. Je, wewe unafikiri kwamba sherehe hizo zinaleta watu karibu zaidi na Mungu?” Iwe mwenye nyumba ahisi kwamba sherehe hizo ni nzuri au mbaya, baada ya kukubali maelezo yake, tungeweza kusema: “Watu wengi hutamani laiti wangekuwa na uhusiano mzuri zaidi na Mungu, labda wakihisi kwamba Mungu yuko mbali nao. Kwa furaha, Mungu mwenyewe hutualika tumtafute.” Kisha uendelee na Kichwa cha Mazungumzo.

6 Kwa kutumia njia nyingine, tungeweza kusema: “Katika pindi hii ya wakati wa Krismasi, mara nyingi twasikia watu wakionyesha tumaini kwamba kutakuwa na amani duniani na nia njema kuelekea watu. Je, wewe unafikiri Mungu ataleta amani duniani katika wakati wetu?” Baada ya hapo twaweza kuendelea kuonyesha kwamba Yesu Kristo ndiye “Mwana-Mfalme wa Amani” aliyetabiriwa. (Isa. 9:6, 7, NW) Akiwa Mtawala aliyewekwa katika serikali ya Mungu, Kristo atachukua hatua karibuni alete amani ya kudumu duniani.—Dan. 2:44; Ufu. 21:3-5.

7 Ingawa watu wengi ni wenye ubaridi kuelekea ujumbe wa Ufalme na wanapendezwa na sikukuu zao za kidini zilizo bandia, bila shaka Yehova atabariki jitihada zetu za kuwapata watafutaji wa kweli, kwa kuwa yeye mwenyewe “awatafuta watu kama hao wamwabudu,” naye atawaelekeza kwenye tengenezo lake.—Yn. 4:23, 24.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki