Wimbo 76
Yehova, Rafiki Yetu Bora Zaidi
1. Yehova Mungu, Yeye ni
Rafiki wa kweli.
Katufanyia dunia,
Katoa uzima.
Ingawa wazazi wetu
Walimwasi yeye,
Anao urafiki na
Wa’minifu wake.
2. Abrahamu mwaminifu,
Rafiki ya Mungu.
Mungu alimujaribu,
Akaaminika.
Akahesabu Yehova
’Ngefufua mwana.
Yehova alimupenda
Abrahamu sana.
3. Mwishowe Mwana wa Mungu
Kaja duniani.
Katoa uhai wake
Turudi kwa Mungu.
Shetani ajapotaka
Kumukengeua,
Kristo alishikamana
Naye Mungu juu.
4. Rafiki walio bora
Ni Yah na Mwanaye.
Wameonyesha upendo
Tupate uzima.
Rafiki za ulimwengu
Adui za Mungu.
Tuwe marafiki wake,
Washikamanifu.