Wimbo 148
Kumtukuza Mungu Wetu Mfalme
1. E mwimbieni Yehova!
Na kusifu kutwa kutwa.
Tutangaze jina lake
Tukaribie zaidi,
Atufungulia ’kono,
Tayari kusaidia.
Tushikamane na yeye;
Yehova Mungu ni mwema.
2. Tuwe washikamanifu
Na wa kweli tubariki.
Maana ni mwadilifu;
Tusifu ukuu wake.
Alinda walio wake;
Kusiwe magumu kamwe.
Atuondolea shida.
Tunabariki Yehova.
3. Ufalme uko karibu
Ulete mambo mazuri
Tangaza Ufalme wake,
Nyote “muliotosheka.”
Yehova ameinua
Mufalme asiyepingwa.
Waovu wataondoshwa.
Enzi ya Mungu thabiti.