Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/91 kur. 1-2
  • Siku Iliyo ya Maana Kupita Zote Katika 1991

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Siku Iliyo ya Maana Kupita Zote Katika 1991
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1991
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • UKUMBUSHO—UMAANA WAKE
  • JINSI TUNAVYOWEZA KUONYESHA UTHAMINI
  • Ukumbusho (Mlo wa Jioni wa Bwana)
    Kutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
  • Ukumbusho—Tukio la Umaana Mkubwa!
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Kuadhimisha Kifo Kitoacho Tumaini la Uhai wa Milele
    Huduma Yetu ya Ufalme—1993
  • Ukumbusho—Sherehe ya Kikristo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1990
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1991
km 3/91 kur. 1-2

Siku Iliyo ya Maana Kupita Zote Katika 1991

1 Siku iliyo ya maana kupita zote katika kalenda yetu mwaka huu ni Jumamosi, Machi 30. Baada ya jua kushuka katika siku hiyo, sisi tutaadhimisha Ukumbusho wa kifo cha Yesu. (1 Kor. 11:20, 24) Kwa nini tarehe ya kifo cha Yesu ikafanywa kuwa siku ya ukumbusho wa pekee?

UKUMBUSHO—UMAANA WAKE

2 Kifo cha Yesu kilikuwa tukio la umaana wa ulimwengu wote mzima. Wakati alipokuwa akiandikia washiriki wa kundi la Kikristo waliozaliwa kwa roho, mtume Paulo alisema hivi: “Kila mwulapo mkate huu na kukinywea kikombe hiki, mwaitangaza mauti ya Bwana hata ajapo.” (1 Kor. 11:26) Kwa hiyo Ukumbusho huelekeza fikira za pekee kwenye umaana wa kifo cha Yesu Kristo katika kutimizwa kwa kusudi la Yehova. Unakazia maana ya kifo cha dhabihu cha Yesu, hasa kuhusiana na lile agano jipya na kwa njia ambayo kifo chake huathiri wale watakaokuwa warithi washirika katika Ufalme wa kimbingu.—Yn. 14:2, 3; Ebr. 9:15.

3 Kwa kudumisha ukamilifu mpaka kifo chake, Yesu alitakasa jina la Baba yake na kuonyesha kwamba mwanadamu mkamilifu angeweza kuthibitika kuwa mwaminifu kwa Mungu chini ya kila aina ya jaribu ambalo huenda Shetani akaleta dhidi yake. Kifo chake kiliandaa pia dhabihu kamilifu ya kibinadamu iliyohitajiwa kukomboa wazao wa Adamu na kuwezesha wengi kadiri watakavyotumia imani kuishi milele katika dunia paradiso. Kwa sababu ya yote ambayo yangetimizwa kupitia kifo cha Yesu, ilifaa sana kwake awaagize wanafunzi wake wakumbuke kifo chake.—rsSW kur. 352, 353.

JINSI TUNAVYOWEZA KUONYESHA UTHAMINI

4 Ulimwengu una miadhimisho mingi mwakani, na mengi yanafanywa kuiendeleza. Kwa upande mwingine, Chakula cha Bwana cha Jioni ndio mwadhimisho pekee ambao wafuasi wa hatua za Yesu waliojitoa waliamriwa kushika. Bila shaka, ndio mwadhimisho wa mwaka ulio mkuu kupita yote kwa Wakristo wote wa kweli. Je, umaana mkubwa wa kukumbukwa kwa Chakula cha Bwana cha Jioni haupaswi utusukume tuukazie fikira wakati wa Machi?

5 Labda tungeweza kuchukua dakika chache kila juma wakati wa Machi kuzungumza pamoja na wanafunzi wetu wa Biblia maandiko ambayo hukazia umaana wa kifo cha Kristo na kuwaonyesha msingi wa Ukumbusho. Tungeweza pia kuwatia moyo wafuate kwa ukaribu usomaji wa Biblia wa Ukumbusho wa Machi 25-30, kama ambavyo imeonyeshwa kwenye 1991 Calendar of Jehovah’s Witnesses au katika toleo hili la Huduma ya Ufalme Yetu. Hiyo yaweza kusaidia kuupa kina uthamini wao wa Chakula cha Bwana cha Jioni.

6 Kwa kuwa mwadhimisho wa Ukumbusho utakuwa Jumamosi, itakuwa rahisi zaidi kwa wengi kuratibu mambo yao ili kuhudhuria. Wahubiri wengi wanajinufaisha na uhakika wa kwamba kuna miisho ya juma mitano katika Machi na kutumikia wakiwa mapainia wasaidizi. Hiyo inawaruhusu kuwa na ushiriki zaidi katika kukazia mwadhimisho wa Chakula cha Bwana cha Jioni.

7 Kwa sababu ya umaana wa mwadhimisho wa Ukumbusho, acheni sisi tufanye kila tuwezalo kusaidia wengine wahudhurie. Vikumbusho vyenye kusaidia juu ya mambo mengine mengi ya kushughulikiwa na wazee yaweza kupatikana katika Huduma ya Ufalme Yetu ya Machi 1989 na April 1990.

8 Sisi na tuikaribie siku hii ya maana kupita zote katika 1991 tukiwa na utambuzi ulio wazi na uthamini wenye kina kwa ajili ya yote ambayo kifo cha Yesu humaanisha kwa ainabinadamu. Ndiyo, sisi sote na tuwepo jioni ya Machi 30 huku waabudu wa kweli wa Yehova waaminifu watiipo amri ya ‘kuendelea kutangaza kifo cha Bwana, mpaka awasilipo.’

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki