Wimbo 75
Sifa Yenye Furaha kwa Yehova
1. Kwa sauti ya furaha
Tunatoa sifa nyingi.
Sababu Mungu hutoa
Vitu tunavyohitaji.
Kwa mioyo ya furaha
Sisi tunasifu Mungu.
Na asante zetu zimwendee;
Tunafurahia yeye.
2. Alitoa Mwana wake,
Ili kuwe na wokovu.
Tunasali jina lake
Liondolewe lawama.
Na tunathamini sana
Ushirika wetu naye.
Tunamupenda sana daima;
Tunamupenda kwa moyo.
3. Ona utukufu wako.
Furaha kwa uongozi!
Tunamwabudu Yehova,
Tunatumaini yeye.
Chini ya uvuli wake,
Tunaupata ulinzi!
Mioyo yetu inamwimbia;
Tuna shauku na yeye.