Wimbo 176
Mkaribisheni Mfalme Anayekuja!
1. Ni wakati wa kukaribisha sana
Mungu Mwenyezi, mwenye vitu vyote.
Yeye na Yesu wakusanya taifa
Zote, na mbingu zinaimba kwa shangwe ya vita.
‘Inua vichwa malango,’ mufurahi;
Mufalme mutukufu atashinda.
Ni wakati wa Yehova kuletea
Watu utawala wa Yesu Kristo.
Ufalme utaonyesha nguvu zake,
Na enzi yake iwe juu ya dunia.
2. Na Bwana Mwenye Enzi Kuu, Yehova.
Yeye ana Ufalme wa milele.
Akaribishwe kwa mikono miwili;
Na Mufalme ajaye ajue twamutetea.
Inuliweni, malango! Tunaleta
Habari njema za furaha nyingi.
‘Yehova ni hodari na ni shujaa.’
Tumletee zawadi na kumtii.
Ni wakati wake wa kubarikia.
Na tuseme “Karibu” Mufalme ajaye.