Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 3/92 uku. 2
  • Yatangazeni Matendo ya Yehova

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Yatangazeni Matendo ya Yehova
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1992
  • Habari Zinazolingana
  • Wanatakwa—Mapainia-Wasaidizi 2,500
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Mradi Mzuri kwa Ajili ya Mwaka Mpya wa Utumishi
    Huduma ya Ufalme—2007
  • Tangazeni Kotekote Sifa Bora za Yehova
    Huduma ya Ufalme—2007
  • Je! Wewe Unaweza Kufanya Upainia Msaidizi?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1992
km 3/92 uku. 2

Yatangazeni Matendo ya Yehova

1 “Yatangazeni matendo yake kati ya mataifa, litajeni jina lake kuwa limetukuka . . . , kwa kuwa ametenda makuu.” (Isa. 12:4, 5) Wewe waitikiaje sihi hiyo? Tunapofikiria juu ya matendo ya Yehova kuelekea sisi sote na tukiwa mtu mmoja mmoja, je! mioyo yetu haisukumwi kuwaambia wengine? Yapata miaka 73 iliyopita, Yehova aliweka huru watu wake kutoka kwa utumwa wa Kibabuloni. Tangu 1919 ibada ya kweli imeimarishwa na sasa imeenea kwenye sehemu zote za dunia. Kadiri ile ambayo Yehova amefanya hayo imepita matarajio yetu. Ukiwa mtu binafsi, je! wewe unathamini kwa kina jinsi gani mwongozo wa Mungu, ulinzi, na baraka? Je! waweza kufanya mengi zaidi kutangaza matendo yake na kulitukuza jina lake?

2 Majira ya Ukumbusho hutukumbusha tendo la kimungu tutakalokuwa wenye shukrani kwalo kwa umilele wote. Mwezi wa Aprili ungekuwa hasa wakati ufaao kumwonyesha Yehova shukrani na uthamini wetu kwa kujiandikisha kuwa painia msaidizi. Pia, ukifanya upainia msaidizi wakati wa ziara ya mwangalizi wa mzunguko, utafaidika zaidi kutokana na msaada wake na kitia moyo katika huduma.

3 Mara nyingi, mipango hufanikiwa wakati vikundi vya wahubiri vinapojiandikisha kuwa mapainia wasaidizi. Ratiba nzuri yaweza kupangwa ili kwamba wote waweze kuwa na mtu wa kuhubiri nao, na akina dada wenye watoto wadogo waweza kupanga wasaidiane. Kwa mipango mizuri, wengi wamepata kwamba si vigumu sana kufikia takwa la saa 60. Hilo lamaanisha kutoa saa 2 tu kwa wastani kila siku au saa 15 kwa juma katika huduma. Mapainia wasaidizi wengine hutoa ushahidi saa moja au mbili kabla au baada ya kazi yao ya kimwili na wanakuwa na vipindi virefu zaidi vya utumishi wakati wa miisho juma.

4 Hata ikiwa huwezi kufanya upainia msaidizi, huenda ukaweza kuongeza utendaji wako wa utumishi wa shambani. Pia, kwa kutoa msaada wa usafiri au kufanya kazi pamoja na wengine wanaopainia, utakuwa kitia moyo kwao. Chochote tuwezacho kufanya ili kutangaza jina la Yehova na matendo yake halitakosa kuonwa na Mungu wetu mwenye uthamini.—Mal. 3:16.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki