Wimbo 220
Paradiso Yetu: Ya Sasa na ya Wakati Ujao
1. Yehova tunakusifu kwa
Paradiso ya ’roho,
Tujifunzamo, kukutana
Hata kusaidiwa.
Tupige asante
Kwa mibaraka
Utumishi wako
Watupa shangwe!
Upendo kwako na jirani
Ni kifungo cha nguvu.
Watuunganisha shambani,
Ili tusianguke!
2. Na usimamizi wa haki
Umempa Kristo Yesu.
Katika kiti cha Ufalme
Anatawala vyote.
Twakusifu Mungu,
Kwa kujulisha
Unataka watu
Kuwakusanya.
Mwenendo wetu upatane
Na tunayohubiri,
Ili tusiwakwaze kamwe
Kondoo tufunzao!
3. Na baada ya siku kuu
Ya pigano la Mungu,
Ibilisi na mashetani
Watafungwa shimoni,
Watumishi kale
Kufufuliwa,
Wakutumikie
Paradisoni.
Na watasaidia wote
Wawe wakamilifu;
Ndipo furaha za milele,
Kufika duniani!