Wimbo 225
Kukaribia Karibu Sana na Yehova
1. Kibali chako, Mungu,
Tunaithamini.
Kama watoto wako
Tukukaribie.
Wewe kuwa Rafiki
Ni hazina bora.
Upendo wako ni safi.
Tunakushukuru.
2. Kama Muchunga wetu,
Ulitufadhili
Kwa Kristo ukatwita
Toka ulimwengu.
Ulisamehe dhambi
Kwa rehema nyingi.
U mwenye fadhili sana
Tukaapo nawe.
3. Mwanao katufunza
Tukujue wewe.
Wororo, wema wako,
Watupa ajabu.
Twataka kukujua,
Tukukaribie.
Urafiki na udumu;
Tukutumikie.