Wimbo 34
Kuishi Kulingana na Jina Letu
1. Yah Mweza Yote, wa tangu milele,
U haki, pendo si la kifani,
Chemuchemi ya kweli, hekima, na
U Mwenyezi Mukuu mbinguni.
’Kumi maelfu malaika zako
Uumbaji wakusifu sana.
Unatuita Mashahidi wako;
E’ na tuishi kwa jina letu!
2. Tusaidie, Yah, nyakati zote
Tukustahi, “kondoo” kulisha,
Kuzifuata hatua za Yesu
Tukifuatisha maagizo.
Tutatunza mwendo wetu daima,
Tusiliharibu jina lako.
Ni pendeleo kuwa Mashahidi;
E’ na tuishi kwa jina letu!
3. Na tufanyapo kazi bora yako,
Upendo, amani, vikiwako,
Tu radhi kimungu nyakati zote;
Furaha tele kwa sifa zako.
Daima tuishi kwa jina letu;
Kweli ya uzima tupe watu;
Tufurahishe sana moyo wako,
Ee Yehova, Mufalme wetu!