Onyesha Hangaikio kwa Wanaopendezwa
1 Zaidi ya wote wengineo, Yehova amekuwa mkarimu katika kuonyesha hangaikio kwa watu. Si kwamba tu ameandaa vitu vya kimwili kwa wingi bali pia ametupatia vitu vya kiroho tunavyohitaji na tunavyofurahia. Yeye hutuhangaikia sana hivi kwamba yeye hata huchunguza yale yaliyomo mioyoni mwetu.—Zab. 139:23.
2 Yesu alipokuwa duniani, alifuata kigezo cha Baba yake kwa ukamili katika kuhangaikia wengine. Wakumbuka mwanamume aliyemwambia Yesu, “Bwana, ukitaka, waweza kunitakasa”? Yesu aliitikia kwa kusema, “Nataka.” (Mt. 8:1-3) Yesu alipoona mjane mwenye kihoro, yeye alifanya nini? Alisimama ili kumsaidia. (Lk. 7:11-15) Je! wewe unaweza kuwa macho zaidi kuhangaikia wanaopendezwa?
3 Kwa kumwiga Baba yetu, Yehova, na Mwanae, Yesu Kristo, ni lazima sisi pia tupendezwe kibinafsi na wengine. Tunafanya hivyo kwa kuweka rekodi ya nyumba kwa nyumba iliyo sahihi. Hilo latia ndani kuandika jina na anwani au mahali anapoishi mtu anayependezwa pamoja na habari iliyozungumziwa katika ziara ya kwanza. Kisha, kabla ya kufanya ziara ya kurudia, ujitayarishe vema. Ikiwa tuliacha magazeti katika ziara ya kwanza, labda ziara yetu ya kurudia yaweza kutegemea wazo hususa linaloelezwa katika mojawapo makala. Ona jinsi hilo laweza kufanywa.
4 Ikiwa uliacha Mnara wa Mlinzi la Septemba 15, 1992 na ukaelekeza kwenye makala “Kwa Nini Watu Wazuri Huteseka?” huenda ukatayarisha kukazia Ufunuo 21:4 na Yohana 17:3 kwenye ziara yako ya kurudia.
Kwa mfano, baada ya kusoma Ufunuo 21:4, kama linavyokaziwa katika ukurasa 7, huenda ukauliza:
◼ “Sisi tunaweza kuwaje sehemu ya ulimwengu kama huo? [Ruhusu itikio.] Sikiliza yale ambayo Yesu alisema yahitajiwa ili kupata uhai katika ulimwengu kama huu.” Kisha soma Yohana 17:3, ukikazia kwamba uhai wa milele katika ulimwengu mpya wenye amani waweza kupatikana kwa kutwaa maarifa juu ya Mungu na Kristo. Ikiwa kuna kupendezwa fulani, jaribu kuanzisha funzo katika trakti Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani.
5 Huenda ukapata itikio zuri kwa kuzungumzia jambo uliloteua kutoka Amkeni! la Oktoba 8, 1992 kuhusu “Wewe Unaweza Kushinda Hisiamoyo Zisizofaa.” Unapofanya ziara ya kurudia, huenda ukategemeza mazungumzo yako kwenye Wafilipi 4:6, 7.
Huenda ukauliza:
◼ “Wewe unaamini ni nini utatuzi wa kushinda hisiamoyo zisizofaa leo?” Kubali itikio halafu useme: “Kwa kupendeza, Biblia huonyesha kanuni ambazo, zinapotumiwa, huchangia kwenye amani ya akili na moyo. [Elekeza fikira kwenye mambo yafaayo kutoka Wafilipi 4:6, 7.] Biblia huelekeza kwenye wakati ambapo wote wataishi kwa kufuata kanuni za Biblia na hakutakuwako hali zinazoleta hisiamoyo zisizofaa.” Kisha kazia baraka nyinginezo za wakati ujao kwa kuzungumzia trakti Uzima Katika Ulimwengu Mpya Wenye Amani, na uongoze kwenye funzo.
6 Namna gani ikiwa mwenye nyumba tayari ana kimojapo vichapo vyetu? Kwa nini usikitumie kuanzisha funzo? Ikiwa ni kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani, fungua kwenye yaliyomo na umwulize mwenye nyumba achague kichwa ambacho angependa kuzungumzia. Halafu unaweza kuanzisha funzo kwa kuzungumzia fungu moja au mawili.
7 Kuonyesha hangaikio kwa watu wanaopendezwa kwa kutayarisha vizuri na kufanya ziara za kurudia zenye matokeo huonyesha kwamba sisi tunamwiga Mungu na Kristo, tukitaka wengi kadiri iwezekanavyo waweze kuokolewa.—2 Pet. 3:9.