Wimbo 177
Inatupasa Kuwa Watu wa Aina Gani?
1. Tunaikaribisha siku ya Yehova.
Tunaelekeza moyo kwake na Yesu.
Usiku waisha Siku karibu;
Mambo yote ya Shetani yaishe.
Daima tuone uhitaji wa sala.
Tujitahidi, sala inahitajiwa.
Tutoe sala kwa moyo wetu wote,
Tuwe na amani ya akili atoayo.
2. Furaha na amani inakuwa wazi.
Na tumekuwa tamasha ya watu wote.
Je! tuwe watu wa aina gani?
Ni vitendo gani vitakatifu?
Tueleze wengine juu ya Ufalme
Na pia mbingu mupya na dunia mupya
Na uadilifu utakaa humo.
Tutie bidii kusema habari hizo.
3. Matendo, na mwenendo wetu tudumishe
Kufuata kanuni za faida kubwa.
Yesu alitusafishia dhambi,
Na sasa tuna amani ya Mungu.
Daima tuwe bila doa wala waa;
Sisi watumishi wa Yehova tu huru.
Na tukiwa na urafiki na yeye,
Atatusaidia mpaka kufika mwisho.