Wimbo 32
“Nyumba kwa Nyumba”
1. Kila nyumba, Kila ’lango,
Neno twaeneza.
Kila muji, Kila shamba,
“Kondoo” walishwa.
Habari njema za ’Falme,
Yesu alisema.
Vijana hata wazee
Wanazitangaza.
2. Kila nyumba, Kila ’lango,
Wokovu twataja.
Wanaomwita Yehova
Kwao unakuja.
Wataitaje jina la
Wasiyemujua?
Nyumbani, ‘langoni pia,
Jina fikisheni.
3. Kwa kweli, Si kila ’lango
Tunakosikiwa;
Kwingine tunagombezwa,
Bila kusikiwa.
Siku za Yesu si wote
Walimusikia.
“Kondoo” wangesikia;
Hatuvunjwi moyo.
4. Basi twende kila ’lango
Tweneze habari.
“Kondoo” na “mbuzi” pia
Kujichagulia.
Angaa Yah tutataja,
Kweli kutangaza.
Tuendapo kila ’lango,
’Taona “Kondoo.”