Wimbo 87
Chakula cha Jioni cha Bwana
1. Yehova, Baba wa mbinguni,
Ni jioni takatifu!
Siku ya kumi na ine Nisani
Kukawa ’tukufu, pendo.
Kondoo kupitwa kaliwa
Israeli wakatoka.
Baadaye Bwana akamwaga damu,
Kuutimiza unabii.
2. Mbele zako tumekutana,
Tukiwa kondoo zako,
Tusifu pendo lilishusha Yesu,
Tuheshimu jina lako.
Mbele yetu tunayo meza.
Ya divai na mukate.
Ni mifano, twajua; ni vikumbusho
Vya chakula cha kutulisha.
3. Mukate mufano wa mwili
Yesu alitutolea.
Divai kikombeni ni mufano
Damu yake ya fidia.
Ukumbusho na tuukaze
Moyoni, na akilini.
Hivyo daima na twende kama Kristo,
Tupate uzima milele.