Wimbo 64
Imani Kama Ile ya Abrahamu
1. Yuna furaha atakaye
kujua Neno;
Mungu kwa uwezo Wake
Yote ayajua.
Kwa faraja na imani
Katufunulia
Yatakayotujilia,
Nayo yatimia.
2. Angalia Abrahamu,
Yule anakwea
Moria kwenye kilele,
Na Isaka pia.
Yah kaagiza Abra’mu
Achinje mwanake
Dhabihu ya kutolea,
Mapenzi yafanywe.
3. Kashinda jaribu lile,
Mufano katoa
Namuna Mwana wa Mungu
Alitufidia.
Wataka uzima kwake?
Lazima utii.
Amini Kiabrahamu
Na uwe mutii.