Wimbo 190
Wimbo kwa Yehova
1. Twaimba wimbo kwa Mungu,
Kwa kutuongoza njia.
Tunamushukuru sana
Twamwimbia sifa.
Ni mwenye fadhili sana
Tu karibu sana naye.
Kweli ’metuweka huru.
Tu mali ya yeye.
2. Shukurani kwa Mungu kwa
Nuru, inatuongoza.
Humulika waziwazi
Kuleta faraja!
Twashukuru kwa tumai;
Hatupapasi gizani
Twayaweza matatizo.
Moyo wafurahi.
3. Twaimba sauti tamu
Tukimuabudu Mungu,
Kupitia Yesu Kristo
Tunatoa sala:
“Yehova Mungu wa pendo,
Pokea shukrani zetu.
Sikia maombi yetu,
Kwa ulinzi wako.”