Wimbo 155
“Mkaribishane”!
1. Karibishaneni kama vile Kristo Yesu!
Nduguyo kafiwa na Kristo, akaribishwe.
Basi wenye nguvu wasaidie dhaifu,
Walishike tumaini, wafuate haki.
Maana yaliyoandikwa na manabii
Yaweza kutupa faraja na tumaini.
Tujaribu daima kupendeza wengine,
Tupendezwe na mambo ya ndugu yetu pia.
2. Yehova anakusanya watu wa amani.
Ni wakati wa Yesu kurudisha amani.
Avuta watu wa taifa zote na lugha,
Anatia ndani yao kupenda sheria.
Kwa utukufu wa Mungu, tunakaribisha
Hatubagui sisi ni rafiki za wote.
Tunafuatisha moyo mukubwa wa Mungu.
Kama Mwanaye, tupanue mioyo yetu.
3. Tuwasihi wote pia, wamutukuze Yah,
Tufurahi na taifa lake tumusifu.
Na tutangaze nyumbani na barabarani,
Habari njema za Mungu kwao watu wote.
Ni heshima kubwa kuimba sifa za Mungu.
Hizi ni siku za mwisho kwa waovu wote.
Tupende ndugu zetu, Mungu awe wa kweli;
Karibishaneni kama tunavyoambiwa.