Wimbo 116
“Ni Lazima Msaidie Wale Walio Dhaifu”
1. Kuna unyonge mwingi
Tulio nao.
Hata hivyo, Yehova
Anatupenda.
Ni mwenye rehema,
Njia zake bora.
Kama yeye tupende,
Tusaidie.
2. Badala ya laumu,
Na tukumbuke
Inafaidi sana
Kuwafadhili.
Tuwe na bidii,
Tuwatie moyo.
Na kuwategemeza,
Wafarijike.
3. ‘Ni nani mudhaifu?’
Kakaza Pa’lo.
Wahisivyo, tuhisi,
Tuhurumie.
Enyi wenye nguvu:
“Wasaidieni.”
Na walikombolewa,
Ili waishi.
4. Wanyonge ’saidie,
Mungu asema.
Na tuwasaidie
Tubarikiwe.
Ni mali ya Mungu.
Na wapate nguvu.
Tuwape musaada
Tutiwe nguvu.