Wewe Huonyesha Roho ya Aina Gani?
1 Paulo alimalizia barua yake kwa kutaniko la Wafilipi kwa kitia-moyo hiki: “Fadhili isiyostahiliwa ya Bwana Yesu Kristo iwe pamoja na roho ambayo nyinyi [mwaonyesha].” (Flp. 4:23, NW) Aliwapongeza kwa kupendezwa kikweli na kuhubiri habari njema na vilevile hangaikio changamfu lenye upendo kwa hali njema ya mtu na mwenzake.—Flp. 1:3-5; 4:15, 16.
2 Inapasa kuwa tamaa yetu kuonyesha roho hiyohiyo katika kutaniko letu. Wote waonyeshapo bidii, fadhili, na ukaribishaji-wageni, hii hutokeza roho ionekanayo dhahiri na watazamaji. Roho iliyo chanya na yenye upendo huleta umoja na maendeleo ya kiroho. (1 Kor. 1:10) Roho isiyofaa hutokeza kuvunjika moyo na moyo usio kamili.—Ufu. 3:15, 16.
3 Wazee Ongozeni: Wazee wana daraka la kuwa na roho nzuri, iliyo chanya miongoni mwao wenyewe na ndani ya kutaniko. Kwa nini? Kwa sababu kutaniko laweza kuathiriwa na mtazamo na mwenendo wao. Twathamini kuwa na wazee walio na bidii katika utumishi wa shambani, ambao hutusalimia kwa tabasamu changamfu na neno la fadhili, na walio chanya na wenye kujenga katika shauri lao, liwe latolewa faraghani au jukwaani.—Ebr. 13:7.
4 Bila shaka, sisi sote twapaswa kufanya sehemu yetu ili kufanya kutaniko liwe lenye urafiki, ukaribishaji-wageni, bidii, na lenye kujali mambo ya kiroho. Tukiwa watu mmoja-mmoja, twaweza kuonyesha uchangamfu na upendo katika ushirika wetu pamoja na wengine. (1 Kor. 16:14) Hakupaswi kuwa na ubaguzi wa umri, jamii, elimu, au hali ya kiuchumi miongoni mwetu. (Linganisha Waefeso 2:21.) Kwa sababu ya tumaini letu, twaweza kuonyesha roho ya shangwe, ukarimu wa ukaribishaji-wageni, na bidii katika huduma.—Rum. 12:13; Kol. 3:22, 23.
5 Wale wote wanaoshirikiana nasi, kutia na wapya, wanapasa kufanywa wahisi wamekaribishwa na wahisi upendo na ujitoaji wa kidugu. Kwa huduma yetu na kwa kuonyesha sifa nzuri za Kikristo, twatoa ithibati kwamba kutaniko ni “nguzo na msingi wa kweli.” (1 Tim. 3:15) Pia twaona usalama wa kiroho kupitia “amani ya Mungu” inayolinda mioyo yetu na nguvu zetu za kufikiri. (Flp. 4:6, 7) Sisi sote na tujitahidi kuonyesha aina ya roho ambayo itatuhakikishia kwamba twafurahia fadhili zisizostahiliwa za Yehova kupitia Bwana Yesu Kristo.—2 Tim. 4:22.