‘Nilishindwa Kukiweka Chini’
KATIKA kisiwa cha Karibbea cha St. Lucia, mwanamke mmoja aliye muuzaji dukani katika mji mkuu alipata nakala moja ya kitabu Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Mtu yule aliyempa kitabu hicho anaandika hivi:
“Kabla juma halijamalizika, mwanamke huyo aliniita dukani mwake mara tatu nilipokuwa nikipita mbele ya duka hilo. Alikuwa amesoma visehemu fulani vya kitabu hicho na alitaka maelezo zaidi juu ya moto wa mateso, nafsi, kutokuwa kwa Mariamu mama ya Mungu, na mambo kama hayo. Ingawa yeye alikuwa muuzaji dukani mwenye shughuli nyingi na hakuwa mtu wa kusoma sana, alikisoma kitabu hicho katika muda wa majuma mawili, naye alisema: ‘Sijapata kusoma sana hivi maishani mwangu. Hata kichwa kiliponiuma kwa sababu ya kusoma, nilishindwa kuweka chini kitabu hicho.’ ”
Kichapo hicho kinazungumza karibu kila fundisho la Kibiblia linalotokeza mabishano, kikiukusanya pamoja ushahidi kwa njia inayolenga shabaha barabara na yenye kueleweka hivi kwamba majibu yanayotolewa kwa maulizo yanakuwa wazi kwa msomaji. Pata nakala yako, nawe utaelewa ni kwa nini kinathaminiwa sana.
Tafadhali mnipelekee, mkiwa mmelipia malipo ya posta, kile kitabu chenye jalada gumu cha kurasa 256 kilicho na picha, kinachoitwa Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani. Mimi nimewapelekea Kshs. 35.00 (Tshs. 100.00).