Wimbo 102
Furaha ya Ufufuo
1. Lazaro kalala
Kaburini fo.
Dada wakalia!
Wasimwokoe.
‘Yesu angewahi
Atangulie,
Kuzuia kifo,
Kisingekuja.’
Yesu kaburini
Kapaza mwito.
Kwa nguvu kaita,
‘Lazaro, njoo!’
Na ajapofungwa
Sanda, atii.
Wakamusikia
Lo! shangwe hiyo!
2. Waliotaraji
Kukombolewa,
Wahuzunikia
Kifo cha Yesu.
Rafiki wamweka
Mule kaburi.
Lo, huzuni gani
Na majonzi we!
Mungu akashinda
Nguvu Hadesi.
Akamufufua,
Siku ya tatu.
Akaonwa nao
Wafuasiye.
Yuna funguo za
Kifo, Hadesi.
3. Adamu kaweka
Sote kifoni;
Kurudi kwa wafu
Katika Kristo.
Walio Hadesi
Watasikia
Sauti yake na
Kutoka hai.
Mbele zake Mungu
‘Tahukumiwa
Kwa matendo yao
Ya muda huo.
Akiyaandika
Majina yao,
Waishi katika
Dunia mupya.