Wimbo 158
Umoja Wetu wa Kikristo
1. Ni nani yu kama Yehova,
Chanzo cha umoja ndiye!
Kufunza kweli, tuwekwe huru,
Alimutuma Mwanaye.
Akaweka musingi wa
Umoja katika Yesu.
Kuwaunganisha kama jamaa
Washikao Neno lake.
2. Sisi wenye umoja naye
Yesu, twadaiwa nini?
Mawazo, Mwenendo yapatane,
Tufanye penzi la Mungu.
Kazi za mwili huzuni,
Tunda la roho furaha.
Na furaha zaidi kwa kutoa,
Tunapofuata Mungu.
3. Uone mupango wa Mungu,
Ni kinga na ni mwongozo.
Ukweli ukiturekebisha,
Tutadumu umojani.
Mungu anataka nini?
Tuonyeshe sifa gani?
Haki na fadhili, kisha kiasi,
Kwenda njia yake njema.