Wimbo 36
“Wenye Furaha ni Wenye Hali Pole”
1. Mungu hubariki wapole;
Furaha yao ni kubwa.
Shidani hawatasumbuka,
Wanamungojea Mungu.
Hawawajali waovu,
Wanaojiweka juu.
Uzima hao watakosa,
Wanyauke kama nyasi.
2. ‘Mimi nalikuwa kijana,’
Kasema hivyo Daudi.
‘Sijaona mwema aachwa,
Mwana aomba chakula.’
Basi Mungu ’tumaini
Tendea watu mema, na
Ukifurahia Yehova,
Atakubariki sana.
3. Watatokomea waovu;
Wawe hawaonekani.
Wapole wataamanika
Na kudumu duniani.
Basi tuzidi kusema
Neno lina roho, kweli
Na tuwe wapole, wanana
Kwa ’wazo na tutendayo.