Wimbo 41
Sifu Yehova, Mwamba
1. ‘Sikilizeni, Mbingu; dunia,
Sikilizeni nawaambia.
Mafundisho yangu kutonatona,
Kweli zangu zinyeshe; kama mvua.’
2. Tuutangaze Ukuu wa Yah,
Wote wajue ukuu wake.
Wote wa kundini kushangilia;
Kazi kamilifu kumusifia.
3. Wa haki Mungu Sifa ni kwake.
Njia zake ni zenye hekima.
Aonyesha sana yuko hakini,
Yehova Mwamba wetu ni amini.
4. Na tumwogope Mungu wa kweli;
Tuzitii za Mungu amuri
Tusitende ovu Upande wetu.
Kwa moyo safi twahudumu Mungu.