Neno la Mungu Huandaa Mwongozo
1 “Twaishi katika ulimwengu wenye matatizo mengi mno na utatuzi mchache mno. Mamilioni wengi hukosa chakula kwa ukawaida. Hesabu zenye kuongezeka ni wazoefu wa dawa za kulevya. Familia zaidi na zaidi zinavunjika. Daima katika habari ni ngono ya watu wa ukoo na jeuri ya familia. Hewa tunayopumua na maji tunayokunywa vinatiwa sumu polepole. Wakati uo huo, zaidi na zaidi kati yetu wanaathiriwa na uhalifu.”
2 Hivyo ndivyo kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? kinavyoanza. Utangulizi wacho unahusu sana leo kuliko wakati ambapo kitabu hicho kilipochapishwa miaka mitano iliyopita. Watu wanahitaji kujua kwamba Neno la Mungu hutoa mwongozo na kuandaa utatuzi wa matatizo yote yanayowapata. Tutajitahidi kusaidia watu Desemba kwa kuwatolea New World Translation na kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? Bila shaka, kumwachia mtu fasihi tu si uhakikisho wa kwamba atakubali mwongozo wa Mungu. Lazima tufanye ziara za kurudia tukiwa na mradi wa kuanzisha funzo la Biblia. Twahakikishiwa msaada ikiwa tutajitahidi. (Mt. 28:19, 20) Hapa pana utoaji mbalimbali uliodokezwa:
3 Ukimkuta mtu mzee unaweza kujaribu mfikio huu:
◼ “Je, naweza kukuuliza: Ulipokuwa kijana, watu katika jamii walitendeanaje? [Ruhusu itikio.] Hali ni tofauti sana sasa, sivyo? Unafikiri sababu ya badiliko hilo ni nini? [Ruhusu itikio.] Kwa kweli tunaona utimizo wa unabii mmoja katika Biblia. [Soma 2 Timotheo 3:1-5.] Mbali na kufafanua tu jinsi ulimwengu ulivyo leo, Biblia huahidi ulimwengu bora katika wakati ujao ulio karibu. Ndiyo sababu tunatia kila mtu moyo aisome Biblia. Je, uliona jinsi lugha ilivyo wazi katika Biblia, New World Translation, niliyokuwa nikisoma?” Eleza kwamba imeandikwa katika Kiingereza cha kisasa, kinachoifanya Biblia ieleweke. Onyesha kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?, na uonyeshe sura ya 10, inayoelezea unabii mwingine ambao tumeona umetimizwa. Toa Biblia na kitabu kwa mchango wa kawaida.
4 Unapomrudia mtu mzee uliyemwangushia Biblia na kile kitabu, unaweza kusema:
◼ “Tulipoongea wakati uliopita, tulikubaliana kwamba katika njia nyingi jamii imebadilika kuwa mbaya zaidi ikilinganishwa na vile maisha yalivyokuwa miaka michache tu iliyopita. Hata hivyo, nimerudi ili kukuonyesha kwamba Biblia hutoa matazamio ya ulimwengu bora zaidi kwa wakati ujao. [Soma Ufunuo 21:3, 4.] Kujua kwamba hili ni Neno la Mungu kwapaswa kututie moyo tuchunguze Biblia inasema nini zaidi.” Fungua kitabu Neno la Mungu kwenye sura ya 14, na usome mafungu 3-4. Toa funzo la Biblia nyumbani bila malipo.
5 Ukimhusisha kijana katika mazungumzo, unaweza kusema:
◼ “Ningependa kukuuliza swali: Ukiwa kijana, je, unafikiri una sababu ya kuwa na maoni yafaayo kuhusu wakati ujao? Wakati ujao unaonekanaje kwako? [Ruhusu itikio.] Kwa uzuri, kuna sababu halisi ya kuwa mwenye maoni yafaayo kuhusu wakati ujao. [Soma Zaburi 37:10, 11.] Kwa kuwa watu wana maoni yaliyotofautiana juu ya Biblia na yaliyomo yake, tumechapisha kitabu hiki, Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? Ona sababu kinachotoa za kusoma Biblia. [Soma mafungu 16-17 kwenye kurasa 10-11.] Mara tu tunaposadikishwa kwamba yale ambayo Biblia husema ni kweli, tunakuja kuwa na tumaini hakika la wakati ujao. Ukipenda kusoma kitabu hiki, nitafurahi kukuachia nakala kwa mchango mdogo wa _________.”
6 Unaporudi kumwona kijana aliyekubali kitabu “Neno la Mungu,” unaweza kuanza kwa kusema hivi:
◼ “Nilithamini kusikia jinsi unavyohangaikia wakati ujao. Kumbuka kwamba nilikuonyesha andiko la Biblia linalotuahidi wakati ujao wenye furaha na usalama. Hili ni jingine. [Soma Ufunuo 21:3, 4.] Kitabu nilichokuachia hutoa uthibitisho wenye kusadikisha kwamba Biblia ni Neno la Mungu, si la mwanadamu. Jambo hilo lina madokezo yenye maana. Angalia yalivyo. [Soma mafungu 1-2 kwenye kurasa 184-185.] Ikiwa ungependa, nitafurahi kujifunza Biblia pamoja nawe bila malipo.” Funzo likikubaliwa, uliza ikiwa mtu huyo ana nakala ya Biblia. Ikiwa hana, mtolee New World Translation kwa mchango wa kawaida.
7 Mtu ambaye hajui mahali pa kupata mwongozo wa kukabiliana na matatizo ya maisha anaweza kuitikia mfikio huu:
◼ “Twaishi wakati ambapo kila mtu anakabiliwa na matatizo mazito. Wengi huendea washauri wa aina zote ili kupata mwongozo. Wengine huendea watu walio na uwezo wa kufumbua mafumbo ili kupata msaada. Unafikiri twaweza kupata wapi shauri la maana ambalo litatufaidi kikweli? [Ruhusu itikio.] Biblia huonyesha jambo la maana ambalo sisi sote twahitaji kung’amua.” Soma Yeremia 10:23. Fungua Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? kwenye ukurasa 187, na usome fungu la 9. “Kitabu hiki kitakusaidia ung’amue jinsi matatizo yote yatakavyoondolewa, chini ya Ufalme wa Mungu. Ungependa kukisoma? Twakitoa kwa mchango mdogo wa _________.”
8 Ikiwa katika ziara ya kwanza uliongea kuhusu uhitaji wa mwanadamu wa kupata mwongozo, unaweza kuendeleza mazungumzo yako kwenye ziara ya kurudia kwa kusema:
◼ “Tulipokutana mara ya kwanza, tulikubaliana kwamba twahitaji mwongozo kutoka kwa Mungu ikiwa tutakabiliana kwa mafanikio na matatizo ya maisha. Kuhusu hilo, nafikiri utathamini maelezo ya kumalizia ambayo yanatolewa katika kitabu nilichokuachia. [Soma mafungu 12-13 kwenye ukurasa 189 katika kitabu Neno la Mungu.] Nafurahi kukutolea mtaala wa funzo la Biblia nyumbani bila malipo, na nimejitayarisha kukuonyesha jinsi ya kufanya hivyo sasa.”
9 Yehova atabariki jitihada zetu tunaposaidia wazee kwa vijana kuthamini ubora wa mwongozo wa Neno la Mungu katika maisha yetu.—Zab. 119:105.