-
BibliaKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Maandiko ili yalingane na maoni yetu wenyewe kwaweza kutokeza madhara yenye kudumu. (2 Pet. 3:15, 16)’ (2) ‘Mambo mawili yanaweza kutusaidia tuielewe Biblia kwa usahihi. Kwanza, fikiria muktadha (mistari inayotangulia na inayofuata) wa andiko lolote. Kisha, ulinganishe andiko hilo na maandiko mengine katika Biblia yanayoshughulikia habari zilezile. Kwa njia hiyo tunaliruhusu Neno la Mungu mwenyewe liongoze kufikiri kwetu, na ufafanuzi si wetu bali ni wake. Hivyo ndivyo vinavyofanya vichapo vya Mashahidi wa Yehova.’ (Ona ukurasa wa 193, 194, chini ya kichwa “Mashahidi wa Yehova.”)
‘Haina faida leo’
Unaweza kujibu hivi: ‘Nasi tunapendezwa na mambo yanayoweza kutufaidi leo, sivyo?’ Kisha unaweza kusema: (1) ‘Je, unakubali kwamba inawezekana kukomesha vita? . . . Je, hukubali kwamba kama watu wangejifunza kuishi pamoja kwa amani na wale wa mataifa mengine, huo ungekuwa mwanzo mzuri? . . . Biblia ilitabiri barabara jambo hilo. (Isa. 2:2, 3) Kwa sababu ya elimu ya Biblia, jambo hilo linatukia leo kati ya Mashahidi wa Yehova.’ (2) ‘Jambo fulani zaidi linahitajiwa—kuondolewa kwa wanadamu na mataifa yote yanayosababisha vita. Je, jambo hilo litatimia? Ndiyo, na Biblia inaeleza jinsi litakavyotimia. (Dan. 2:44; Zab. 37:10, 11)’
Au unaweza kusema hivi: ‘Naelewa ni kwa nini unaona hivyo. Ikiwa kitabu cha mwongozo hakifai, ungekuwa upumbavu kukitumia, sivyo?’ Kisha unaweza kuongezea: ‘Je, unakubali kwamba kitabu kinachotoa shauri zuri la kutuwezesha tuwe na maisha ya familia yenye furaha kinafaa kutumiwa? . . . Nadharia na mazoea yanayohusu maisha ya familia yamebadilika mara nyingi, na matokeo tunayoona leo si mazuri. Lakini wale wanaojua na kutumia yale ambayo Biblia inasema wana familia zenye furaha, zilizo imara. (Kol. 3:12-14, 18-21)’
‘Biblia ni kitabu kizuri, lakini hakina ukweli kamili’
Unaweza kujibu hivi: ‘Ni kweli inaonekana kwamba kila mtu ana maoni tofauti. Na hata ikiwa mtu anafikiri amelifahamu jambo fulani, mara nyingi anagundua kwamba kuna angalau jambo lingine ambalo hakulifikiria. Lakini kuna mtu ambaye hana udhaifu huo. Huyo ni nani? . . . Naam, ni Muumba wa ulimwengu wote.’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Ndiyo sababu Yesu Kristo alimwambia hivi: “Neno lako ni kweli.” (Yoh. 17:17) Kweli hiyo imo katika Biblia. (2 Tim. 3:16, 17)’ (2) ‘Mungu hataki tupapase-papase kwa kutojua; amesema mapenzi yake ni kwamba sisi tupate ujuzi sahihi wa ile kweli. (1 Tim. 2:3, 4) Kwa njia yenye kutosheleza kabisa Biblia inajibu maswali kama . . . ’ (Ili kuwasaidia watu fulani, huenda kwanza ukahitaji kuzungumzia uthibitisho utakaowasaidia kuamini kwamba kuna Mungu. Ona ukurasa wa 215-221, chini ya kichwa “Mungu.”)
‘Biblia ni kitabu cha wazungu’
Unaweza kujibu hivi: ‘Ni kweli kwamba wamechapisha Biblia nyingi. Lakini Biblia haisemi kwamba jamii moja ni bora kuliko nyingine.’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Biblia imetoka kwa Muumba wetu, naye hana ubaguzi. (Mdo. 10:34, 35)’ (2) ‘Neno la Mungu linawapa watu wa mataifa na makabila yote nafasi ya kuishi milele hapa duniani chini ya Ufalme wake. (Ufu. 7:9, 10, 17)’
Au unaweza kusema: ‘Sivyo hata kidogo! Muumba wa wanadamu ndiye aliyekuwa na haki ya kuwachagua wanadamu ambao angewaongoza waandike vitabu 66 vya Biblia. Na ikiwa aliamua kutumia wazungu, alikuwa na haki ya kufanya hivyo. Lakini ujumbe wa Biblia haukuwa kwa ajili ya wazungu tu.’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Ona aliyosema Yesu . . . (Yoh. 3:16) “Kila mtu” hutia ndani watu wa rangi yoyote. Pia, kabla ya kupanda mbinguni, Yesu aliwaambia wanafunzi wake maneno haya ya kuwaaga . . . (Mt. 28:19)’ (2) ‘Inapendeza kwamba, Matendo 13:1 husema juu ya mwanamume mmoja aitwaye Nigeri, jina linalomaanisha “mweusi.” Alikuwa mmoja wa manabii na walimu wa kutaniko la Antiokia, Siria.’
‘Mimi naamini Biblia yangu tu’
Unaweza kujibu hivi: ‘Ikiwa iko karibu, ningependa kukuonyesha jambo fulani ambalo nimeona kuwa lenye kutia moyo sana.’
Au unaweza kusema: ‘Watu wengi wanatumia tafsiri hiyo ya Biblia, nami nina moja katika maktaba yangu.’ Kisha unaweza kuongezea: (1) ‘Je, unajua kwamba mwanzoni Biblia iliandikwa katika Kiebrania, Kiaramu, na Kigiriki? . . . Je, unaweza kusoma lugha hizo? . . . Kwa hiyo, tunafurahi kwamba Biblia imetafsiriwa katika Kiswahili.’ (2) ‘Chati hii (“Orodha ya Vitabu vya Biblia,” katika NW) inaonyesha kwamba Mwanzo, kitabu cha kwanza cha Biblia, kilimalizika mwaka wa 1513 K.W.K. Je, unajua kwamba, baada ya Mwanzo kuandikwa, miaka 3,400 hivi ilipita kabla Biblia nzima kutafsiriwa katika Kiswahili?’ (3) ‘Tangu wakati huo, Kiswahili kimekuwa na mabadiliko mengi. Tumeona hivyo katika muda wa maisha yetu wenyewe, sivyo? . . . Basi tunathamini tafsiri za kisasa zinazoeleza kwa uangalifu zile kweli za awali katika lugha tunayosema leo.’
‘Ninyi mna Biblia yenu wenyewe’
Ona kichwa “Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.”
-
-
DamuKutoa Sababu kwa Kutumia Maandiko
-
-
Damu
Maana: Umajimaji wa ajabu sana unaozunguka katika mishipa ya wanadamu na katika wanyama walio na chembe nyingi, ukipeleka chakula na oksijeni, ukiondoa takataka, na kutimiza sehemu kubwa katika kuulinda mwili usiambukizwe magonjwa. Damu inahusika sana katika kuendeleza uhai hivi kwamba Biblia inasema “nafsi ya mwili iko katika damu.” (Law. 17:11) Akiwa Chanzo cha uhai, Yehova ametoa maagizo hususa kuhusu matumizi ya damu.
Wakristo wanaamriwa ‘wajiepushe na damu’
Mdo. 15:28, 29: “Roho takatifu na sisi wenyewe [baraza linaloongoza la kutaniko la Kikristo] tumependelea tusiwaongezee ninyi mzigo zaidi, ila mambo haya ya lazima, kuendelea kujiepusha na vitu vilivyotolewa dhabihu kwa sanamu na damu na vitu vilivyonyongwa [au, kuuawa pasipo kutolewa damu] na uasherati. Mkijiepusha kwa uangalifu na mambo haya, mtafanikiwa. Afya njema kwenu!” (Katika andiko hilo, kula damu kunalinganishwa na ibada ya sanamu na uasherati, mambo ambayo hatupaswi kuyafanya.)
-