Ukumbusho—Tukio la Umaana Mkubwa!
1 Jumapili, Machi 23, baada ya jua kushuka, tutasherehekea Ukumbusho wa kifo cha Kristo. (Luka 22:19) Kwa kweli hili ni tukio la umaana mkubwa! Kwa kushika uaminifu-maadili kwa Yehova hadi kifo, Yesu alithibitisha kwamba inawezekana binadamu kudumisha ujitoaji kimungu kabisa hata chini ya mkazo mkali, hivyo akitegemeza uhaki wa enzi kuu ya Yehova. (Ebr. 5:8) Kwa kuongezea, kifo cha Kristo kiliandaa dhabihu kamilifu ya kibinadamu inayohitajiwa kufidia wanadamu, ikifanya iwezekane kwa wale wanaodhihirisha imani kuishi milele. (Yn. 3:16) Kwa kuhudhuria Ukumbusho, tunaweza kuonyesha uthamini wetu wa kutoka moyoni kwa upendo wa Yehova na kwa dhabihu ya Yesu kwetu.
2 Wote wanatiwa moyo kufuatia programu ya usomaji wa Biblia inayoratibiwa kwa Machi 18-23, kama inavyoonyeshwa kwenye 1997 Calendar of Jehovah’s Witnesses. Pia, mazungumzo ya familia juu ya sura 112-116 za kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi yatasaidia kukazia fikira juma la pekee zaidi katika historia ya binadamu.
3 Je, waweza kuongeza wakati unaotumia katika huduma ya shambani wakati wa majira ya Ukumbusho? Watangazaji wengi watatumia kwa manufaa miisho-juma mitano katika Machi watumikie wakiwa mapainia-wasaidizi. Kwa nini usiwe miongoni mwao? Sisi sote twaweza kushiriki kikamili kukazia umaana wa kuhudhuria Ukumbusho. Kwa kuwa utakuwa Jumapili, itakuwa rahisi zaidi kwa wengi kuhudhuria. Hakikisha unaalika mafunzo yako yote ya Biblia na watu wengine wenye kupendezwa wajiunge nasi. Shiriki nao yaliyoandikwa kwenye ukurasa 127, fungu la 18, katika kitabu Ujuzi kuhusu siku moja ya mwaka ambayo huadhimishwa kipekee.
4 Ona tukio hili kubwa zaidi la 1997 kwa uthamini wa yote ambayo kifo cha Yesu humaanisha kwetu. Uwepo jioni ya Machi 23, Wakristo wote kila mahali waadhimishapo kwa uaminifu Ukumbusho.