Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Kizazi Changu—cha Pekee Sana na Chenye Kupendelewa Sana Sana!
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Agosti 1
    • ukweli?” Bila kusita ninajibu: “Kuona yakitimizwa katika kizazi changu maunabii ya Biblia yaliyoandikwa na wanaume walioongozwa kwa roho na walio wakfu karne nyingi zilizopita.”

      Washiriki wa kizazi changu nje ya tengenezo la kitheokrasi, bila shaka, wamekuwa sawa-sawa kama vile Mchezo wa Kuigizwa wa Uumbaji wa 1914 ulivyosema wangekuwa: wenye kichaa cha pesa, kichaa cha anasa, na kichaa cha umashuhuri. Wale wetu tuliomo ndani ya tengenezo la Bwana tumejaribu, katika kila njia iwezekanayo, kuelekeza fikira zao kwenye ujumbe wa uzima. Tumetumia maneno ya shime, matangazo ya ukurasa mzima, redio, magari yenye kutoa sauti, vinanda vya kuchezea sahani za santuri, mikusanyiko mikubwa, maandamano ya watu wanaotembea wakibeba ishara, na jeshi linaloendelea kuongezeka la wahudumu wa nyumba kwa nyumba na wahubiri penye pembe za barabara za mji. Utendaji huu umetumika kugawanya watu wale wanaopendelea Ufalme wa Mungu uliosimamishwa wakiwa upande mmoja, na wale wanopinga wakiwa upande mwingine. Hii ndiyo kazi aliyotabiri Yesu kwa kizazi changu!—Mathayo 25:31-46.

      Mpaka huu “moyo uliochoka” wangu upige pigo lao la mwisho, utaendelea kupiga katika uthamini wa pendeleo ambalo nimefurahia la kuwa wa kizazi cha pekee sana. Utaendelea kupiga kwa msisimuko juu ya pendeleo ninalo sasa la kuona mamilioni ya nyuso zenye kutabasamu ambazo zimekusudiwa ziendelee kutabasamu milele.

  • Mmoja Aliye Mchanga Amsifu Yehova
    Mnara wa Mlinzi—1987 | Agosti 1
    • Mmoja Aliye Mchanga Amsifu Yehova

      NAFASI nyingi za kutoa ushuhuda ziko wazi kwa walio wachanga wanapokuwa na tamaa yenye nguvu ya kumtumikia Yehova. Hilo lilionekana katika jambo lililoonwa na kivulana mwenye umri wa miaka mitano katika Magharibi mwa Kenya.—Mhubiri 12:1.

      Mamaye alimuuliza: “Unataka kuwa nini utakapokuwa mtu mzima?” Kivulana huyo alikuwa amemwona painia wa pekee katika kundi naye akajibu: “Mimi nataka kuwa painia wa pekee kama Ndugu F .” Mamaye akajibu: “Lakini hilo haliwezekani; wewe huwezi hata kuwa painia wa kawaida kwa sababu wewe huna funzo la Biblia.” Yule kivulana akauliza: “Naweza kufanya nini basi?” Mama yake akamdokezea ajaribu kufundisha wenzake anaocheza nao akitumia nakala yake ya Kitabu Changu cha Hadithi za Biblia.

      Kivulana huyo mwenye umri wa miaka mitano akachukua kitabu chake cha Hadithi za Biblia akaenda kuwaita rafiki zake, akiwaalika wajifunze Biblia pamoja naye. Matokeo yakawaje?

      Yeye alifanyiza kikundi cha watoto kumi ambao angeweza kujifunza pamoja nao. Yeye alitumia vizuri zile picha, akauliza maswali mengi yenye kuchunguza mambo kindani na akauliza maswali ya kurudia mambo waliyojifunza mwisho wa funzo. Ikiwa wao hawakukumbuka, alirudia tena habari hiyo pamoja nao. Mamaye alieleza kwamba ilikuwa furaha kweli kweli kuona watoto hao wote wakiketi chini mbele ya nyumba yake wakijifunza pamoja! Mwanaye mwenye umri wa miaka mitano ndiye huyo akiuliza maswali, kisha mikono yote ingeinuliwa juu kujibu.

      Ilikuwa furaha zaidi kwa mama huyo, na kwa kundi pia, kuona wanane wa watoto hao wakihudhuria mikutano ya kundi. Wale wengine wawili walikuwa wadogo mno. Yote hayo yalitokea kwa sababu kivulana mmoja mwenye umri wa miaka mitano alitaka kumsifu Yehova na kusaidia wengine.

Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki