Wimbo 174
Kaeni Macho, Simameni Imara, Mwe Hodari
1. Muwe macho na imara
Vitani adilifu.
Fanyeni kiumeume,
Ushindi u karibu.
Yesu Gideoni Mukuu,
Twazunguka Wamidiani.
Karibu agizo litoke,
Kukimbiza adui.
2. Muwe macho na akili,
Na tayari kutii.
Kila mutu akitii
Neno la Yesu Kristo.
Mufano wake watufunza
Kukubaliwa na Yehova.
Kama jeshi lenye umoja,
Kumutii Yehova.
3. Uwe macho, vumilia;
Mungojee Yehova.
Aongoza mambo yote;
Hachelewi kutenda.
Kama jeshi la Gideoni,
Amiri atatuambia.
Tii amuri za pigano,
Mungu akatetewe.
4. Tuwe macho na umoja
Kutetea Injili.
Tutii utaratibu
Wa kitheokrasi tu.
Na washikamani tupaze:
“’Panga wa Mungu, Gideoni!”
Tukae macho na imara!
Na hivyo hadi mwisho!