Wimbo 38
Kuonyesha Ushikamanifu
1. Yehova anao watu,
Wapenda jina lake,
Ni kundi shikamanifu;
Lenye wakifu kwake.
Penye meza ya kiroho
Wala kwa shukurani,
Wanamupendeza Yeye
Kwa wazo, neno, tendo.
2. Tutashikamana nalo
Kundi shikamanifu,
Hata wakati wa shida
Twalitii thabiti.
’Talinda faida zalo,
Zisiharibiwe la;
Tukiiona hatari,
Tutapiga king’ora.
3. Tutasaidia ndugu,
Wapya, dhaifu pia,
Katika Funzo, huduma
Kwa fadhili, upole.
Namo katika jamaa,
Hatutazusha shaka,
Kwa kila uhusiano
Tuwe washikamani.
4. Tuwe washikamanifu,
Katika ulimwengu.
Kwao wanaostahili
Ipasavyo Ukristo.
Shetani awe muwongo,
Yehova ni wa kweli.
Ushikamanifu wetu,
Wamupendeza yeye.