Wimbo 96
Kumtukuza Baba Yetu, Yehova
1. Yehova viumbe vyako
Vyakutukuza wewe.
Ulikusudia viwe
Na vinasimulia.
Watoa baraka nyingi,
Zawadi nzuri zote.
Umetabiri, yanatimia
ndani ya Yesu.
Na Yesu aliimbiwa
Na malaika wako.
U mwema, ulitukomboa
kupitia Yesu!
2. Twafurahi Yesu katimiza
utume wake.
Lo! na yeye alishinda
Akabadili hali,
Sasa akiwa Mufalme
Ashika amri zako,
Jina na kusudi lako
Anajulisha kote,
Na sisi tunafurahi
Tunaimba kwa shangwe:
“Bwana Yehova, ataondoa
huzuni yote.”
3. Je! tusiimbe sifa zako,
na kukupendeza?
Tukijiweka wakifu,
Tukuhudumu sana?
Tutetee jina lako
Tufanye kazi yako.
Upendo wetu uzidi,
Pia bidii yetu.
Na tutakutumikia
Milele na milele.
Kuheshimu jina lako
Ndiyo tamaa yetu.