Kikumbusha Chenye Kusaidia
“Katika nchi kadhaa twasikia juu ya ‘vilabu’ au vikundi vya watu wanaokusanya fedha kwa makusudi mbalimbali. Kwa kawaida wao hufanya mikutano inayoendelea au karamu katika nyumba mbalimbali, ambapo wote husaidia familia moja katika kikundi kwa ‘mkopo’ au kusaidia gharama kubwa sana. Ni zipi baadhi ya kanuni za Biblia zinazoweza kuchunguzwa ili kuona msimamo wa Kikristo wa jambo hili? Baadhi yake ni Waefeso 5:3, 5 inayozungumza juu ya pupa, Waroma 13:8 na Mithali 22:7 juu ya kukopa, 1 Wakorintho 15:33 na 2 Wakorintho 6:14, 15 juu ya mashirika na mikataba na vilevile Waefeso 5:18 na 1 Petro 4:3 juu ya kunywa au kufanya karamu na wasioamini. Hayo yapaswa kutosha na kutuwezesha kufikia uamuzi ufaao.”
Sasa miaka mitano imepita tangu kikumbusha hiki kitolewe. Tangu wakati huo wengi wamekubali kweli. Kukiwa na hali ngumu za kiuchumi katika ulimwengu wa leo, wengi wetu watathamini kikumbusha hiki. Mshiriki wa kutaniko anapokuwa na uhitaji, ndugu mmoja-mmoja wanaweza kusaidia. Katika hali fulani, wazee wa kutaniko wanaweza kupanga kutoa msaada fulani.