Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 6/99 uku. 2
  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Juni

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mikutano Ya Utumishi Kwa Juni
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Vichwa vidogo
  • Juma Linaloanza Juni 7
  • Juma Linaloanza Juni 14
  • Juma Linaloanza Juni 21
  • Juma Linaloanza Juni 28
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 6/99 uku. 2

Mikutano Ya Utumishi Kwa Juni

Juma Linaloanza Juni 7

Wimbo 45

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyoteuliwa kutoka katika Huduma ya Ufalme Yetu. Habari za Kitheokrasi.

Dak. 15: “Twafundishwa na Yehova.” Toa utangulizi usiozidi dakika moja, na ufuatishe kwa mazungumzo ya maswali na majibu. Alika wasikilizaji wasimulie baadhi ya manufaa ambazo wamepokea kutokana na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, Shule ya Utumishi wa Painia, Shule ya Huduma ya Ufalme, na kadhalika. Kazia jinsi ambavyo zimesaidia watu wa Yehova waweze kuwa wenye matokeo zaidi katika huduma.

Dak. 20: “Tumia Wakati Wako kwa Matokeo.” Mazungumzo kati ya kiongozi wa Funzo la Kitabu la Kutaniko na mhubiri mmoja au wawili wenye uzoefu ambao wanasimulia jinsi wanavyotumia wakati wao kushiriki kikamili iwezekanavyo katika utumishi wa shambani. Wanaeleza umaana wa ratiba yenye kutumika na kukazia uhitaji wa kuwa nayo. Wanasema jinsi ambavyo wameepuka vipoteza-wakati kama vile kuchelewa kuanza, kukosa kupanga mapema, au kuongea sana wakati wa huduma. Mkifikiria hali za kwenu, toeni madokezo ya jinsi ya kutumia wakati kwa matokeo.

Wimbo 48 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 14

Wimbo 63

Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Ripoti ya hesabu.

Dak. 15: “Kikumbusha Chenye Kusaidia.” Hotuba itolewe na mwangalizi-msimamizi.

Dak. 20: “Je, Waweza Kusaidia?” Mazungumzo na wasikilizaji yakiongozwa na mzee. Tia ndani madokezo ya kusaidia wazazi walio peke yao, yaliyo katika gazeti Amkeni! la Oktoba 8, 1995, ukurasa wa 8-9. Alika wengine waeleze uthamini wao kwa msaada wenye upendo ambao wamepokea kutoka kwa wengine katika kutaniko.

Wimbo 53 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 21

Wimbo 72

Dak. 10: “Matangazo ya kwenu. Ikiwa kutaniko lina nakala za Vijana Huuliza au Ujana akibani, onyesha jinsi vitabu hivyo vinavyoweza kutumiwa kwa matokeo katika huduma, tunapokuta matineja nyumbani.

Dak. 17: Tumia Vizuri Vidio na Kaseti za Drama Inapowezekana. Je, zile vidio 10 na kaseti za drama 11 zilizotolewa na Sosaiti zaweza kutumiwa ifaavyo? Je, wewe na familia yako mmetazama au kusikiliza yoyote kati ya hizo? Pitia vichwa kadhaa, ukikazia jinsi zinavyoweza kuboresha usomaji wetu wa Biblia, kutuimarisha kiroho na kutoa ushahidi mzuri kwa ile kweli. Piga kifupi kaseti mbili au tatu. Waulize wasikilizaji watoe maelezo juu ya vidio au drama ambazo wameona zikiwa na matokeo hasa katika kutia moyo familia zao au kuelekeza wapya kwenye tengenezo. Simulia mambo yaliyoonwa yanayoonyesha matokeo mazuri. (Ona 1999 Yearbook, ukurasa wa 51-52.) Tia moyo wote watumie vizuri vidio na kaseti za drama.

Dak. 18: “Je, Wewe Huona Tu Sura ya Nje?” Hotuba na mazungumzo pamoja na wasikilizaji. Kazia sababu ambazo hutufanya tusikate kauli haraka juu ya watu tunaokuta. Pitia kifupi somo ambalo Yehova alimfundisha Yona, ambaye alihukumu kimakosa wale aliowaona kuwa wasiostahili. (Ona Mnara wa Mlinzi, Agosti 15, 1997, ukurasa wa 21-22, fungu la 17-19.) Alika wasikilizaji watoe maelezo juu ya watu mbalimbali waliowakuta katika eneo, wakisema jinsi walivyodumisha mtazamo ufaao kuwaelekea na kumwachia Yehova awahukumu.

Wimbo 77 na sala ya kumalizia.

Juma Linaloanza Juni 28

Wimbo 85

Dak. 15: Matangazo ya kwenu. Wakumbushe wote watoe ripoti za utumishi wa shambani za Juni. Pitia toleo la fasihi la Julai. Onyesha broshua zipatikanazo kwa wingi kwenu, na udokeze sehemu moja au mbili tunazoweza kukazia katika utoaji wetu. Pia taja vichapo vilivyo toleo la pekee vinavyopatikana kutanikoni. Tia moyo wale ambao hawana vichapo hivi katika maktaba yao ya kitheokrasi wavichukue. Pia tunaweza kutoa vichapo hivi nyumba hadi nyumba na kwenye mafunzo yetu ya Biblia nyumbani. Tia ndani onyesho lililotayarishwa vizuri.

Dak. 13: Kwa Nini Yehova Huruhusu Kunyanyaswa kwa Watu Wake? Hotuba itolewe na mzee, ikitegemea kitabu Mashahidi wa Yehova—Wapiga-Mbiu wa Ufalme wa Mungu, ukurasa 676-677. Kama Yesu alivyotabiri, sisi ‘twachukiwa na mataifa yote.’ (Mt. 24:9) Huenda tukakabili upinzani tunapokuwa hudumani, tunaposhirikiana na watu wa jamaa walimwengu, au kushughulika na watu wasio Mashahidi kazini au shuleni. Kwa njia yenye kujenga, msemaji aeleza sababu inayomfanya Yehova aruhusu mnyanyaso huo au upinzani na jinsi uvumilivu wetu utakavyoongoza kwenye baraka hatimaye.

Dak. 17: Nenda Mahali Palipo na Watu! Hotuba ikitegemea kichapo 1997 Yearbook, ukurasa wa 42-48. Ijapokuwa twapaswa kuendelea kutoa ushahidi nyumba hadi nyumba kwa ukawaida, twatafuta fursa kwa bidii za kutoa ushahidi wa vivi hivi—wakati wowote, mahali popote. Simulia mambo yaliyoonwa kutoka katika Yearbook kuonyesha jinsi ambavyo wengine wamefanya hivyo kwa mafanikio mazuri wanapokuwa ndani ya basi, wanapotembea barabarani au ufuoni, wanapoelekea mahali palipoegeshwa magari, wanapokwenda kwenye vituo vya basi, wanapotumia simu, na wanapoandika barua. Wakati ukiruhusu, alika wasikilizaji wasimulie baadhi ya mambo fulani yaliyoonwa yao wenyewe. Tia moyo wote watumie kwa manufaa kila fursa ya kutoa ushahidi mahali popote palipo na watu.

Wimbo 75 na sala ya kumalizia.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki