Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 12/99 uku. 8
  • Utamwambia Nini Mtu Asiyeamini Mungu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Utamwambia Nini Mtu Asiyeamini Mungu?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Habari Zinazolingana
  • Aliyepinga Kuwapo kwa Mungu Awa Mtumishi wa Mungu
    2015 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Watu Wanaoamini Hakuna Mungu Wanatafuta Wafuasi
    Amkeni!—2010
  • Je, Inawezekana Kuamini Kuna Muumba?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Je, Sayansi Imethibitisha Kwamba Hakuna Mungu?
    Amkeni!—2010
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1999
km 12/99 uku. 8

Utamwambia Nini Mtu Asiyeamini Mungu?

1 “Mimi siamini Mungu,” ndivyo profesa mmoja kutoka Poland alivyomwambia mishonari mmoja Afrika. Hata hivyo, dada huyo aliweza kuwa na mazungumzo pamoja na mwanamke huyo na kumpa kitabu Life—How Did It Get Here? By Evolution or by Creation? Mishonari huyo aliporudi juma lililofuata, profesa huyo alimwambia hivi: “Mimi si mtu asiyeamini Mungu tena!” Alikuwa amesoma kitabu chote cha Creation na akamwomba funzo la Biblia. Unaweza kufanya nini ili ufanikiwe kutolea ushahidi wale ambao husema kwamba hawaamini Mungu? Kwanza, fikiria sababu mbalimbali zinazowafanya watu wadai hivyo.

2 Mambo Yanayochangia Kutoamini: Si wote ambao hawaamini Mungu waliozaliwa hivyo. Wengi wao walikuwa na mazingira ya kidini nao walimwamini Mungu wakati fulani. Hata hivyo, matatizo makubwa ya kiafya au ya familia au ukosefu wa haki wa aina fulani ambao walipatwa nao ulidhoofisha imani yao. Kwa wengine, masomo waliyofundishwa kwenye shule za chuo kikuu yamewaathiri vibaya kuhusu maoni yao juu ya Mungu. Ona vielelezo vifuatavyo vya watu wasioamini Mungu ambao hatimaye walisitawisha itikadi yenye nguvu katika Yehova Mungu na wakawa Mashahidi wake.

3 Mwanamke mmoja kutoka Paris alikuwa amezaliwa na maradhi ya kudhoofisha mifupa. Ijapokuwa alikuwa amebatizwa awe Mkatoliki, alidai kuwa asiyeamini Mungu. Alipouliza watawa kwa nini Mungu alimruhusu azaliwe na ulemavu huo, jibu lao lilikuwa: “Kwa sababu anakupenda.” Alikataa kuamini wazo hilo la kipuuzi. Pia, mfikirie kijana mmoja kutoka Finland ambaye alipatikana kuwa na maradhi yasiyotibika ya misuli naye ikambidi adumu kwenye kiti chenye magurudumu. Mama yake alimpeleka kwa Mpentekoste mmoja aliyedai anatibu wagonjwa. Lakini hakukuwa na tiba ya muujiza. Tokeo likawa kwamba, kijana huyo alipoteza kupendezwa kwake na Mungu na akawa asiyeamini Mungu.

4 Mwanamume mmoja katika Honduras alilelewa akiwa Mkatoliki lakini akajifunza falsafa ya Kijamii na kutoamini Mungu. Akisadikishwa na mafundisho ya chuo kikuu kwamba mwanadamu alitokana na mageuzi, aliacha kabisa kuamini Mungu. Vivyo hivyo, mwanamke mmoja Mmarekani alilelewa akiwa Mmethodisti. Akiwa kwenye chuo kikuu alijifunza masomo ya saikolojia. Itikadi yake iliathiriwaje? Yeye alisema: “Wakati wa kiangazi fulani waliharibu imani yote niliyokuwa nayo kuhusu dini.”

5 Kufikia Mioyo ya Watu Wenye Mioyo Myeupe: Watu wengi ambao husema kwamba hawaamini Mungu wangethamini kujua kama kuna suluhisho la matatizo ya afya mbaya, kutopatana kwa familia, ukosefu wa haki, na kadhalika. Wanapendezwa kwa moyo wote kupata majibu ya maswali kama haya: ‘Kwa nini kuna uovu?’ ‘Kwa nini watu wazuri hupatwa na mambo mabaya?’ na ‘Uhai una maana gani?’

6 Mume na mke wanaoishi Uswisi walilelewa wakiwa wasioamini Mungu. Walipofikiwa na kweli mara ya kwanza, hawakuikubali. Lakini walikuwa na matatizo mabaya sana ya familia nao walikuwa wakifikiri juu ya talaka. Shahidi aliporudi tena, aliwaonyesha wenzi hao kutoka katika Biblia jinsi ya kushinda matatizo yao. Wenzi hao walistaajabia shauri lenye kutumika lililo katika Maandiko, na wakakubali kujifunza Biblia. Ndoa yao iliimarishwa, walifanya maendeleo kiroho, na wakabatizwa.

7 Unaloweza Kumwambia Mtu Asiyeamini Mungu: Mtu akuambiapo yeye haamini Mungu, jitahidi kujua ni kwa sababu gani anasema hivyo. Je, ni kwa sababu ya elimu ambayo amepokea, matatizo ambayo ameyapata, au unafiki wa kidini na mafundisho yasiyo ya kweli? Unaweza kumwuliza: “Je, sikuzote umekuwa na maoni hayo?” au “Sababu ya uamuzi wako ni nini?” Jibu lake litakusaidia uamue jambo la kusema. Mahali panapohitajiwa hoja yenye nguvu, huenda kitabu kinachohitajiwa kiwe ni Je, Kuna Muumba Anayekujali?

8 Unaweza kuendeleza mazungumzo na mtu asiyeamini Mungu kwa kuuliza:

◼ “Je, umepata kujiuliza: ‘Kama Mungu yupo, kwa nini kuteseka ni kwingi mno na ukosefu wa haki ni mwingi mno ulimwenguni?’ [Ruhusu jibu.] Naweza kukuonyesha maoni ya Biblia kuhusu habari hiyo?” Soma Yeremia 10:23. Baada ya kusoma, mwulize maoni yake juu ya andiko hilo. Kisha mwonyeshe ukurasa wa 16 na 17 katika broshua Je! Ulimwengu Usio na Vita Utakuwako Wakati Wowote? Au badala yake, unaweza kutumia sura ya 10 katika kitabu Muumba. Mwombe akubali kichapo hicho na asome habari hiyo.—Ili upate madokezo zaidi, ona kitabu Kutoa Sababu, ukurasa wa 223-224.

9 Kwa kukiri wazi, si watu wote wasioamini Mungu watakaokubali kweli. Lakini kuna wengi ambao huwa tayari kuchunguza maoni mengine. Tumia mantiki, ushawishi na zaidi ya yote, nguvu ya Neno la Mungu uwasaidie waone kweli.—Mdo. 28:23, 24; Ebr. 4:12.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki