Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 2/03 kur. 3-4
  • Hubiri na Kutoa Ushahidi Kamili

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Hubiri na Kutoa Ushahidi Kamili
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • Habari Zinazolingana
  • Wanatakwa—Mapainia-Wasaidizi 2,500
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Je, Tutaufanya Tena?—Mwito Mwingine wa Mapainia-Wasaidizi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Tangazeni Kotekote Sifa Bora za Yehova
    Huduma ya Ufalme—2007
  • Je! Wewe Unaweza Kufanya Upainia Msaidizi?
    Huduma Yetu ya Ufalme—1992
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2003
km 2/03 kur. 3-4

Hubiri na Kutoa Ushahidi Kamili

1 Akiwa “kiongozi na jemedari,” Yesu aliwazoeza wanafunzi wake kwa ajili ya kazi kubwa ya kuhubiri ambayo wangefanya. (Isa. 55:4; Luka 10:1-12; Mdo. 1:8) Mtume Petro alisema hivi kuhusu kazi ambayo Yesu aliwapa: “Alituagiza sisi tuwahubiri watu na kutoa ushahidi kamili kwamba Huyu ndiye aliyeagizwa na Mungu kuwa hakimu wa walio hai na wafu.” (Mdo. 10:42) Tunawezaje kutoa ushahidi kamili?

2 Twaweza kujifunza mengi kwa kuchunguza kielelezo cha mtume Paulo. Alipokutana na wazee wa kutaniko la Efeso, aliwakumbusha hivi: “Sikuepuka kuwaambia nyinyi lolote kati ya mambo yaliyokuwa yenye kuleta faida wala kuwafundisha nyinyi hadharani na kutoka nyumba hadi nyumba. Lakini nilitoa ushahidi kikamili kwa Wayahudi na Wagiriki pia juu ya toba kuelekea Mungu na imani katika Bwana wetu Yesu.” Ajapokabili majaribu, Paulo alijitahidi kuwahubiria habari njema watu wengi iwezekanavyo. Hakuridhika tu kuwaeleza wasikilizaji wake kweli za msingi, bali alijitahidi kuwaambia “shauri lote la Mungu.” Ili kutimiza hilo, alikuwa tayari kujitahidi na kujidhabihu. Aliendelea kusema: “Siifanyi nafsi yangu kuwa kitu chenye thamani sana kwangu, kama tu ningepata kumaliza mwendo wangu na huduma niliyopokea ya Bwana Yesu, kutoa ushahidi kamili kuhusu habari njema ya fadhili isiyostahiliwa ya Mungu.”—Mdo. 20:20, 21, 24, 27.

3 Tunawezaje kuiga kielelezo cha Paulo leo? (1 Kor. 11:1) Kwa kuwatafuta na kuwahubiria habari njema watu wanaostahili wa makabila yote na lugha, na kujitahidi kuwasaidia wanaopendezwa tujapokabili majaribu. (Mt. 10:12, 13) Ili kutimiza hilo ni lazima tutumie wakati wetu, jitihada, na kuwapenda watu.

4 Je, Unaweza Kuwa Painia-Msaidizi? Machi na Aprili inaweza kuwa fursa nzuri ya kutoa ushahidi kamili kwa kufanya upainia msaidizi. Tulitiwa moyo kuona wengi wakijitahidi sana kufanya upainia msaidizi mwaka jana.

5 Dada mmoja mwenye umri wa miaka 80 aliye na matatizo mengi ya afya alichochewa na kitia-moyo kilichotolewa na tengenezo la Yehova. Aliandika hivi: “Kilichochea tamaa niliyokuwa nayo kwa muda mrefu, na kunifanya nihisi kwamba ninapaswa kufanya upainia msaidizi mara nyingine tena.” Aliamua kuweka mradi wa kufanya upainia msaidizi mwezi wa Machi. Alisema: “Kwanza, niliketi chini na kuhesabu gharama. Nikazungumza na binti yangu kuhusu jambo hilo kwa sababu ningehitaji msaada wake. Alinishangaza alipoamua kuchukua upainia msaidizi pia.” Dada huyo mzee alihubiri muda wa saa 52 mwezi huo. “Mara nyingi nilimwomba Yehova aniongeze nguvu nilipoanza kuchoka. Mwishoni mwa mwezi, nilifurahi na kuridhika. Nimemshukuru Yehova mara nyingi kwa kunisaidia. Ningependa kufanya upainia msaidizi tena.” Huenda wengine wakatiwa moyo kufanya upainia msaidizi licha ya matatizo ya kiafya wanaposoma kuhusu shangwe ambayo dada huyo alipata.

6 Ndugu mmoja aliyefutwa kazi ghafula alitumia fursa hiyo kufanya upainia msaidizi. Alipokuwa akifanya upainia msaidizi, bidii yake ya kuhubiri iliongezeka, na kufikia mwisho wa mwezi alikuwa ameanzisha funzo jipya la Biblia. Alisema hivi alipofikiria matokeo aliyopata: “Ulikuwa mwezi wenye kuthawabisha sana.” Alifurahi sana kwa ajili ya mwongozo na msaada wa Yehova! Naam, Yehova alimmwagia baraka nyingi sana kwa sababu ya jitihada yake katika huduma. Yehova atakubariki pia.—Mal. 3:10.

7 Si rahisi kwa wahubiri wengi kufanya upainia msaidizi. Hata hivyo, ndugu na dada wengi wamefanya upainia msaidizi wajapokuwa na madaraka mengi ya familia na magumu ya kibinafsi. Ili kutoa ushahidi kamili, mara nyingi ni lazima tudhabihu wakati na nguvu zetu, lakini tutapata baraka zisizo na kifani.—Mit. 10:22.

8 Machi na Aprili ni miezi inayofaa kufanya upainia msaidizi. Mwezi wa Machi una miisho-juma mitano. Baadhi ya wahubiri wanaofanya kazi wanaweza kufanya upainia msaidizi kwa kuhubiri miisho-juma hiyo na jioni. Kwa kuongezea, unaweza kuhubiri wakati wa sikukuu za mwezi wa Aprili. Huenda wengine wakawa wamefunga shule au wakawa likizoni na wanaweza kutumia pindi hiyo kutimiza takwa la saa 50. Ili kuhubiri muda wa saa 50 mwezi wa Machi au Aprili, je, unaweza kutumia mojawapo ya ratiba zilizoonyeshwa katika makala hii? Zungumza na washiriki wa familia yako na wahubiri wengine kuhusu ratiba yako; bila shaka watatiwa moyo kujiunga nawe katika huduma. Usipoweza kufanya upainia msaidizi, weka miradi hususa miezi hiyo na kuwaunga mkono wale watakaofanya upainia. Panga mambo yako sasa ili uhubiri zaidi miezi ya Machi na Aprili.

9 Onyesha Kwamba Unathamini Ukumbusho: Kila mwaka maelfu ya wahubiri huonyesha kwamba wanathamini fidia kwa ‘kununua kabisa wakati’ ili kufanya upainia msaidizi wakati wa Ukumbusho. (Efe. 5:15, 16) Katika nchi zilizo chini ya ofisi yetu ya tawi, mwaka jana kulikuwa na mapainia-wasaidizi 2,878 mwezi wa Machi na 2,180 mwezi wa Aprili. Kwa hiyo kulikuwa na wastani wa mapainia 2,529 miezi hiyo miwili. Idadi hiyo ni kubwa inapolinganishwa na wastani wa wahubiri 1,340 waliofanya upainia msaidizi katika miezi iliyotangulia ya mwaka wa utumishi uliopita. Wakati huu wa Ukumbusho, tuna nafasi nzuri sana ya kuonyesha pia kwamba tunathamini kabisa dhabihu ya fidia ya Kristo kwa kuhubiri zaidi.

10 Aprili 16 inapokaribia, fikiria Ukumbusho unamaanisha nini kwako. Fikiria mambo yaliyotukia kabla ya kifo cha Kristo na mambo mazito yaliyokuwa akilini na moyoni mwake. Tafakari pia shangwe iliyowekwa mbele yake na jinsi ilivyomsaidia kuvumilia mateso. Fikiria cheo chake akiwa Kichwa cha kutaniko, akiongoza kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi. (1 Kor. 11:3; Ebr. 12:2; Ufu. 14:14-16) Kisha onyesha kwamba unathamini yote ambayo Kristo amekufanyia kwa kushiriki kikamili kazi ya kuhubiri kulingana na hali zako.

11 Watie Moyo Wengine Watoe Ushahidi Kikamili: Wazee na watumishi wa huduma wanaweza kuwatia moyo wengine kwa kufanya upainia msaidizi. Kila mmoja wao ana nafasi nzuri ya kuwasaidia wengine washiriki kikamili katika utendaji huu wa pekee anapohubiri nao katika huduma ya shambani na anapofanya ziara za uchungaji. Sote na tusali kuhusu utendaji huo wa pekee na kuimarisha jitihada zetu za kutoa ushahidi kamili.

12 Ingawa wazee wote na watumishi wa huduma wataunga mkono mipango ya kutaniko ya kuongeza utumishi miezi ya Machi na Aprili, mwangalizi wa utumishi hasa anapaswa kufanya mipango inayofaa ya kuhubiri. Anapaswa kupanga mahali na wakati wa mikutano ya utumishi utakaowafaa wahubiri wengi na kuhakikisha kwamba mipango hiyo inatangazwa kwa ukawaida. Mipango inaweza kufanywa ili kuwe na mikutano kadhaa ya utumishi wa shambani kwa siku, ili wote kutanikoni wapate nafasi ya kushiriki njia mbalimbali za kutoa ushahidi. Wanaweza kuhubiri eneo la kibiashara, barabarani, nyumba kwa nyumba, kufanya ziara za kurudia, na kutoa ushahidi kwa kutumia simu iwezekanapo. Kwa kuongezea, anapaswa kuhakikisha kwamba kuna vichapo, magazeti, na eneo la kutosha miezi hiyo.

13 Toleo la Machi ni kitabu Ujuzi, na tutakuwa na mradi wa kuanzisha mafunzo ya Biblia. Madokezo mazuri ya kutoa kitabu Ujuzi yanapatikana katika nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Januari 2002. Toleo la Aprili ni magazeti Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Jaribu kutumia madokezo yaliyo katika sehemu “Mambo ya Kusema Kuhusu Magazeti.” Wote wanapaswa kujitayarisha vizuri ili kutoa ushahidi kamili.

14 Ni furaha iliyoje kufanya kazi chini ya mwongozo wa kichwa cha kutaniko, Kristo Yesu, na kuwa na pendeleo la kuwahubiria wengine habari njema! Tunapokaribia mwezi wa Machi na Aprili, na tujitahidi tena kufanya miezi hiyo kuwa bora zaidi huku tukitii amri ya Kristo ya kuhubiri na kutoa ushahidi kamili.

[Sanduku katika ukurasa wa 4]

Ratiba Mbalimbali za Kufanya Upainia Msaidizi Mwezi wa Machi na Aprili 2003

Siku Saa

Jumatatu 1 2 — — 2

Jumanne 1 — 3 — — —

Jumatano 1 2 — 5 — —

Alhamisi 1 — 3 — — —

Ijumaa 1 2 — — — —

Jumamosi 5 4 3 5 6 7

Jumapili 2 2 3 2 2 3

Machi 56 56 54 55 50 50

Aprili 50 50 51 53 — —

Je, mojawapo ya ratiba hizi itakufaa?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki