Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w99 12/15 uku. 25
  • Walijipa Ujasiri

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Walijipa Ujasiri
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Habari Zinazolingana
  • Mwige Yesu—Hubiri Kwa Ujasiri
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • ‘Sema Neno la Mungu kwa Ujasiri’
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Je, Wahubiri kwa Ujasiri?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Endelea Kusema Neno la Mungu kwa Ujasiri
    Huduma ya Ufalme—2005
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
w99 12/15 uku. 25

Walijipa Ujasiri

SI RAHISI wakati wote kujipa ujasiri wa kuhubiri. Hata mtume Paulo alisema kwamba pindi moja yeye alijipa ujasiri “kwa kushindana sana.” (1 Wathesalonike 2:2) Je, inastahili “kushindana sana” ili uweze kuhubiri? Si lazima tupate mambo yenye kutokeza, lakini mara nyingi watu wa Mungu hufurahi kwamba wamejipa ujasiri. Ebu fikiria vielelezo vichache.

Tara, msichana mmoja mwenye umri wa miaka minane, alisikiliza kwa makini mwalimu wao alipokuwa akiambia darasa kwamba wakati wa Vita ya Ulimwengu ya Pili, Wayahudi waliokuwa wamefungwa katika kambi za mateso walilazimishwa kuvalia ishara ya Star of David yenye rangi ya manjano kwa ajili ya utambulisho. Tara akajiuliza kama anapaswa kusema kwa ujasiri. “Nikasali macho yangu yakiwa wazi,” yeye akumbuka. Kisha akainua mkono, akasema kwamba Mashahidi wa Yehova pia walikuwa katika kambi hizo, na walilazimishwa kuvalia beji ya rangi ya zambarau yenye pembe tatu. Mwalimu alifurahi akamshukuru. Maelezo ya Tara yakatokeza mazungumzo zaidi pamoja na mwalimu huyo, ambaye baadaye hata alionyesha darasa lote ile vidio Jehovah’s Witnesses Stand Firm Against Nazi Assault.

Nchini Guinea, Afrika Magharibi, Irène, mhubiri mchanga ambaye hakuwa amebatizwa alitaka kuboresha huduma yake. Mishonari aliyejifunza naye Biblia alimtia moyo ajaribu kuwaangushia wanafunzi wenzake shuleni magazeti ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! Irène alisita kwa sababu wanadarasa wenzake hawakuwa wakimsikiliza. Lakini, akiwa ametiwa moyo na mishonari huyo, Irène aliamua kumwendea kwanza mwanafunzi ambaye alionekana kuwa mwenye upinzani zaidi. Irène alishangaa sana kwamba msichana huyo alisikiliza vizuri na kukubali kwa furaha magazeti hayo. Wanafunzi wengine pia waliyakubali. Irène aliangusha magazeti mengi sana mwezi huo kuliko jumla ya magazeti ambayo alikuwa ameangusha kwa miezi mitano iliyotangulia.

Kule Trinidad mzee mmoja alisita sana kumwendea mkuu wa shule ili kumwonyesha jinsi gazeti la Amkeni! linavyoelimisha. Lakini akajipa ujasiri. Yeye asema: “Nilisali nilipokuwa nikiingia kwenye ua. Sikuamini wakati yule mkuu alipoonyesha furaha isivyo kawaida.” Alikubali gazeti la Amkeni! la “Vijana wa Leo Wana Tumaini Gani?” na hata akakubali litumiwe kufundisha darasa. Tangu wakati huo, amekubali magazeti 40 yanayozungumzia mambo mbalimbali.

Akiwa kijana, Vaughn aliona kuhubiri kuwa jambo gumu. “Nilikuwa nashikwa na wasiwasi, natoka jasho mikononi, na kuzungumza haraka-haraka—singeweza kuzungumza polepole.” Hata hivyo, baadaye akawa mhudumu wa wakati wote. Na bado anapata ugumu wa kuzungumza. Pindi moja baada ya kuvunjika moyo akitafuta kazi, alitaka kumtolea mtu fulani ushahidi kwenye gari-moshi, “ili angalau apate mafanikio fulani kwenye siku hiyo mbaya.” Lakini aliwaogopa watu walioonekana kuwa wafanyabiashara mashuhuri waliokuwa katika gari-moshi la chini ya ardhi. Hatimaye, akajipa ujasiri wa kuzungumza na mzee mmoja aliyeketi kando yake. Wakawa na mazungumzo marefu. “Unauliza maswali mazuri sana ilhali wewe ni mchanga,” akasema mfanyabiashara huyo, akiuliza, “Je, wewe ni mwanatheolojia?” Vaughn akajibu, “La, mimi ni mmoja wa Mashahidi wa Yehova.” “Aha,” mtu huyo akasema akitabasamu. “Sasa nimeelewa.”

Mashahidi hao wote—na wengine wengi—wamefurahi kwamba walijipa ujasiri wa kuhubiri. Je, wewe pia utajipa ujasiri?

[Picha katika ukurasa wa 25]

Tara

[Picha katika ukurasa wa 25]

Vaughn

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki