Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/04 uku. 1
  • Ubora wa Hekima ya Mungu

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ubora wa Hekima ya Mungu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari Zinazolingana
  • Thamani Bora Zaidi ya Elimu ya Kimungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Kutumia kwa Yehova “Upumbavu” ili Kuwaokoa Wanaoamini
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1992
  • ‘Lo! Kina cha Hekima ya Mungu!’
    Mkaribie Yehova
  • Hekima ya Kweli Inapaza Sauti Kubwa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2022
Pata Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 1/04 uku. 1

Ubora wa Hekima ya Mungu

1 Watu fulani husema kwamba Mashahidi wa Yehova wanapaswa kujitahidi hasa kuwasaidia wanadamu kuondoa matatizo yanayowapata. Watu hao hukosa kuona ubora wa kazi yetu ya kufundisha Biblia. Ni kama mtume Paulo alivyosema: “Neno juu ya mti wa mateso ni upumbavu kwa wale wanaoangamia, lakini kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu za Mungu.” (1 Kor. 1:18) Kwa kweli tunajua kwamba huduma ya Kikristo ndiyo kazi muhimu zaidi inayofanywa duniani leo.

2 Maisha Bora Sasa: Jitihada za wanadamu za kutatua matatizo hazijafanikiwa kabisa. Sheria hazijakomesha ongezeko la uhalifu. Mikataba ya amani na majeshi ya kulinda amani havijakomesha vita. Mipango ya kusaidia jamii imeshindwa kumaliza umaskini. (Zab. 146:3, 4; Yer. 8:9) Kinyume na hayo, ujumbe wa Ufalme umebadili maisha ya mamilioni ya watu kwa kuwasaidia kuvaa utu mpya unaokubalika kwa Mungu. (Rom. 12:2; Kol. 3:9, 10) Kwa kufanya hivyo, wanafurahia maisha bora sasa.—1 Tim. 4:8.

3 Wakati Ujao Mzuri: Mbali na kutusaidia kukabili matatizo ya maisha kwa mafanikio, hekima ya Mungu hutuwezesha kupangia vizuri wakati ujao. (Zab. 119:105) Hiyo hutuepusha na ubatili wa kujaribu kuurekebisha mfumo wa mambo uliopo. (Mhu. 1:15; Rom. 8:20) Tunashukuru kama nini kwa sababu hatuharibu maisha yetu kwa kufuatilia miradi ambayo ni ndoto tu! Badala yake, tunaelekeza jitihada zetu kwenye ahadi hakika ya Yehova ya “mbingu mpya na dunia mpya” ambamo uadilifu utakaa. Siku ya hukumu ya Yehova itakapofika, itakuwa wazi kwamba wale waliotegemea hekima ya Mungu walifanya uamuzi mzuri.—2 Pet. 3:10-13; Zab. 37:34.

4 Ingawa hekima ya Mungu huenda ikaonekana kuwa jambo lisilowezekana kwa wale waliojiingiza sana katika “hekima ya mfumo huu wa mambo,” kwa hakika hiyo ndiyo njia pekee tunayopaswa kufuata. (1 Kor. 1:21; 2:6-8) Kwa hiyo, tunaendelea kutangaza duniani pote ujumbe unaotoka kwa Mungu, aliye “mwenye hekima peke yake.”—Rom. 16:27.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki