Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • km 1/04 uku. 1
  • Tunaweza Kuwasaidiaje Wenzi Wasio Mashahidi?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tunaweza Kuwasaidiaje Wenzi Wasio Mashahidi?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 1/04 uku. 1

Tunaweza Kuwasaidiaje Wenzi Wasio Mashahidi?

1 Watumishi wengi wa Yehova wana wenzi wa ndoa ambao hupendezwa na Mashahidi na kuvutiwa na kutaniko lakini hujiepusha kuwa watumishi wa Mungu. Mume mmoja alikiri hivi: “Lile wazo la kuhubiri nyumba kwa nyumba lilikuwa kizuizi kikubwa kwangu.” Huenda wengine wakawa na mazoea yasiyopatana na maandiko ambayo wanapaswa kuyaacha, au huenda wakaona kwamba hawawezi kamwe kufuata ratiba ya kitheokrasi yenye mambo mengi kama wenzi wao wanavyofanya. Tunaweza kuwasaidiaje?

2 Onyesha Kupendezwa Kibinafsi: Kupendezwa kibinafsi na watu wengine na kutambua mahangaiko yao kunaweza kuwasaidia waikubali kweli ya Biblia. (Flp. 2:4) Mara nyingi wale ambao hapo zamani hawakuwa wakishirikiana na wenzi wao katika imani hutaja jinsi ambavyo wengine walipendezwa nao. “José, ambaye ni mzee kutanikoni, alipendezwa nami kwa njia ya pekee,” akasema yule mume aliyetangulia kutajwa. “Nafikiri kwamba ni kitia-moyo chake ambacho mwishowe kilinifanya nianze kujifunza kwa bidii.” Mume mwingine anakumbuka kwamba ndugu waliomtembelea walijitahidi kuzungumza juu ya mambo anayopenda. Akasema, “Nilianza kuwa na maoni tofauti kabisa kuhusu imani [ya mke wangu]. Rafiki zake walikuwa watu wenye akili sana ambao walikuwa na uwezo wa kuzungumza kuhusu mambo mbalimbali.”—1 Kor. 9:20-23.

3 Toa Msaada Wenye Kutumika: Huenda wenzi wa ndoa ambao si Mashahidi wakachochewa kupitia msaada wenye fadhili wanaopewa. (Met. 3:27; Gal. 6:10) Wakati mmoja, gari la mume fulani asiyeamini liliharibika, kisha Shahidi mmoja kijana akaja kumsaidia. “Jambo hilo lilinivutia kwelikweli,” anakumbuka. Ndugu mwingine alitumia siku nzima akimsaidia mume asiyeamini wa dada mmoja kujenga ua kwenye shamba lake. Walipokuwa wakifanya kazi na kuzungumza pamoja, walisitawisha urafiki. Majuma mawili baadaye, mwanamume huyo alimwendea ndugu huyo na kusema: “Wakati umefika wa kufanya mabadiliko fulani katika maisha yangu. Je, utajifunza Biblia pamoja nami?” Alifanya maendeleo haraka na sasa yeye ni Shahidi aliyebatizwa.

4 Tunapoendelea kuwatafuta wale wanaostahili katika eneo letu, acheni tuendelee kuwasaidia wale ambao wameoa au kuolewa na waamini wenzetu.—1 Tim. 2:1-4.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki